HALMASHAURI YA MBEYA YAKAMILISHA UTENGENEZAJI MADAWATI WAMKABIDHI MKUU WA MKOA WA MBEYA AYAGAWE KWA SHULE 51

June 11, 2016

 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla akikagua madawati hayo kabla ya kuyagawa.
 Mkuu wa Mkoa, Amos Makalla akigawa madawati hayo.
Halmashauri ya Mbeya imekamilisha utengenezaji wa madawati 5,371 ikiwa ni agizo la Rais kuhakikisha wanafunzi wote wanakaa katika madawati.

Akisema taarifa kwa Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla, mkurugenzi wa halmashauri hiyo Upendo Sanga amesema wamekamilisha maoema utengenezaji madawati mapema kabla ya juni 30 kwenda sambamba na agizo la Mkuu wa mkoa halmashauri zote zikamilishe madawati tarehe 20 juni siku kumi kabla ya tarehe ya mwisho ya mheshimiwa Rais.

Mkuu wa Mkoa amekabidhi madawati 3,746 kwa shule 51 na yaliyobaki ameagiza yaendelee kukabidhiwa kwa Shule zingine.

Amesisitiza halmashauri zote kukamilisha utengenezaji wa madawati ifikapo tarehe 20 Juni.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »