Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job
Ndugai (kulia) akisalimiana na Mheshimiwa Saul Amon (kushoto) leo katika
Viwanja vya bunge Mjini Dodoma. Katikati ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe.
Dkt. Tulia Ackson (Mwenye miwani), anaefuata ni Mwenyekiti wa Chama cha
Mapinduzi (CCM) kutoka Mkoa wa Mbeya, Ndg. Jacob Mwakasole na wengine ni
Viongozi Mbali mbali wa Chama cha Mapinduzi kutoka Mkoa wa Mbeya na
Wilaya zake ambao ni wageni wa Naibu Spika wa Bunge.
Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt.
Tulia Ackson (kushoto) akisalimiana na mmoja ya Wajumbe wa Kamati ya
Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kutoka Mkoa wa Mbeya leo katika
Viwanja vya bunge Mjini Dodoma. Kulia ni Mhe. Victor Mwambalasw
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya
Viziwi kutoka Mkoa wa Dodoma pamoja na Shule ya Sekondari Tagamenda
kutoka Mkoa wa Iringa wakifuatilia mijadala inayoendelea ndani ya Bunge
ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya Mafunzo Bungeni.
Viongozi Mbali mbali wa Chama
cha Mapinduzi (CCM) kutoka Mkoa wa Mbeya na Wilaya zake wakifuatilia
jinsi muhimili wa Bunge unavyofanya kazi yake, leo katika ukumbi wa
Bunge Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (wa
saba kulia mbele), Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (wa tisa
kulia mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Mbali mbali wa
Chama cha Mapinduzi (CCM) kutoka Mkoa wa Mbeya na Wilaya yake leo katika
viwanja vya Bunge Mjini Dodoma. Wa nane kulia mbele ni Mwenyekiti wa
Chama cha Mapinduzi (CCM) kutoka Mkoa wa Mbeya, Ndg. Jacob Mwakasole
(PICHA NA OFISI YA BUNGE