|
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku akizungumza na waandishi wa habari kulia ni Katibu wa CUF wilaya ya Tanga,Thobias Haule |
Naibu Meya wa Jiji la Tanga (CUF) Mohamed Haniu akizungumza kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Tanga,Alhaj Mussa Mbaruku kulia ni Katibu wa CUF wilaya ya Tanga,Thobias Haule |
Diwani wa viti maalumu (CUF) akizungumza |
Sehemu ya wanachama wa chama hicho wakifuatilia mkutano huo
CHAMA cha Wananchi CUF wilaya ya Tanga kimekanusha uvumi unaoonezwa kuwa wanajuta uwepo Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku huku kikiwataka wananchi kuwapuuza wanaoeneza taarifa hizo.
Hata hivyo amesema wamesikitishwa na kauli zinazoelezwa kuwa chama hicho kinawaomba radhi wananchi wa Jiji hilo kutokana na mbunge huyo kutokuwa na uwakilishi mzuri bungeni kwani tokea apewe nafasi hiyo amekuwa hodari na shupavu kusimamia maendeleo ya Jimbo hilo.
Hayo yalibainishwa leo na Katibu wa Chama cha CUF wilaya ya
Tanga,Thobias Haule wakati wa mkutano wao na waandishi wa habari uliofanyika jana mjini hapa uliohudhuriwa na mbunge huyo na wanachama wa chama hicho ambapo alisema kuna mambo yanayofanyika ni yasiyokuwa na tija ndani ya chama hicho.
Alisema wao wamechaguliwa kuhakikisha wanawatumikia wananchi na sio kutunishia misuli jambo ambalo linaweza kupelekea kushindwa kuwatumikia wananchi.
“Ndugu zangu waandishi kuna mambo yanafanyika ya kihuni na ndani ya CUF Uhuni hauna nafasi nisema Jiji la Tanga limetulia na Mbunge anafanya kazi na madiwani nao pia ….sisi tumechaguliwa kwa maslahi ya Tanga na sio vyenginevyo “Alisema.
“Kwanza hatujakaa kikao chohote na hatujasema tunaomba radhi wakazi wa Jiji la Tanga eti Mbunge Mussa hana uwezo ...eti hafai tumeshuhudia wabunge wengi wa miaka ya nyuma ambao walikuwa hawaeleze changamoto za wananchi kwenye vikao vya bunge lakini huyu tunaona namna anavyopambana.
Naye Mwanachama wa chama hicho,Jumbe Zahoro alisema wamesikitishwa sana na kauli kuwa wao wanasikitika kwa sababu hawawezi kusikitika kwa kiongozi ambaye wamemteua na baadae kumpigana mpaka atachaguliwa kuliongoza jimbo hilo.
“Nimesikishwa kuona mtu anasimama na kueleza maneno anayoyataka kwa sababu chama hicho kina kanuni na katiba haiwezekani mtu anasimama na kusema tunasikitika kwa mbunge ambaye tumemchagua bila kuangalia chama hicho ni cha watu hilo jambo sio kweli “Alisema.
Alisema sio kweli wao CUF wanasikitika kwa mtu ambaye tumeanza kumteua na baadae kuanza kumchagua jambo ambalo haliwezi kuwaingia akilini watu.
Awali akizungumza,Mbunge Mussa alisema hivi sasa dhamira kubwa ni kuhakikisha anawatumikia wananchi kwa moyo mmoja ili kuweza kusogeza mbele gurudumu la maendeleo kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
“Tanga imerudisha heshima yake kwa kuanza kupokea miradi mbalimbali mikubwa ambayo kwa namna moja au nyingine itakuwa mkombozi kwa wakazi wa Tanga hata mikoa ya jirani hii ni ishara tosha sasa tunarudi kwenye enzi zetu za viwanda “Alisema.
Alisema matarajio hayo hivi sasa yanakwenda sambamba na ujio wa miradi ya Bomba la mafuta,ujenzi wa kiwanda cha saruji eneo la Amboni kitakachomilikiwa na Wachina,ujenzi wa barabara ya
Tanga-Pangani-Saadan hadi Bagamoyo.
