Afisa Mahusiano wa Mo Dewji Foundation,
Zainul Mzige (wa pili kulia) akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi
milioni 100 kwa Mwenyekiti wa mradi ufugaji kuku wa kienyeji katika
kijiji cha Msoga, Michael Mkindo (wa tatu kushoto). Wanaoshuhudia tukio
hilo ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Mh. Ridhiwani Kikwete (wa pili
kushoto), Mkuu wa Wilaya ya ya Bagamoyo, Mh. Majid Mwanga (kushoto) na
Diwani wa kata ya Msoga, Hassan Mwinyikondo (kulia).
Afisa
Mahusiano wa MO Dewji Foundation, Zainul Mzige akisoma hotuba wakati wa
makabidhiano ya mfano wa hundi kwa wafugaji wa kuku wa kienyeji chotara
kutoka kijiji cha Msoga, Chalince mkoa wa Pwani. Wa kwanza kushoto ni
mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya
Chalinze, Majid Mwanga, wa kwanza kulia ni Diwani wa Kata ya Msoga,
Hassan Mwinyikondo.
Mfuko wa MO Dewji umeupatia mradi wa
ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara wa kijiji cha Msoga mkoani Pwani
shilingi milioni 100 kufanikisha uendeshaji wa mradi huo awamu ya
kwanza.
Mradi huo unaokisiwa kuwa na makisio ya
uzalishaji ya sh 2,777,901,500 ulibuniwa mwaka 2013 kwa lengo la
kukabiliana na umaskini kijijini hapo.
Kwa mujibu wa taarifa za mradi makisio ya
mapato kutokana na mauzo ya mayai, vifaranga na kuku baada ya kukoma
kutaga zinakadiriwa kuwa sh 4,913,708,000
Aidha mradi huu unasimamiwa na kufadhiliwa na rais Mstaafu Dk Jakaya Mrisho Kikwete.
Akikabidhi hundi hiyo ya sh milioni 100,
Afisa Mahusiano wa Mo Dewji Foundation, Zainul Mzige alisema kwamba
fedha hizo zitaumika kujenga mabanda 200, ununuzi wa vifaranga, ununuzi
wa chakula cha kuku, chanjo na dawa na malipo kwa wataalamu.
Afisa Mahusiano wa MO Dewji Foundation,
Zainul Mzige akisoma hotuba wakati wa makabidhiano ya mfano wa hundi
kwa wafugaji wa kuku wa kienyeji chotara kutoka kijiji cha Msoga.
Mambo mengine ni utawala, mawasiliano, ununuzi wa chachu za mpunga na vifaa vya chakula na maji.
Mzige alisema pamoja na kutoa fedha hizo
kuunga mkono juhudi za Msoga Poultry Farming Project (MPFP) kuendesha na
kuuendeleza mradi kibiashara, aliwataka wahisaniwa kutambua kwamba
maendeleo ya mradi wao yatategemea sana namna wanavyokuwa makini kutumia
fursa mbalimbali kujiimarisha.
Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita
Mo Dewji Foundation imetumia zaidi ya dola za Marekani milioni 3 kwa
ajili ya kusaidia miradi mbalimbali ya kijamii nchini.
Aidha hivi karibuni Mfuko wa MO Dewji kwa
kushirikiana na kampuni ya Darecha Limited walizindua shindano la Mo
Mjasiriamali lenye lengo la kusaidia kukuza ujasirimali miongoni mwa
vijana.
Shindano ya Mo Mjasiriamali litatoa fursa
ya ukuzaji wa mitaji, ulezi wa wajasiriamali na mitandao ya biashara
kuongeza mwanga, ujasiri na kuzalisha wajasiriamali Tanzania.
Ili kufanikisha nia ya kuwa na
wajasiriamali wengi, shindano hilo linatarajiwa kuwa daraja kwenda kwa
Ofisa Mtendaji, Mohammed Dewji (MeTL Group na mwenyekiti wa Mo
DewjiFoundation) ambapo vijana ambao wanaonekana wana kitu cha kufanya,
lakini hawana msaada watashiriki kwa lengo la kupata msaada katika mfumo
wa mtaji, mtandao na usimamizi wa ukuaji wa shughuli wanayofanya au
kutaka kuifanya ili kuianzisha na kuikuza.
Kwa niaba ya wananchi wa Msoga, mbunge wa
Chalinze, Ridhiwani Kikwete alimshukuru Mwenyekiti wa Taasisi ya Mo
Dewji, Mohammed Dewji kw ufadhili ambao ameufanya kwa wananchi wa kijiji
cha Msogo na kumtaka kuwa na moyo wa kutoa zaidi ili azidi kusaidia
wananchi walio na mahitaji.
Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete
akitoa neno la shukrani kwa MO Dewji Foundation mara baada ya
kukabidhiwa mfano wa hundi ya shilingi 100 kwa ajili ya ufugaji wa kuku
wa kienyeji Chotara.
Alisema kuwa kupitia mradi huo wa ufugaji
wa kuku wa kienyeji chotara, wananchi wa kijiji cha Msoga wataweza
kujikwamua na janga la umasikini na wataendelea kuwa wakiandika maombi
ya miradi mbalimbali ambayo wanataka kuifanya ili kuzidi kutengeza ajira
zaidi kwa wananchi wa Mzoga.
“Tunamshukuru Mohammed Dewji kwa msaada
huu tunaimani utasaidia wananchi wa Mzoga na namuomba asisite kutupokea
muda mwingine tunapokuwa na miradi mingine,” alisema Kikwete.
Nae Mratibu wa Mradi wa ufugaji wa kuku
wa kienyeji chotara (Msoga Poultry Farming Project), Novatus Kailembo
alisema wazo la kuanzisha mradi huo lilitolewa na Rais wa awamu ya nne,
Dkt. Jakaya Kikwete mwaka 2013 ili kusaidia kuboresha maisha ya wananchi
wa Msoga kama kiuchumi, kielimu na kiafya.
Alisema wanataraji kuanza na wanakijiji
300 ukiwa ni mradi wa mfano, awamu ya kwanza ambao wanataraji kuanza
kufanyika katika vitongoji tisa ambavyo ni Hospital, Takalagame, Kota,
Mnazi Mmoja, Tumbi Juu, Tumbi Chini, Kingugi, Mkundi na Mokela.
Mkuu wa Wilaya ya Chalinze, Majid
Mwanga akimshukuru Mwenyekiti wa MO Dewji Foundation, Mohammed Dewji kwa
ufadhili ambao ameutoa kwa wilaya yake kwa ajili ya ufugaji wa kuku wa
kienyeji chotara ambapo ufugaji huo unataraji kufanyika katika kijiji
cha Msoga.