Wanaume wa shoka wakilisakata rhumba wakati wa kuwafurahisha mashabiki wa bendi ya Skylight wakati wa mkesha wa eid
Mwimbaji
wa bendi ya Skylght Natasha akiwa anawapa mashabiki vionjo vya nyimbo
za taratibu (kistaarabu) wakati wa mkesha huo wa Eid ndani ya kiwanja
cha Escape One Mikocheni
Bendi
ya waimbaji wakali wa Skylight ikirindimisha baadhi ya nyimbo zao huku
mbele kabisa akiwa anawaongoza wenzake katika uimbaji wa nyimbo hiyo
Sony Samba.
Ashura Kitenge (kushoto) akiwa na Kasongo Junior wa Skylight band wakitoa burudani ya kukata na shoka kwa mashabiki wao ndani ya kiwanja cha Escape One Mikocheni
Sam
Mapenzi ni muimbaji mashuhuri na huwa anajua kukonga nyoyo za watu
hususani katika ule muziki wa Afrika magharibi weee utampenda hata kwa
mkopo, hapo akiwa anaimba kwa kushirikiana na wenzake ndani ya bendi ya
Skylight siku ya mkesha wa Eid.
Hii
siku zote huwa inapatikana ndani ya Skylight tu na sio kwingineko maana
ukihitaji kuburudika njoo tuungane pamoja katika bendi yetu inayoenda
kwa kusikiliza mashabiki zaidi na sio kubagua mashabiki.
Mashabiki sasa zamu yao kulisakata wakati bendi ya Skylight ikiwa inatoa burudani hiyo ndani ya Escape One Mikocheni
Rapa
mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower akiwa katika hatua yake ya
kukusanya mashabiki ili tu waende sawa aisee huyu jamaa ni hatari
jumapili hii atakuwepo pale Escape One Mikocheni bila kukosa sogea
taratibu uje ushuhudie vitu kutoka Skylight band.
Sam
Mapenzi (kushoto) akiwa na Ashura Kitenge wakitoa burudani ya nguvu
ndani ya Skylight band wakati wa mkesha wa kuamkia sikukuu ya Eid
Mmoja wa viongozi wa Bendi ya Skylight Joshua Ndege (katikati) akionyesha umahiri wake sambamba na waimbaji wa bendi hiyo.