VIJANA KUANDALIWA KUWA CHACHU YA MAENDELEO YA JAMII
Mkuu wa kitengo cha kozi fupi na ushauri chuo cha Mzumbe Pro. Shiv K. Tripathi akichangia wakati wa majadiliano ya awali jinsi ya kuendeleza vijana kwa maendeleo ya jamii, kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Pro. Elisante Ole Gabriel na kushoto ni Mkuu wa Kampuni ya TATA Africa Holdings (Tanzania) Ltd Bw. Prashant Shukla.
Mkurugenzi
Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi akielezea kuhusu moja ya kituo
cha vijana kinachojishughulisha na ufundi makanika kilichopo Ilonga
Morogoro, kulia ni Mkuu wa Kampuni ya TATA Africa Holdings (Tanzania)
Ltd Bw. Prashant Shukla wakati wa majadiliano ya awali ya kuendeleza
vijana kwa maendeleo ya jamii.
Na Genofeva Matemu (MAELEZO)
Wizara
ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa kushirikiana na kampuni ya
TATA Africa Holdings (Tanzania) Ltd imeadhimia kuanzisha programu ya
kuendeleza maendeleo ya jamii kwa kutumia vijana waliopo katika ajira
mbalimbali kwa kuwajengea uwezo utakaowawezesha kuleta maendeleo katika
jamii yao.
Hayo
yameafikiwa wakati Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo Pro. Elisante Ole Gabriel alipokutana kwa ajili ya
majadiliano ya awali na Mkuu wa Kampuni ya TATA Africa Holdings
(Tanzania) Ltd Bw. Prashant Shukla pamoja na Mkuu wa kitengo cha kozi
fupi na ushauri chuo cha Mzumbe Pro. Shiv K. Tripathi ofisini kwake leo
jijini Dar es Salaam.
Lengo
kuu la majadiliano hayo ni kupata ufafanuzi wa awali na kutambua maeneo
ambayo Wizara itaweza kushirikiana na kampuni hiyo ili kuongeza ajira
kwa vijana haswa ajira ya kujitegemea, pamoja na kuwajengea uwezo vijana
katika masuala ya ujasiriamali, uongozi na ufundi makanika.
“Programu
itakayoanzishwa italenga vijana hususani wale wanaojihusisha na ufundi
makanika, madereva wa daladala, pamoja na waendesha pikipiki kwa maana
ya usalama wao, usalama wa pikipiki na ujasiriamali utakaowawezesha
kujipatia kipato na kuleta maendeleo katika jamii” amesema Pro. Gabriel.
Kwa
upande wake Mkuu wa Kampuni ya TATA Africa Holdings (Tanzania) Ltd Bw.
Prashant Shukla ameiahidi Wizara kushirikiana nayo bega kwa bega muda
wote ili kuhakikisha kuwa tatizo la vijana mitahani linaisha na kuwa na
vijana ambao wanauelewa na uwezo wa kuleta maendeleo katika jamii yao.
Naye
Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi ameitaka kampuni hiyo
kushirikiana na Wizara kwa kuchukua fursa ya kuboresha karakana ya
Ufundi makanika iliyopo katika kituo cha vijana Ilonga Morogoro kama
njia mojawapo ya kuwakomboa vijana na kuleta maendeleo.