Muandaaji
wa matamasha ya injili hapa nchini, Alex Msama akizungumza na waandishi
wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo. Kuhusiana na tamasha
la kuombea Amani ya nchi juu ya uchaguzi utakaofanyika Oktoba 25 mwaka
huu hapa nchiini na kushoto ni Mjumbe wa kamati ya maandalizi ya tamasha
la kuombea amani ya nchi yetu kuelekea uchaguzi, Hamis Pembe. Msama pia
aliipongeza serikali kwa kukataza uwanja wa taifa kutumika kufanyia
matukio ya kisiasa. Pia amesema kuwa katika tamasha hilo litahudhuriwa
na wananchi mbalimbali pamoja na wasanii wa nyimbo za injili hapa
nchini.
Baadhi ya waandishi wa habari
wakimsikiliza Alex Msama jijini Dar es Salaam leo. pia amengeza kuwa kwa
waimbaji waliopo tayari kwa tamasha hilo ni pamoja na Boniface Mwaitege
pamoja na Christopher Mwahangira.
Picha na Avila Kakingo Globu ya Jamii.