Mwanafunzi wa kidato cha
tatu katika shule ya Sekondari
ya Istiqama iliyoko mjini Mpanda Mkoa wa Katavi (17) jinalake limehifadhiwa amejeruhiwa
kwa kuchomwa na kisu mara mbili
tumboni na mwanafunzi mwenzake wa
kike (15) wa kidato cha tatu wa shule hiyo kwa kisa cha kugombea mwanaume.
Kwa mujibu wa
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi
Kamishina Dhahiri Kidavashari alisema
tukio hilo la mwanafunzi huyo kuchomwa
kisu tumboni mara mbili lilitokea
hapo Desemba 14 mwaka huu majira ya saa
kumi na mbili na nusu jioni katika eneo
la mtaa wa Kashaulili mjini hapa
Siku hiyo ya tukio mwanafunzi huyo aliyejeruhiwa alimtumia
ujumbe wa mfupi
wa simu ya mkononi ya kumtukana
mwanafunzi mwenzake wa kike wa kidato
cha tatu wa shule hiyo ya Sekondari ya Istiqama akimtaka pia aache mahusiano ya kimapenzi na mwanaume ambae ni mpenzi wake
na aliyejeruhiwa
Alisema kutokana na ujumbe huo wa matusi ulipelekea
siku hiyo wanafunzi hao wa kike
walipokutana kutokee ugomvi baina yao katika eneo hilo la Mtaa wa Kashaulili
Kamanda Kidavashari alieleza ndipo wakati wa
ogomvi huo mwanafunzi huyo alipo
chomwa kisu mara mbili tumboni hari ambayo ilimfanya apige mayowe ya kuomba
msaada na watu waliokuwepo jirani na eneo hilo walifika na kumkamata mtuhumiwa
na kumfikisha kituo cha polisi cha Wilaya ya Mpanda
Kidavashari alisema
majeruhi amelazwa katika
Hospitali ya Wilaya ya Mpanda akiendelea kupatiwa matibabu huku hali yake ikiwa inaendelea vizuri
Mtuhumiwa tayari amefikishwa katika mahakama
ya Wilaya ya Mpanda hapo kujibu mashitaka ya kumchoma kisu mwanafunzi
mwenzake
Chanzo sangafesto.blogspot.com
Chanzo sangafesto.blogspot.com

EmoticonEmoticon