February 05, 2014
BARAZA LA SANAA ZANZIBAR LATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA SUALA LA UTAMADUNI 
Na Masanja Mabula -Pemba .05/02/2014.

Afisa utamaduni Mkoa wa Kaskazini Pemba Hamad Said Mgau amelitaka Baraza la Sanaa Zanzibar  kusimamia vyema suala la utamaduni  ili kudhibiti upotoshaji wa utamaduni wa asili unaofanywa na baadhi ya wanii hapa nchini .

Amesema kuwa utamaduni wa asili visiwani hapa ikiwemo ngoma ya Msewe imekuwa ikipotoshwa na baadhi ya watu kwa makusudi , hivyo ni vyema kwa Baraza kuwa makini katika kusimamia na kulinda asili ya utamaduni huo .

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake Wete , Mgau amesema kuwa endapo Baraza halitakuwa makini kuwadhibiti watu wanaochafua utamaduni huo , basi vizazi vijavyo vitarithi utamaduni usiolingana na maadili .

"Tunashughudia baadhi ya wanii wanapotosha kabisa uhalisia wa ngoma ya msewe , hivyo ni vyema Baraza la Sanaa kuwa makini na watu wa aina hiiambao wamekusudia kuharibu uahalisia wa sanaa hiyo " alifahamisha Mgau .

Aidha amefahamisha kwamba utamaduni wa asili umekuwa ni kivutoa kwa watalii , na kuongeza kwamba kitendo cha kupotoshwa kunaweza kuleta athari kwa Taifa ikiwa udhibiti wake hautapewa kiupambele .

Hata hivyo ameeleza kwamba Upotoshaji wa Ngoma ya Msewe zaidi umakuwa ukifanywa na wanii nje ya Kisiwa Cha Pemba , na kusema kuwa wnaotaka kuiga kucheza ngoma hiyo ni lazima wafuate taratibu zake .

"Msewe asili yake  ni Mombasa nchini Kenya ,   kwa sasa unachezwa zaidi katika Shehia Kambini katika kijiji cha Kichokochwe lakini kama kuna msanii anataka kuiga ifike kichokochwe na sio kupotosha kwa makusudi " alisisitiza .

Pia Mgau kapongeza usimamizi wa sanaa unaofanywa na kamisheni ya Utamaduni Unguja na Pemba jambo ambalo limeongeza uhasishaji na uimarishaji wa utamaduni Visiwani hapa .

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »