UVCCM TANGA KUANZA ZIARA KESHO MKOANI TANGA.

December 07, 2013

IMEWEKWA JUMAMOSI:DESEMBA 7 SAA 6:45 JIONI.

 JUMUIYA wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga(UVCCM) inatarajia kuanza ziara yake kesho kwa mkoa mzima wa Tanga kukutana na viongozi wa umoja huo ngazi za wilaya pamoja na kufanya mikutano ya hadhara.


Akizungumza leo na Blog hii,Mwenyekiti wa Umoja huo,Abdi Makange amesema ziara hiyo itakuwa na lengo la kukutana na mabaraza ya umoja wa vijana kila wilaya ili  kuwekeana mikakati mbalimbali ya kuufanya umoja huo uzidi kuwa imara pamoja na kuwashukuru wajumbe wa umoja huo.



Amesema  suala lengine watakalolifanya katika ziara hiyo ni kuangalia uhai wa jumuiya hiyo kwenye wilaya hizo utakaoendena sambamba na ufunguzi wa matawi ya umoja huo lengo likiwa ni kuuimarisha



Makange amesema ziara hiyo kwa kila wilaya zitakuwa zikihitimishwa na ufanyikaji wa mikutano ya hadhara ambapo wananchi wa wilaya husika watapata nafasi ya kupata sera makini za umoja huo ambazo zitakuwa zikitolewa na viongozi wake.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »