Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akisalimiana na Rais wa Comoros, Azali Assoumani, kwenye ndege ya
shirika la Ethiopian Airline, wakiwa safarini kueleke Ethiopia, katika
Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU, Waziri Mkuu,
anamwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano huo. Januari 28,
2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga, wakati alipo wasili kwenye
uwanja wa Kimataifa wa ndege wa Addis Ababa, kumwakilisha Rais John
Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa
Afrika AU Nchini Ethiopia. Januari 28, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akisalimiana na Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, kwenye hafla ya miaka
100 ya kumkumbuka Rais wa kwanza wa Afrika Kusini, Nelson Mandela,
iliyofanyika kwenye Hoteli ya Sheraton, Mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu
yupo Nchini Ethiopia kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye
Mkutano huo. Januari 28, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akisainiwa kitabu cha kumbukumbu, cha Rais wa kwanza wa Afrika Kusini,
Nelson Mandela na Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, kwenye hafla ya
miaka 100 ya kumkumbuka Kiongozi huyo, iliyofanyika kwenye Hoteli ya
Sheraton, Mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia
kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano huo. Januari 28,
2018.
Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu