Kamishna Jenerali wa Magereza
nchini Dkt. Juma Malewa akikagua jiko la gesi katika Gereza la Mahabusu
Keko. Jeshi la Magereza tayari limeanza kutekeleza maelekezo ya Serikali
ya kuachana na matumizi ya kuni kwa kutumia nishati ya gesi katika
baadhi ya magereza nchini hivyo kutunza mazingira.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la
Magereza wakiwa katika chumba Maalum, Gereza Keko ambapo chumba hicho
kitatumika katika Uendeshaji wa Mashauli mbalimbali kwa kutumia njia ya
TEHAMA. Uwepo wa mfumo huu utalipunguzia gharama Jeshi la Magereza
katika kuwasafirisha Mahabusu mahakamani na kuwarejesha magerezani.
Kamishna Jenerali wa Magereza
nchini, Dkt. Juma Malewa(katikati) akiwa katika Chumba Maalum ambacho
kitatumika katika uendeshaji wa mashauli kwa kutumia njia ya TEHAMA(wa
kwanza kushoto) ni Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es
Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Noel James(wa kwanza kulia) ni
Mkuu wa Gereza Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah
(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).