“SUMATRA TANGA WAWATANGAZIA KIAMA WAMILIKI WA MABASI MKOANI TANGA”

February 07, 2015



MAMLAKA ya Usimamizi wa Usafiri nchi Kavu na Majini Mkoani Tanga (Sumatra) umewapa muda wa siku mbili wamiliki wa mabasi mkoani hapa kuhakikisha wanahamia kwenye kituo kipya cha mabasi kilichopo kange jijini Tanga ndani ya siku mbili zijazo la sivyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Agizo la hilo lilitolewa na Ofisa Mfawizi wa Sumatra Mkoa wa Tanga, Walukani Luhamba wakati alipofanya ziara ya kutembea kituo hicho kuangali namna ya agizo la Mkuu wa mkoa wa Tanga, Said Magalula namna linavyokwenda.


Alisema kuwa kimsingi wamiliki hao kuendelea kubaki kwenye stendi ya zamani ikiwemo wengine kupaki magari pembezoni mwa ofisi zao zilizopo karibu na maeneo hayo ni kukiuka amri iliyotolewa na mamlaka hiyo hivyo watakaobainika kufanya hivyo baada ya muda uliotolewa watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Aidha alisema licha ya kuchukuliwa sheria kali kwa watakaobainika kukaidi agizo hilo lakini pia watawatoza faini ya sh.lakini mbili (200,000) pamoja na kuvutiwa leseni ili kuweza kuwa fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo.


Ofisa huyo alisema kuwa serikali imetumia fedha nyingi kuhakikisha stendi hiyo inakuwa katika kiwango kizuri kwa ajili ya kupunguza msongamano eneo la mjini kwa kuijenga lakini wao wameshindwa kufikiria suala hilo na kuendelea kubaki mjini.

Awali akizungumza ,Mwenyekiti wa Muungano wa Wasafirishaji wa Daladala  Jijini Tanga,Atwabi Shabani aliwataka wamiliki hao kuhakikisha wanazingatia agizo hilo ili kuweza kuepukana na adhabu wanazoweza kukumbana nazo.

Kwa upande wao baadhi ya madereva wanaofanya safari zao kati ya Tanga na mikoa mengine waliotii agizo hilo waitaka mamlaka hiyo kwa kushiriki Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama barabarani kuhakikisha wanasimamia suala hilo ipasavyo ili kuepusha malalamiko.

Mmoja kati ya madereva hao,Omary Chuchuli alisema kuwa utaratibu huo ni nzuro kwa sababu unaondoa manung;uniko kwa baadhi ya wasafirishaji wengine ambao walikwisha kutii agizo la kuhamia kwenye kituo hicho cha mabasi.


Naye Fadhili Jumanne alisema lazima vyombo vinavyohusika na jambo hilo kuhakikisha vinashirikiana kwa pamoja ili kuweza kuondoa changamoto hiyo iliyopo.


Share this

Related Posts

Previous
Next Post »