HIVI NDIVYO RAIS KIKWETE ALIVYOZINDUA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA MKINGA

July 17, 2014

Mhe. DktJakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa na viongozi wa kitaifa, Mkoa  na Wilaya ya Minga mwishoni mwa wiki wakati akizindua rasmi nyumba mpya za gharama nafuu  ambazo zimejengwa na Shirika la nyumba (NHC) kwa ajili ya  watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga   zinalenga kupunguza kero ya makazi kwa watumishi hao .

 Mhe. Kikwete amekuwa kwenye ziara ya siku moja katika Wilaya hiyo ambapo amepata fursa ya kuongea na wananchi katika mkutano wa hadhara  na kisha kuwafuturisha eneo la malamba jeshini.
 Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Benedick Kilimba  akimuonyesha Rais Jakaya Kikwete michoro ya nyumba ambazo Shirika hilo imezijenga Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga wakati wa uzinduzi  wa mradi wa nyumba za gharama nafuu kwa watumishi wa Wilaya hiyo jana
 Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete akikata utepe kuashiria uzinduzi wa nyumba mpya za watumishi wa halmashauri ya Wilaya ya Mkinga  Mkoani Tanga zilizojengwa na Shirika la nyumba la Taifa (NHC), kulia ni  Naibu Waziri wa Ardhi, nyumba na Maendeleo na Makazi, George Simbachawene  na kushoto ni Mwakilishi wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba  na  watatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa.



Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuashiria kupokea  mashine mpya na za kisasa 40  za kufyatulia  matofali (Hydraform) ambazo Shirika la nyumba la Taifa (NHC)  imezipa Halmashauri zote za Mkoa wa Tanga ili kuwapatia vikundi vya vijana  kuanzisha mradi wa ufyatuaji wa matofali na kuweza kujikwamua kimaisha. Picha na Salim Mohamed-Mwananchi

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »