MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO LEONIDAS GAMA AZINDUA DUKA JIPYA LA KAMPUNI YA SIMU ZA MKONONI YA TIGO.

June 03, 2015

Duka jipya la kampuni ya mawasiliano ya simu
za mkononi,Tigo lafunguliwa mjini Moshi.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa duka jipya la kampuni ya simu za mkononi ya Tigo.wengine wanaoshuhudia toka kulia ni mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga,Meneja huduma kwa wateja kanda ya
kaskazini,Gwamaka Mwakilembe na kushoto ni Meneneja wa Ubora wa Huduma ka wateja ,Mwangaza Matotola.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
akizungumza wakati wa uzinduzi wa duka jipya la kampuni ya simu za mkononi ya Tigo lililozinduliwa mjini Moshi.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga
akifuatilia kwa makini shughuli za uzinduzi wa duka la Tigo katika mji
wa Moshi.
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu za
mkononi ya Tigo,wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas
Gama wakati wa uzinduzi wa duka jipya la kampuni hiyo mjini
Moshi.
Meneja huduma kwa wateja kanda ya
Kaskazini,Gwamaka Mwakilembe akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama wakati akitembelea vitengo mbalimbali ndani ya duka hilo.
Wafanyakazi wa kampuni ya Tigo wakiwa kazini.
Uuzaji wa simu za aina mbalimbali pia ulikuwa ukifanyika katika duka hilo.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
,akifurahia jambo mara baada ya kutembelea ndani ya duka hilo na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na kampuni hiyo ya Tigo.
Meneja huduma kwa wateja Kanda ya
Kaskazini,Gwamaka Mwakilembe akitoa neno la shukurani kwa mkuu wa mkoa
wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama (hayupo pichani)mara baada ya uzinduzi
wa duka jipya la kampuni ya Tigo.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama
akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kampuni ya Tigo muda
mfupi mara baada ya uzinduzi wa duka hilo.
………………………………………….
Na Dixon
Busagaga wa Globu ya jamii Kanda ya Kaskazini.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »