MECHI YA SIMBA YAACHA PIGO COASTAL UNION.

July 31, 2013
Na Mwandishi Wetu,Tanga.
KATIBU Mkuu wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga,Kassim El Siagi (aliyekaa pichani juu)amesema mechi yao na Simba SC imewaachia pigo licha ya kuibuka na ushindi kutokana na kuwasababishia majeraha washambuliaji wawili mahiri katika timu hiyo baada ya kuumia kwenye mchezo huo.

Akizungumza na Blog hii,El Siagi alisema mechi hiyo ilikuwa nzuri kutokana na wao kuibuka na ushindi lakini wakajikuta pia wachezaji wake hao wakipata majeraha madogo madogo ambayo watalazimika kuyatibu kabla ya kuanza msimu mpya wa ligi kuu hapa nchini.

El Siagi aliwataja washambuliaji hao kuwa ni Crispian Udulla na Keneth Masumbuko ambao kila mmoja kwa wakati wake waliweza kutoa mchango mkubwa sana ambapo masumbuko aliifungia Coastal Union bao la ushindi kwenye mechi yao na URA wakati Crispian Udulla aliweza kuwa mwiba kwenye mecho ya na Simba kwa kuifungia timu hiyo bao.

Aliongeza kuwa malengo yao makubwa ni kucheza mechi nyengine ya kirafiki Iddi Mosi na timu nyengine ambayo wataitangaza baadae baada ya kumalizia mazungumzo yao ambapo yakienda vizuri watacheza na Yanga.

"Malengo yetu msimu ujao ni kuhakikisha tunacheza ligi kwa mafanikio makubwa ikiwemo kuchukua ubingwa wa ligi hiyo kwani hilo linawezakana kutokana na uimara wa kikosi hicho na mshikamano uliopo miongoni mwao "Alisema El Siagi.

Katibu huyo alisema timu hiyo msimu ujao itakuwa tofauti na vile inavyofikiriwa na wadau wa soka hapa nchini kwani usajili ambao wameufanya na wanaotarajiwa kuufanya utakuwa kielelezo tosha cha timu hiyo kuelekea maandalizi yao.

UHURU SELEMAN HUYO AKICHEZA KWA STAIL WAKATI WA MAZOEZI LEO.

MAZOEZI SIO MCHEZO.

KIKOSI CHA COASTAL UNION KIKIWA MAZOEZINI JANA UWANJA WA MKWAKWANI.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »