.TUTAISHANGAZA DUNIA -TIMU YA JUMUIYA YA MADOLA
TANGA UWASA YATENGA MILIONI 900 KUPUNGUZA UPOTEVU WA MAJI
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shiloo akizungumza kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Rashid Shabani |
Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi inayosimamia usambazaji maji (ATAWAS) Constantine Chiwalo akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo ya Maji Cup |
Na Oscar Assenga,TANGA.
MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) katika mwaka wa fedha 2022/2023 wametenga milioni 990 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali kuhakikisha wanapambana na upotevu wa maji.
Hayo yalisemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Rashid Shabani wakati wa ufunguzi wa Mashindano ya Maji Cup yanayofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Kombezi Jijini Tanga.
Alisema fedha hiyo imetengwa kwa ajili ya kutekeleza kazi mbalimbali zikazopelekea kupunguza upotevu wa maji ambapo mwaka jana ulikuwa wastani wa asilimi 30 kwa kutekeleza hayo hiyo miradi wanaimani watapunguza upotevu huo hadi kufikia asilimia 26 June 2023.
Alisema kazi ambazo wanazilenga kuzifanya ni kuboresha miundombinu kwa ajili ya kuzibiti na kupunguza upotevu wa maji kutoka kwenye mabomba na watanunua na kufunga mita za malipo kabla hizo mita ni za aina yake na hivyo itakuwa mamlaka ya maji ya kwanza kuonyesha aina hiyo ya mita.
“Mita hizi tunatarajia tutaanza kuzifunga mwezi huu uzuri mita hizi kama kuna uvujaji mbele ya mita mteja anapata ujumbe kuna matumizi yanafanyika hebu fuatilia agizo hilo ni la wizara na sisi tunatekeleza kwa sababu tunataka kufunga mita ambazo ni rafiki kwa mtumiaji hiyo ni aina rafiki kwa sababu ina mjali mteja”Alisema
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema wamekuwa wakipokea malalamiko bili kubwa na moja ya chanzo ni maji kuvunja mbele ya mita hivyo hilo litakwenda kutatua hilo tatizo ikiwemo kuendelea kuelimisha jamii juu ya udhibiti wa upotevu wa maji na utoaji wa taarifa kwa mamlaka.
“Tunamshukuru Rais kutoa fedha zilizowezesha kutekeleza miradi mbalimbali ya maji inayolenga kuondoa kero ya maji nchini na nyengine nga imeshaleta mabadiliko makubwa ya utapatikanaji wa huduma ya maji nchini ikiwemo Jiji la Tanga ambapo kwa sasa imefikia asiimia 97”Alisema
Hata hivyo alisema Serikali itoa bilioni 13.31kwa ajili ya kujenga miradi ya maji kuhakikisha wananchi wa Jiji la Tanga wanapata huduma ya maji safi na salama.
Alisema pia wamepenga kutanua mtambo wa kusafisha maji eneo la Mowe ambapo wametenga Bilioni 9.1 na kwa sasa unaendelea na umefikia asilimia 62.
“Lakini pia tumeendeleza mtandao wa mabomba kilimota 17.6 maeneo ya Kichangani,Pongwe,Masiwani na Neema huu ni mradi wa kukabiliana na ugonjwa wa Uviko na umekamilika asilimia 100 ulikuwa na thamani milioni 500”Alisema
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema licha ya hivyo serikali imewezesha fedha kujenga mradi wa maji kufikisha huduma maeneo ya Kibafuta,Mleni ,ndaoya,mpirani na chongoleani na kata ya chongoleani ni eneo pekee la Jiji la Tanga ambalo lilikuwa halina mtandao wa huduma ya maji sasa miundombinu imefika na wananchi na wameanza kupata huduma hiyo ya maji.
“Mradi hu wa kupelekea maji Chongoleani una thamani ya Milioni 918 na utekelezaji mradi umefikia asilimi 90 lakini pia kuna mradi wa kulaza bomba kubwa kuboresha hali ya upatikanaji wa maji katika eneo hilo ”alisema
Alieleza hiyo inatokana na wananchi wa eneo la Chongoleani kupata maji kwa mgawo na serikali imetoa bilioni 2.7 kwa ajili ya kulaza bomba kubwa kutoka eneo la Amboni mpaka Chongoleani ili kuhakikisha wanapata maji muda wote.
Mwisho.
WAZIRI MCHENGERWA AITEMBELEA TIMU YA JUMUIYA YA MADOLA,AIFUNDA
HOMA YA MGUNDA ISIWE KIKWAZO CHA KUTOKULA NYAMA
Mkurugenzi
wa Huduma za Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Hezron Nonga
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dodoma na
kuwaasa watanzania kuwa ugonjwa wa Homa ya Mgunda usiwe kikwazo kwao
kula nyama bali wapate nyama kwenye machinjio rasmi ambapo nyama hizo
zinakaguliwa na mtaalamu wa mifugo kutoka serikalini. (Picha na Edward
Kondela, Afisa Habari – Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Msajili
wa Bodi ya Nyama Tanzania Dkt. Daniel Mushi akizungumza na waandishi wa
habari (hawapo pichani) jijini Dodoma na kuwashauri watanzania wapate
nyama kwenye machinjio rasmi na ipikwe iive vyema kufikia nyuzi joto
sabini (70) kabla ya kula ili kuua vimelea vya ugonjwa wa Homa ya Mgunda
pamoja na kuhakikisha nyama wanayokula kwenye maeneo ya starehe
inachomwa vizuri na kukaushwa damu yake. (Picha na Edward Kondela, Afisa
Habari – Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Mkurugenzi
wa Huduma za Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Hezron Nonga
(kulia) akiwa na Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania Dkt. Daniel Mushi
wakati walipozungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kutoa
ufafanuzi juu ya ugonjwa wa Homa ya Mgunda kwa nyama inayopatikana
kutoka kwenye mifugo hapa nchini, kutokana na uwepo wa baadhi ya taarifa
zisizo sahihi juu ya uwepo wa ugonjwa huo na ulaji wa nyama. (Picha na
Edward Kondela, Afisa Habari – Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Na. Edward Kondela
Serikali imesema
ugonjwa wa Homa ya Mgunda usiwe kikwazo cha watanzania kutokula nyama na
kwamba asilimia tisini ya nyama inayopitia kwenye machinjio rasmi iko
salama.
Akizungumza jijini Dodoma (27.07.2022) kupitia vyombo
mbalimbali vya habari, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo kutoka Wizara ya
Mifugo na Uvuvi Prof. Hezron Nonga amesema, nyama ya mnyama anayechinjwa
kwenye machinjio rasmi huwa inakaguliwa na mtaalamu wa mifugo wa
serikali kabla ya kwenda sokoni ili kuepusha madhara yoyote kwa
binadamu.
Prof. Nonga amebainisha kuwa kutokana na utafiti
uliofanywa umebaini kuwa mnyama ambaye ameathirika na vimelea vya
ugonjwa wa Homa ya Mgunda akitolea mfano wa ng’ombe, nyama yake inakuwa
na rangi ya njano hivyo ni rahisi kwa mtaalam wa mifugo kubaini nyama
hiyo machinjioni na kutoruhusu kupelekwa sokoni.
“Kuchinja
mifugo kwenye machinjio na nyama ikaguliwe na daktari au mtaalamu wa
mifugo wa serikali kwa kuwa tushaona ng’ombe akipata shida ya Homa ya
Mgunda, nyama yake inakuwa na rangi ya njano hivyo mtaalam atagundua
kuwa haifai kwa matumizi ya binadamu, hivyo watanzania watakuwa salama.”
Amesema Prof. Nonga
Ameongeza kuwa njia nyingine ya watanzania
kujikinga na ugonjwa wa Homa ya Mgunda ni kuhakikisha nyama inapikwa
vyema na kuiva ili kuua vimelea vya ugonjwa huo ambavyo vinaishi kwenye
majimaji ya mnyama ambaye ameathirika, ukiwemo mkojo na kinyesi chake.
Aidha,
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.
Hezron Nonga amewataka watanzania kutokula nyama ya wanyama wasiyo rasmi
kwenye chakula akiwemo panya kwa kuwa amebainika kuwa ni moja ya
wanyama ambao wanahusishwa kwa kiasi kikubwa kubeba vimelea vya ugonjwa
wa Homa ya Mgunda na magonjwa mengine.
Amefafanua kuwa ulaji wa
nyama ni muhimu katika mwili wa binadamu kwa kuwa ni chanzo cha Protein
katika daraja la kwanza ikiwa ni pamoja na kinga mwilini, hivyo
watanzania wanatakiwa kula nyama iliyo rasmi katika kundi la chakula,
kununua nyama iliyokaguliwa na mtaalamu wa mifugo wa serikali kwenye
machinjio rasmi pamoja na kuipika nyama hiyo vyema na kuiva ili kuua
vimelea vya ugonjwa wa Homa ya Mgunda pamoja na magonjwa mengine.
Pia,
amewaasa wafugaji kuhakikisha wanachanja mifugo yao dhidi ya magonjwa
mbalimbali ukiwemo ugonjwa wa Homa ya Mgunda ambao umekuwepo kwa siku
nyingi lakini umeanza kuonesha athari kwa binadamu.
Kwa upande
wake Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania Dkt. Daniel Mushi
amewatahadharisha watanzania wanaokula nyama kwenye maeneo mbalimbali
yakiwemo ya starehe kuhakikisha nyama imechomwa na kukauka vizuri na
kutokuwa na damu kwa kuwa ikipikwa vizuri hakuna sababu ya kuogopa
ugonjwa wa Homa ya Mgunda kwa sababu vimelea vyake vinakufa kwenye
mapishi yanayofikia nyuzi joto sabini (70).
Dkt. Mushi amewaasa
pia watanzania kununua nyama kwenye maduka yaliyosajiliwa na kukaguliwa
ambapo nyama iliyokaguliwa inakuwa na mhuri kwenye mguu wa nyuma wa
mnyama na kuwataka kuacha kula nyama kutoka kwenye machinjio yasiyo
rasmi yasiyoeleweka au nyama inayopatikana mitaani kwa bei nafuu kwa
kuwa ni hatari kwa afya ya binadamu.
Ameongeza kuwa ni wajibu
kwa watoa huduma kwenye maduka ya nyama kutakiwa kupimwa afya zao kila
baada ya miezi sita ili wasiwe chanzo cha maradhi mengine kwa walaji wa
nyama wanazouza.
Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Bodi ya Nyama
Tanzania zimelazimika kutoa taarifa juu ya ugonjwa wa Homa ya Mgunda kwa
nyama inayopatikana kutoka kwenye mifugo hapa nchini, kutokana na uwepo
wa baadhi ya taarifa zisizo sahihi juu ya uwepo wa ugonjwa huo na ulaji
wa nyama.
ZAIDI YA WATANZANIA MILIONI 61 KUHESABIWA KWENYE SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA HUU
MKUU wa Mkoa wa Tanga Adam Malima akizungumza wakati wa kikao hicho kushoto ni Kamisa wa Sensa ya Watu na Makazi nchini Anna Makinda na kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Manyema akifuatiwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa
Na Oscar Assenga, TANGA.
ZAIDI ya watanzania Milioni 61 wanakadiriwa kuhesabiwa wakati wa zoezi la Sensa ya Watu na Makazi itakalofanyika Agosti 23 mwaka huu hapa nchini.
Hayo yalisemwa na Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi Anna Makinda wakati wa kikao cha viongozi wa madhehebu ya dini mkoani Tanga,Serikali wakiwemo wakuu wa wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri.
Alisema Sensa ni kitu muhimu kinachoipa Serikali ubora wa kufanya kazi zake na ya mwaka huu itakuwa tofauti kabisa ndio maana wakadiria watanzania milioni 61 hadi 64 kutokana na uzazi walioupata mwaka 2012 walikuwa wakiongeza kwa asilimia 2.9.
Alisema suala la Sensa ni takwa la kisheria na ni ustarabu wa kuendesha serikali mbalimbali ulimwenguni kutokana na kwamba unapokuwa na watu basi uwajue ili uweze kupanga mipango yako vizuri.
“Lengo la Sensa ni kujua idadi ya watanzania kama ham hesabiani itakuwa ni fujo sana kuweza kuendesha nchi hivyo ni jambo muhimu kama kiongozi lazima ujue idadi ya watu wako”Alisema
Alisema kwamba sensa ya mwaka huu itakwenda kidigitali na mpaka sasa sasa makarani waliotenga maeneo wanayo kabisa kwamba kitongoji hiki kina nyumba ngapi na hali gani na kitu gani.
Aidha alisema kutokana na hilo hakuna namna karani wa Sensa anaweza kuruka nyuma ataonekana toka Dodoma na wamechukua picha za Satelite kila nyuma inaonekana kwa maana wanahesabu na majengo pia.
Kamisaa huyo alisema viongozi wa dini wana nafasi kubwa sana kuwasiliana na watu kwa karibu sana hivyo ni muhimu wakatumia nafasi zao kuhamasisha zoezi hilo kwenye madhehebu yao.
“Viongozi wa dini ni mwakilishi wa Mungu ,watu wanawasikilizeni mkisema hawafanyi ubishi na viongozi wa mila pia watu wana watii sana hata waganga wa kienyeji wanaheshimika kama mtu anaweza kulala huko kugaragara hao watu wanaaminika kwa asilimia kubwa”Alisema Kamisaa.
Awali akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Tanga Adam Malima alisema watu ambao watataka kuhujumu zoezi la Sensa watatumia sheria kali dhidi yao kwa sababu watakuwa hawana nia ya maendeleo.
Alisema suala la sensa ya watu na makazi ni jambo muhimu sana hasa kwenye kupanga maendeleo ya nchi na mgao wa rasilimali kwenye sekta mbalimbali nchini ikiwemo afya na ujenzi wa miundombinu na nyengine zote.
Malima alisema huko nyuma zoezi hilo lilikuwa likipata shida kidogo kutokana na kutokufahamu kwamba viongozi wa dini wanasikilizwa sana kwenye maeneo yao hivyo hakikisheni mnalihamasiha.
Alisema viongozi wa dini wana nafasi kubwa katika madhehebu yao kulihamasisha suala hilo ili kuhakikisha waumini wao wanashiriki kwenye zoezi hilo la kuhesabiwa kutokana na kwamba kila mtu anamuamini kiongozi wa kiroho.
Mwisho.
WAZIRI MCHENGERWA AONGOZA KIKAO CHA UJUMBE WA TANZANIA BIRMINGHAM UINGEREZA
VIFARANGA VYA KUKU KUTOKA NJE YA NCHI MWISHO JULAI 30
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), akizungumza kwenye kikao cha wadau wa tasnia ya kuku kilichofanyika jijini Dodoma na kuweka wazi kuwa baada ya tarehe 30 mwezi huu, hakuna vifaranga vya kuku vitakavyoingizwa hapa nchini kutoka nje ya nchi na kwamba serikali haitoi tena vibali vya kuingiza vifaranga hivyo ili kuzuia ugonjwa mafua ya ndege na kulinda wazalishaji wa vifaranga wa ndani ya nchi. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Bw. Stephen Michael ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko akizungumza kwenye kikao cha wadau wa tasnia ya kuku kilichofanyika jijini Dodoma ambapo amesema katika Mpango Kabambe wa Sekta ya Mifugo wa Mwaka 2016 umefanya tathmini na kuainisha kuwa hadi kufikia Mwaka 2031 kutakuwa na upungufu wa nyama kwa tani milioni 1.8 hivyo tasnia ya kuku ni rahisi ikitiliwa mkazo itasaidia katika kuongeza uzalishaji wa nyama nchini. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Sekta ya Mifugo Bw. Evance Ntiyalundura akiwa kwenye kikao cha wadau wa tasnia ya kuku jijini Dodoma ambapo amefafanua hatua mbalimbali katika kukuza tasnia hiyo ikiwemo ya kuimarisha ushirikiano baina ya serikali na wadau wa tasnia. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Hezron Nonga, akiwa mmoja wa washiriki katika kikao cha wadau wa tasnia ya kuku kilichofanyika jijini Dodoma na kuelezea umuhimu wa wadau kujisajili kwenye mfumo ili kutambulika kisheria na namna serikali inavyotoa vibali mbalimbali vya kusafirisha mifugo kikiwemo cha kuku. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Nyanda za Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo Dkt. Asimwe Rweguza akifafanua umuhimu wa matumizi ya vyakula bora vya mifugo hususan vya kuku na kuwakumbusha wazalishaji wa vyakula hivyo kutumia maabara ya Wakala ya Veterinari Tanzania (TVLA) kuhakiki ubora wa vyakula wakati aliposhiriki kikao cha wadau wa tasnia ya kuku kilichofanyika jijini Dodoma. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Msajili wa Bodi ya Nyama nchini Dkt. Daniel Mushi akitolea ufafanuzi ombi la wafugaji wa kuku kuwepo kwa machinjio ya kuku kila wilaya ili kuzuia uuzwaji holela wa kuku na kuwepo kwa bei elekezi ya kuku sokoni, wakati aliposhiriki kikao cha wadau wa tasnia ya kuku kilichofanyika jijini Dodoma. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Katibu wa Chama cha Wadau wa Kuku Tanzania (PAT) Bw. Manase Mrindwa akielezea changamoto za chakula cha kuku kuwa kumetokea ongezeko la bei ya chakula cha kuku hadi kufikia Shilingi Elfu 80 kwa mfuko mmoja kwa mwezi wa Julai kutokana na ongezeko la bei ya mahindi na mashudu ya soya kwenye soko la Tanzania pamoja na kuelezea uwepo wa uhaba wa vifaranga, wakati akisoma taarifa ya chama hicho kwenye kikao cha wadau wa tasnia ya kuku kilichofanyika jijini Dodoma. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Muonekano wa washiriki katika kikao cha wadau wa tasnia ya kuku kilichoandaliwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambapo kimejumuisha menejimenti ya wizara Sekta ya Mifugo, wazalishaji wa vifaranga vya kuku, chakula cha kuku na wafugaji wa kuku ambapo wametoa maoni mbalimbali ya namna ya kuboresha tasnia hiyo na kuomba kuwepo kwa vikao vya namna hiyo mara kwa mara lengo likiwa ni kukuza tasnia. (Picha na Edward Kondela, Afisa Habari - Wizara ya Mifugo na Uvuvi)
Na. Edward Kondela
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema baada ya tarehe 30 mwezi huu, hakuna vifaranga vya kuku vitakavyoingizwa hapa nchini na kwamba serikali haitoi tena vibali vya kuingiza vifaranga hivyo.
Naibu Waziri Ulega amebainisha hayo (22.07.2022) jijini Dodoma wakati wa kikao cha wizara na wadau wa tasnia ya kuku, kujadili namna ya kukuza tasnia hiyo ambapo lengo la hatua hiyo ni utekelezaji wa sheria ya mwaka 2006 ambapo serikali imekuwa ikizuia uingizaji wa vifaranga nchini kutoka nje ya nchi ili kudhibiti ugonjwa wa mafua ya ndege kwa mifugo jamii ya ndege na kulinda wazalishaji wa kuku ndani ya nchi.
