AZAM YAFUZU ROBO FAINALI BAADA YA KUIFUNGA TUSKER 1-0
Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
MABINGWA
watetezi, Azam FC wamefanikiwa kuwa timu ya kwanza kufuzu Robo Fainali
za Kombe la Mapinduzi, baada ya usiku huu kuifunga Tusker ya Kenya bao
1-0, katika mchezo wa Kundi B, Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Hadi
mapumziko, tayari Azam walikuwa mbele kwa bao hilo 1-0 lililotiwa
kimiani na mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche baada
ya kuchukua pasi ya Waziri Salum.
|
Mfungaji wa bao pekee la Azam leo, Kipre Tchetche akimtoka beki wa Tusker anayejaribu kulala kuokoa mpira |
|
Wachezaji wa Azam wakimpongeza Kipre Tchetche kulia baada ya kufunga bao muhimu leo Amaan |
Tusker
ndiyo waliouanza mchezo huo kwa kasi na kupeleka mashambulizi langoni
mwa Azam kwa takriban dakika 10, lakini baada ya hapo vijana wa Joseph
Marius Omog wakazinduka na kuanza kuwapeleka Wakenya.
Safu ya kiungo ya timu ya Francis Kimanzi ilizidiwa mno na Azam na kutoa mwanya kwa wapinzani wake kuutawala mchezo.
Kpindi cha pili, Tusker walibadilika mno na kulishambulia kama nyuki lango la Azam, ingawa haikuwa bahati yao kupata bao.
Azam
nayo iliyofanya mabadiliko ya safu yake ya ushambuliaji ikiwatoa Brian
Umony na Joseph Kimwaga na kuwaingiza Muamad Ismael Kone na Seif
Abdallah Karihe iliendelea kushambulia na kukosa mabao kadhaa ya wazi.
Ushindi huo unaifanya Azam ifikishe pointi sita baada ya kucheza mehi mbili, wakati Tusker inabaki na pointi zake tatu.
Kikosi
cha Azam FC leo kilikuwa; Mwadini Ali, Erasto Nyoni/Malika Ndeule dk85,
Waziri Salum, David Mwantika, Aggrey Morris, Kipre Wilfred Michael
Balou, Himid Mao Mkami/Jabir Aziz dk73, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Brian
Umony/Muamad Kone dk57, Kipre Herman Tchetche na Joseph Kimwaga/Seif
Abdallah dk70.
Tusker
FC; Samuel Odhiambo, Anhtony Boki, Luke Ochieng, Martin Kiiza, Lloyd
Wahome, Collins Okoth/Osborn Monday dk58, Andrew Tololwa, Dennis
Nzomo/Frederick Onyango dk57, Jesse Were, Ismail Dunga na Michael
Olonga/Ali Abando dk78.
|
Mshambuliaji
wa Azam FC, Kipre Herman Tchetche kulia akipiga mpira uliompita kipa wa
Tusker FC ya Kenya, Samuel Odhiambo na kwenda nje sentimita chache
kutoka langoni katika mchezo wa Kundi C, Kombe la Mapinduzi usiku wa leo
Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Azam FC ilishinda 1-0 na kuwa timu ya kwanza
kufuzu Robo Fainali ya michuano hiyo. |
|
Kiungo wa Tusker, Michael Olonga akiwatoka wachezaji wa Azam |
|
Seif Abdallah wa Azam akimiliki mpira pembeni ya Martin Kiiza wa Tusker |
|
Salum Abubakar 'Sure Boy' wa Azam Fc akipasua katikati ya Uwanja |
|
Beki wa Tusker akijaribu kumpokonya mpira mshambuliaji wa Azam FC, Kipre Tchetche |
|
Mshambuliaji wa Azam FC, Brina Umony akijaribu kuumiliki vyema mpira mrefu aliotanguliziwa |
|
Kiungo mkabaji wa Azam FC, Kipre Balou akiondosha mpira miguuni mwa mshambuliaji wa Tusker FC |
|
Winga wa Azam FC, Joseph Kimwaga akimuacha chini beki wa Tusker FC |
|
Kikosi cha Tusker FC |
|
Kikosi cha Azam FC |
Share this