MAJANGILI WAIBUKA UPYA , MMOJA AKAMATWA NA NYAMA YA SWALA KARIBU NA HIFADHI YA RUAHA IRINGA
| Swala wakiwa katika hifadhi |
WAKATI
taarifa ya wizara ya maliasili na utalii iliyotolewa na naibu waziri
mwenye dhamana na wizara hiyo Lazaro Nyalandu kudai kuwa
kumekuwepo na ongezeko kubwa la ujangili wa wanyama katika hifadhi za
Taifa baada ya oparesheni ya tokemeza ujangili kusimama ,jeshi la
polisi mkoani Iringa
linamshikilia mkazi mmoja wa kijiji cha Idodi wilaya ya Iringa
vijijini Bw Kegete Makoga (56) kwa tuhuma za kukutwa na nyara za
serikali ambazo ni nyama ya swala kilo 8 .
Kamanda
wa polisi wa mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi ameueleza mtandao huu leo kuwa tukio hilo lilitokea Desemba
29 majira ya saa
3 usiku katika tarafa ya Idodi karibu na maeneo ya hifadhi ya Taifa
ya Ruaha .
Alisema
kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na askari wa hifadhi ya Taifa ya
Ruaha Iringa ambao walikuwa katika doria katika hifadhi hiyo.
Kamanda
Mungi aliasema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na nyama hiyo ya
Swala baada ya doria ya askari hao na kwa sasa anashikiliwa na jeshi
la polisi kwa uchunguzi zaidi kabla ya kufikishwa mahakamani kwa
kosa la kukutwa na nyara za serikali kinyume na utaratibu.
CHANZO:FRANCIS GODWINBLOG
CHANZO:FRANCIS GODWINBLOG
EmoticonEmoticon