SPLM YAANZA UTEKELEZAJI WA MAKUBALIANO YA ARUSHA

February 07, 2015

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (wa tatu kutoka kushoto) akiwa kwenye mazungumzo na Ujumbe wa Viongozi wa Makundi ya Chama cha SPLM cha Sudan ya Kusini
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (wa tatu kutoka kushoto) akiwa kwenye picha ya na Ujumbe wa Viongozi wa Makundi ya Chama cha SPLM cha Sudan ya Kusini 

Ujumbe wa Viongozi wa Makundi ya Chama cha SPLM cha Sudan ya Kusini yalifanya mazungumzo  na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mjini Dar es Salaam jana.
Mazungumzo haya yalilenga kuandaa utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa mjini Arusha  mwezi wa januari tarehe 21 ambayo yanalenga kuyaunganisha makundi matatu katika chama cha SPLM kurudisha Amani na kuunda Serikali itakayowajumuisha viongozi kutoka makundi yote.
Katika mazungumzo ya jana makundi haya yamekubaliana kuendelea na mkakati  wa utekelezaji wa makubaliano ya Arusha kwa lengo la kuandaa utaratibu wa viongozi  wa makundi yote kurudi Sudan ya Kusini mapema iwezekanavyo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »