SEKRETARIETI YA BUNGE LA KATIBA KUKABIDHIWA UKUMBI BAADA YA KUKAMILIKA KWA MAREKEBISHO KUELEKEA BUNGE LA KATIBA
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiwa na wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge, wakati walipofika kukagua ukumbi huo baada ya kukamilika kwa marekebisho ya ukumbi huo kuelekea Bunge la Katiba, linalotarajia kuanza Feb 18, mwaka huu.
Muonekano wa Ndani ya ukumbi huo baada ya kazi ya uwekaji viti kukamilika
Spika wa Bunge Mhe. Anna Makinda, (katikati) Naibu Spika Mhe. Job Ndugai (kushoto), Katibu wa Bunge (Wa pili Kulia) na Mhe. Hamadi Rashid Mohamed Kulia wakiangalia baadhi ya maboresho yaliyofanywa katika Ukumbi wa Bunge kwa ajili ya Bunge la Katiba.
Spika wa Bunge Mhe. Anna Makinda pamoja na wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge wakiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi walioshiriki kuukarabati ukumbi wa Bunge kwa ajiri ya matumizi ya Bunge la Katiba.
Picha kwa hisani ya Bunge