Akizungumza wakati akifunga kikao hicho kilichojadili ajenda mbalimbali zikiwemo za upatikanaji wa vifaranga vya kuku, chakula cha kuku na bei ya kuku sokoni, Mhe. Ulega amesema ni mategemeo kuwa serikali haitaona vifaranga vinaingizwa nchini kutoka nje ya nchi na kutaka kuwepo kwa mfumo wa taarifa zinazohusu wazalishaji wa vifaranga vya kuku kuanzia wazalishaji wakubwa hadi wadogo ambao wamesajiliwa na kutoa taarifa serikalini ili kuiwezesha kujua kiwango cha uzalishaji na kuwa na takwimu sahihi juu ya mahitaji ya vifaranga nchini.
“Ni mategemeo yetu ni kutokuona baada ya tarehe 30 mtu anaingiza vifaranga hapa nchini kutoka mahali popote pale, jambo la pili kuwepo na mfumo ambao utasaidia serikali kujua ni kiasi gani cha uzalishaji vifaranga ndani ya nchi yetu ili kujipima uwezo wetu na mahitaji yetu ndani ya nchi.” Amesema Mhe. Ulega
Awali Naibu Waziri Ulega akizungumza wakati akifungua kikao hicho cha wizara na wadau wa tasnia ya kuku amesema tasnia hiyo imekua kwa kasi miaka ya hivi karibuni kutokana na kuwepo kwa soko linalotokana na ongezeko la watu na kipato, ongezeko la uwekezaji na uwepo wa mazingira bora ya uwekezaji katika tasnia ya kuku, urahisi wa kufuga kuku na uwezekano mkubwa wa kuwamiliki kuliko wanyama wakubwa.
Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Bw. Stephen Michael akizungumza kwenye kikao hicho amesema kutokana na umuhimu wa tasnia ya kuku katika Mpango Kabambe wa Sekta ya Mifugo wa Mwaka 2016 umefanya tathmini na kubainisha kuwa hadi kufikia Mwaka 2031 kutakuwa na upungufu wa nyama kwa tani milioni 1.8 hivyo tasnia ya kuku ni rahisi ikitiliwa mkazo itasaidia katika kuongeza uzalishaji wa nyama nchini.
Bw. Michael ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, amesema ufugaji wa kuku ni njia rahisi na ambayo haihitaji maeneo makubwa na miundombinu mingi tofauti na mifugo mingine hivyo kikao hicho ni muhimu kwa kuwa kimeunganisha wadau wa tasnia hiyo pamoja na kutatua changamoto zilizopo kwa kuzingatia uwepo wa taasisi mbalimbali zinazotoa mikopo kwa vijana na akina mama na vikundi mbalimbali ambao wengi wamejizatiti katika biashara ya kuku.
Naye Katibu wa Chama cha Wadau wa Kuku Tanzania (PAT) Bw. Manase Mrindwa amebainisha changamoto za chakula cha kuku kuwa kimefikia hadi Shilingi Elfu 80 kwa mfuko mmoja kwa mwezi wa Julai ambapo kunatokana hasa na ongezeko la bei ya mahindi na mashudu ya soya kwenye soko la Tanzania.
Bw. Mrindwa amebainisha pia changamoto ya kutokea kwa uhaba wa vifaranga kwa wakati fulani wa mwaka, huku mitaani bado viko vifaranga visivyo bora ambavyo vinawafikia wafugaji hususan wafugaji wadogo.
Kikao cha wadau wa tasnia ya kuku kilichoandaliwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kimejumuisha menejimenti ya wizara Sekta ya Mifugo, wazalishaji wa vifaranga vya kuku, chakula cha kuku na wafugaji wa kuku ambapo wametoa maoni mbalimbali ya namna ya kuboresha tasnia hiyo na kuomba kuwepo kwa vikao vya namna hiyo mara kwa mara lengo likiwa ni kukuza tasnia hiyo kwa kuirasimisha na kuwepo kwa machinjio maalum kwa ajili ya kuku na bei elekezi ya kuku sokoni.
Mwisho
WAZIRI MCHENGERWA AMWAGA VIFAA VYA MICHEZO SHULE ZOTE WILAYA YA RUFIJI,AANZISHA LIGI YA SENSA