Na Oscar Assenga,Tanga.
MKURUGENZI wa Ufundi wa Klabu ya Coastal Union ya
Tanga,Nassoro Hemed “Binslum amesema timu hiyo haina mpango wa kumsajili mlinda
mlango mwengine isipokuwa waliopo wakishirikiana na Shabani Kado.
Kauli hiyo ya Binslum inafuatia taarifa ambazo zimekuwa
zikieleza kuwa uongozi wa klabu hiyo wana mpango wa kumsajili aliyekuwa mlinda
mlango wa Simba Juma Kaseja katika kipindi hiki na kusema taarifa hizo hazina
ukweli wowote ule.
Binsulum alisema wanachokifanya hivi sasa ni kuangalia wachezaji
wenye uwezo wa kuweza kuiletea mafanikio timu hiyo na sio majina kwani wapo
wachezaji wa aina hiyo ambao hawaweze kuwa msaada katika timu.
Alisema kuelekea msimu mpya wameimarisha safu ya walinda
milango ambapo Shabani Kado atasaidiana na Said Rubawa aliyesajiliwa kutoka
Oljoro JKT na Mansour A.Mansour ambaye walimpandisha kutoka katika kikosi chao
cha pili chini ya umri wa miaka 20.
Mkurugenzi huyo aliendelea kusisitiza kuwa hawajafanya
mazungumzo yoyote na Juma Kaseja pia hawana mpango nae ambapo wao wanasajili
kwa mipango lengo lao likiwa ni kupata mafanikio kwenye msimu mpya wa Ligi kuu
Tanzania bara.
Alisema kabla ya kufanya usajili huo walimu walitoa mipango
yao nao kama uongozi wakaona watekeleze na kueleza kuwa katika kikosi chao
mchezaji huyo hana nafasi kutokana na kuwa na walinda milango mahiri.
Wakati
huo huo uongozi klabu hiyo umemteua Hafidhi Kido kuwa mwandishi wa
klabu hiyo ambaye atakuwa na jumuku la kuhakikisha taarifa za klabu hiyo
zinafika kwa wakati katika vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini
nafasi ambayo aliteuliwa leo(jana).