Alisema miradi hiyo itafungua fursa za kiuchumi kwa mkoa wa Tanga huku akiwataka wananchi kujiandaa kuchangamkia fursa hizo kwa ili kuweza kujikomboa kwa kuanzisha shughuli mbalimbali ikiwemo ujasiriamali.
Hata hivyo amesema wamesikitishwa na kauli zinazoelezwa kuwa chama hicho kinawaomba radhi wananchi wa Jiji hilo kutokana na mbunge huyo kutokuwa na uwakilishi mzuri bungeni kwani tokea apewe nafasi hiyo amekuwa hodari na shupavu kusimamia maendeleo ya Jimbo hilo.
Hayo yalibainishwa leo na Katibu wa Chama cha CUF wilaya ya
Tanga,Thobias Haule wakati wa mkutano wao na waandishi wa habari uliofanyika jana mjini hapa uliohudhuriwa na mbunge huyo na wanachama wa chama hicho ambapo alisema kuna mambo yanayofanyika ni yasiyokuwa na tija ndani ya chama hicho.
Alisema wao wamechaguliwa kuhakikisha wanawatumikia wananchi na sio kutunishia misuli jambo ambalo linaweza kupelekea kushindwa kuwatumikia wananchi.
“Ndugu zangu waandishi kuna mambo yanafanyika ya kihuni na ndani ya CUF Uhuni hauna nafasi nisema Jiji la Tanga limetulia na Mbunge anafanya kazi na madiwani nao pia ….sisi tumechaguliwa kwa maslahi ya Tanga na sio vyenginevyo “Alisema.
“Kwanza hatujakaa kikao chohote na hatujasema tunaomba radhi wakazi wa Jiji la Tanga eti Mbunge Mussa hana uwezo ...eti hafai tumeshuhudia wabunge wengi wa miaka ya nyuma ambao walikuwa hawaeleze changamoto za wananchi kwenye vikao vya bunge lakini huyu tunaona namna anavyopambana.
Naye Mwanachama wa chama hicho,Jumbe Zahoro alisema wamesikitishwa sana na kauli kuwa wao wanasikitika kwa sababu hawawezi kusikitika kwa kiongozi ambaye wamemteua na baadae kumpigana mpaka atachaguliwa kuliongoza jimbo hilo.
“Nimesikishwa kuona mtu anasimama na kueleza maneno anayoyataka kwa sababu chama hicho kina kanuni na katiba haiwezekani mtu anasimama na kusema tunasikitika kwa mbunge ambaye tumemchagua bila kuangalia chama hicho ni cha watu hilo jambo sio kweli “Alisema.
Alisema sio kweli wao CUF wanasikitika kwa mtu ambaye tumeanza kumteua na baadae kuanza kumchagua jambo ambalo haliwezi kuwaingia akilini watu.
Awali akizungumza,Mbunge Mussa alisema hivi sasa dhamira kubwa ni kuhakikisha anawatumikia wananchi kwa moyo mmoja ili kuweza kusogeza mbele gurudumu la maendeleo kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
“Tanga imerudisha heshima yake kwa kuanza kupokea miradi mbalimbali mikubwa ambayo kwa namna moja au nyingine itakuwa mkombozi kwa wakazi wa Tanga hata mikoa ya jirani hii ni ishara tosha sasa tunarudi kwenye enzi zetu za viwanda “Alisema.
Alisema matarajio hayo hivi sasa yanakwenda sambamba na ujio wa miradi ya Bomba la mafuta,ujenzi wa kiwanda cha saruji eneo la Amboni kitakachomilikiwa na Wachina,ujenzi wa barabara ya
Tanga-Pangani-Saadan hadi Bagamoyo.
Alisema miradi hiyo itafungua fursa za kiuchumi kwa mkoa wa Tanga huku akiwataka wananchi kujiandaa kuchangamkia fursa hizo kwa ili kuweza kujikomboa kwa kuanzisha shughuli mbalimbali ikiwemo ujasiriamali.
EmoticonEmoticon