Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala na Serikali za Mitaa ikiwasili katika Hospital ya Kilolo kukagua
ujenzi wa Hospital ya Wilaya.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala na Serikali za Mitaa ikipokea Taarifa ya Ujenzi wa Hospital ya
Wilaya ya Kilolo ilipofanya ziara ya Ukaguzi wa Katika Mradi huo!
Huu ndio muonekano wa Sehemu ya Jengo la Hospital ya Wilaya ya Kilolo inayoendelea kujengwa.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Josephat Kakunda(Pili
Kushoto) akijadili jambo na Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikalinza
Mitaa wakati wa Ziara katika Mradi wa Ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya
Kilolo.
………………
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala na Serikali za Mitaa imepongeza ujenzi wa majengo mbalimbali ya
kutolea huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa.
Kamati hiyo imetoa
Pongezi hizo wakati walipotembelea Kilolo na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali hiyo.
Wabunge wamepongeza kazi inayofanywa na wakandarasi kwani ipo katika ubora mzuri na kiwango cha kuridhisha.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Mwanne Mchemba aliyeongoza
Waheshimiwa hao amesema “naipongeza sana Halmashauri ya Wilaya ya
Kilolo, uongozi na watumishi kwa ujumla kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa
Hospitali ya Wilaya, ujenzi ni wa kiwango cha juu na thamani ya fedha
inaonekana”.
Kamati imeagiza Halmashauri kuhakikisha inakamilisha majengo yote kwa wakati ili huduma ianze kutolewa mara moja.
Ameongeza kuwa ni vizuri kipindi hiki ambacho ujenzi
unaendelea Halmashauri ijipange kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba,
vitendanishi na dawa pamoja na kuajiri watumishi.
Naye Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.
Josephat Kandege ameziagiza Halmashauri zote nchini ambazo hazina
Hospitali za Wilaya zianze taratibu za ujenzi mara moja ili kuimarisha
utoaji wa huduma za afya nchini.
Hadi sasa ujenzi uliofanyika ni wa majengo matano ambayo ni
jengo la wagonjwa wa nje; jengo la maabara; jengo la huduma ya mionzi;
jengo la huduma ya afya ya uzazi na mtoto; na jengo la wagonjwa wa
ndani. Ujenzi wa majengo haya hadi kukamilika unatarajia kutumia kiasi
cha fedha shilingi bilioni 4.4.
Aidha, mradi mzima wa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilolo utagharimu Tsh. Bil 12.