HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA(TANAPA) KUPITIA UJIRANI MWEMA WAKABIDHI MRADI WA MAJI KATIKA KIJIJI CHA ASHIRA WILAYA YA MOSHI

June 03, 2015

Mkuu wa mkoa wa Kilimajaro,Leonidas Gama
akikaribishwa na Mhifadhi Mkuu Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro
(KINAPA)Erastus Rufungulo katika makabidhiano ya mradi wa maji wa
ujirani Mwema uliotolewa na hifadhi za taifa nchni
TANAPA.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
akikata utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi katika tanki la maji la mradi wa ujirani mwema uliotolewa na TANAPA kwa wananchi katika kijiji cha Ashira wilaya ya Moshi vijijini.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama
akisoma kilichoandikwa katika vibao mara baada ya uzinduzi wa mradi
huo.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama
kuashiria uzinduzi rasmi wa mradi huo.
RC ,Gama akinywa maji kwa kutumia mkono mara
baada ya kufungua bomba la maji katika kijiji cha Ashira wilaya ya
Moshi vijijini.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,akimtwisha ndoo
ya maji mmoja wa wakazi wa kijiji cha Ashira katika wilaya ya Moshi
ikiwa ni ishara ya kukabidhi mradi huo wa maji ulifadhiliwa na TANAPA
kupitia mradi wa ujirani mwema.
Tanki la Maji la mradi wa ujirani mwema
uliofadhiliwa na Hifadhi za Taifa ,Tanzania (TANAPA).
Mhifadhi mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima
Kilimanjaro (KINAPA) Erastus Rufungulo akiwasalimia wananchi katika kijiji cha Ashira wilaya ya Moshi wakati wa kukabidhi mradi wa maji wa ujirani mwema uliofadhiliwa na TANAPA.
Baadhi ya wananchi katika kijiji cha Ashira
wilaya ya Moshi vijijini.
Meneja Ujirani mwema wa Hifadhi za Taifa
,Tanzania(TANAPA) Ahmed Mbugi akizungumza kuhusu miradi ya ujirani mwema ambayo TANAPA imekuwa ikiitoa kwa jamii katika kijiji cha Ashira wilaya ya Moshi vijijini.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Ashira
katika wilaya ya Moshi .
Kaimu Mkurugenzi mkuu TANAPA,Ibrahim Musa
akitoa taarifa mbele ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama
kuhusu ujenzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Ashira wilaya ya
Moshi ,
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga
akizungumza wakati wa makabidhiano ya mradi wa maji uliofadhiliwa na
TANAPA kwa ajili ya wananchi wa kijiji cha Ashira wilaya ya
Moshi.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
akiwahutubia wananchi waliofika katika makabidhiano ya mradi wa maji
katika kijiji cha Ashira wilaya ya Moshi ,uliofadhiliwa na hifadhi za
taifa Tanzania (TANAPA) .

Na Dixon Busagaga wa Globu ya
Jamii,Kanda ya Kaskazini, 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »