IMEWEKWA:1:12
Na Oscar Assenga, Tanga.
MASHINDANO ya Pool Table ngazi ya Mkoa wa Tanga yanatarajiwa kuanza
kutimua vumbi leo kwenye ukumbi wa Fax Night Clabu na kushirikisha vilabu kumi
kutoka maeneo mbalimbali mkoani hapa.
Akizungumza jana, Katibu wa Chama cha Pool Table Mkoa wa
Tanga,(TARPA) Shabani Kibelo alisema msimu huu wamejipanga vema kuhakikisha
mapungufu yaliyojitokeza mwaka jana hayajirudii katika mashindano hayo lengo
likiwa ni kupata wachezaji wazuri ambao
wataunda timu mkoa huo.
Kibelo alivitaja vilabu hivyo kuwa ni Hai Pub Club,BP
Muheza,Michael Pub,Tanga Beathing Club na Absam Pool Club ambapo vilabu hivyo
vitakuwa katika kundi A huku kundi likiwa na High Way Club,Spaider
Club,Carribean Club,Kijiti Club na Etu Bomba Fax Club.
Katibu huyo alisema mashindano hayo msimu huu yatafunguliwa
na Afisa Utamaduni wa Halmashauri ya Jiji la Tanga,Peter Semfuko ambapo pia
aliwataka chama hicho taifa kuhakikisha wanawaletea mapema vifaa vya muhimu
ikiwemo meza za kuchezea.
Aidha aliwataka wadau mbalimbali wa mchezo huo kujitokeza kwa
wingi ili kuweza kushuhudia mashindano hayo ambayo mwaka huu yanatarajiwa kuwa
na upinzani mkubwa kutokana na timu shiriki kufanya maandalizi mapema.
Mwisho.