KENYA YATINGA NUSU FAINALI KWA KUIFUNGA RWANDA 1-0, SASA KUCHEZA NA KILI STARS

December 07, 2013

Na Mahmoud Zubeiry, Mombasa
TANZANIA Bara, Kilimanjaro Stars itamenyana na wenyeji, Kenya, Harambee Stars katika Nusu Fainali ya Kwanza ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge Desemba 10, mwaka huu Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.
Mshambuliaji wa Kenya, Haambee Stars, Jacob Keli akiwatoka mabeki wa Rwanda, AmavubiBayisenge Emery kulia na Tubane James kushoto Uwanja wa Manispaa, Mombasa leo.

Hiyo inafuatia Kenya kuifunga Rwanda 1-0 katika Robo Fainali ya pili CECAFA Challenge jioni hii Uwanja wa Manispaa, Mombasa Kenya, bao pekee la beki wa Azam FC ya Dar es Salaam, Joackins Atudo kwa penalti dakika ya 56.
Mapema katika Robo Fainali ya kwanza, Stars iliwatoa mabingwa watetezi, Uganda kwa penalti 3-2 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90.
Robo Fainali nyingine zitachezwa kesho, Ethiopia na Sudan na Zambia na Burundi, Uwanja wa Manispaa pia.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »