*MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA KAMPENI MPYA YA KUZUIA MALARIA YA M-ZINDUKA

December 05, 2013
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya wasanii wa muziki wa Kizazi kipya 'Bongo Flava', walioshiriki katika kuandaa wimbo wa M Zinduka unaohamasisha kushiriki katika kampeni mpya ya Malaria inayokwenda kwa jina la M Zinduka, baada ya kuizindua rasmi jana usiku kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia kwenye  uzinduzi wa Kampeni ya Kuzuia Malaria inayojulikana kama ‘M-Zinduka’ inayoendeshwa kwa pamoja kati ya Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom,  Tanzania House of Talents na Malaria  no more.  
 Wasanii hao wakiimba wimbo wao waliorekodi wa kampeni ya kuzuia malaria.
 Makamu wa Rais Dkt. Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na wasanii hao.
Makamu wa Rais Dkt. Bilal akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Vodacom.
Picha zote kwa hisani ya Sufianimafotoblog

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »