BOMBO WAIKABIDHI TAASISI YA TADENE JENGO LA CLIF KWA AJILI YA KUFANYA UKARABATI MDOGO

July 12, 2023
Kamati ya Ujenzi ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo 





UONGOZI wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo leo umewakabidhi Taasisi ya Tadene ambao wanafanya kazi kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani kwa ajili ya kufanyia ukarabati mdogo wa sehemu ya eneo la Jengo la Clif ambalo baadhi ya sehemu ya nguzo zake zimeanguka.

Akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo,Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo Dkt Juma Ramadhani alisema kwamba wamewakabidhi jengo hilo ili waweze kufanya ukarabati mdogo.

Dkt Juma alisema kwamba wanatarajia waanze kufanya kazi yao hivi karibuni mara masuala la msamaha wa kodi yatakapokamilika ingawa wanatarajia baadhi ya shughuli zianze kwa sasa.

Alisema wanatarajia shughuli ndogo ndogo za ukarabati huo zianze kabla ya kuanza kupata msamaha wa kodi.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa Taasisi ya Tadene Dkt Ally Fungo alisema kwamba taasisi hiyo kwa kushirikiana na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo wamemkabidhi mkandarasi kutoka kampuni ya Ray Build jengo linalofanyiwa ukarabati ambalo ni la kihistoria lililojengwa 1890.

Alisema jengo hilo lilikuwa likitumika kama sehemu ya mwanzo wa Hospitali ya Rufaa ya Bombo hata kwa ukanda wa Afrika Mashariki wakati huo walikuwa wakitegemea Hospitali hiyo.

“Jengo hili kwa muda mrefu limekuwa likiporomoka kutokana na kutokutumika sawasawa na kutokupata matunzo na mwaka 2011 Desemba kona ya nguzo moja iliporomoka hatua inayotishia jengo zima kuporomoka”Alisema

Dkt Fungo alisema hivyo wanafanya jitihaza za kuhakikisha kona hiyo inakaa sawasawa nguzo nzima inyooke mpaka juu ili iweze kulishikilia jengo wakati wanatafuta msaada wa kulikarabati jengo nzima .














Share this

Related Posts

Previous
Next Post »