VIONGOZI WA DINI WAKIRI ELIMU NI KIKWAZO CHA UNYANYAPAA KWA WAATHIRIKA

December 17, 2013
IMEWAKWA DESEMBA 17  Na Dege Masoli, Korogwe.
Baadhi  ya viongzi  wa madhehebu mbalimbali ya dini Wilayani hapa, wamekiri kuwa ukosefu wa elimu ya ushauri nasaha  kuhusu  VVU  na  Ukimwi  na jinsi ya kuwahudumia  waathirika  wa ungonjwa  huo iliwafanya kuwa  kikwazo katika mapambano ya unyanyapaa.
Viongozi hao walieleza hayo wakati wa mafunzo ya jinsi ya kushughulikia unyanyapaa,madhara na faida za kutokuwepo kwa unyanyapaa  yaliyoambatana na kupima afya zao kwa hiari, walidai kuwa  kukosa elimu hiyo ili kuliwafanya wawe  kikwazo bila ya wao kujijua.
 
Katika mafunzo hayo ya siku mbili viongozi 30  wa madhehebu ya dini   kutoka maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Korogwe  walipima afya zao  kwa hiari ambapo mtaalamu wa upimaji afya, Joice Mwanga  alisema kuwa maambukizi yalikuwa asilimia 0%  ya washiriki wote.
Wakizungumza na Blog hii, Viongozi hao  walieleza kuwa  zoezi la upimaji wa afya limefanikiwa kutokana na elimu  waliyoipata kuwapa  mwanga wa kujitambua tofauti na walivyokuwa awali ambapo suala la kupima afya lilikuwa ni kinyume na imani na taratibu za dini zao.
“Tumejifunza mengi lakini kubwa ni kutambua  jinsi ya kushughulikia unyanyapaa ndani ya jamii, madhara na faida za kutokuwepo kwa unyanyapaa huo…….  huu ni mwanga kwetu”  alisema Yahaya Yussuph.
Naye  Richard  David  yeye alieleza kuwa  .inawezekana wao walikuwa kikwazo  cha  kupunguza kama siyo kuondoa kabisa tatizo hilo bila ya wao kujua na kwamba sasa wataendeleza  mapambano ya unyanyapaa na upimaji afya kwa hiari huku wakiwa mfano  kwa wengine.
Janeth  Mshana   alibainisha kuwa ukosefu wa elimu ya unyanyapaa na faida za upimaji wa afya  lilikuwa tatizo si kwa waumini pekee lakini pia hata kwa viongozi wa dini lilikuwa ni jambo la miujiza ambalo halikuwa rahisi kulitangaza bayana mbele ya jamii zaidi ya kuegemea katika masuala ya kiimani pekee.
Omari Abdalah   alisema kuwa tatizo hilo lilikuwa kikwazo katika mapambano ya harakati za unyanyapaa na kupima afya  na kwamba baada ya kupata mafunzo hayo  watahakikisha mabadiliko  ndani ya nyumba za ibada na jamii kwa ujumla katika maeneo yao yanapatikana.
Hata hivyo Mwajuma Athuman  alidai kuwa kutokana na elimu waliyoipata wameweka  mkakati wa  kubadilisha mtazamo wa waumini wao  kwa  kutoa elimu  juu  ya  athari za unyanyapaa  kwa  waathirika wa ukimwi  na utambuzi na faida ya kupima afya zao kwa hiari.
Walisema kuwa  wamepata  nguvu na muamko mpya kwani awali walikuwa hawana uwezo wa kujieleza juu ya suala zima la VVU na ukimwi mbele ya waumini wao  jambo walilodai kuwa  sasa si kujieleza pekee  bali na hata kutoa maelezo kwa mtu mwingine, kumuandaa  mtu na majibu  yake  yawe  ya ugonjwa ama uzima na jinsi ya kukabiliana na matatizo aliyonayo.
Alisenma kabla ya mafunzo hayo viongozi wengi wa dini walikuwa na mtazamo tofauti juu ya maambukizi ya VVU na ukimwi na kwamba ilikuwa vigumu kumkabili mtu kutokana na ukweli kuwa uathirika lilionekana ni  tendo la aibu na linaloashiria kifo.
Mratibu wa Mtandao  wa  Viongozi wa dini wanaoishi kwa matumaini nchini, Tanzania  Network  of  Religious  Leaderrs  Living with  or Personally  Aftected by HIV (TANERELA ) ,  Mchungaji  Amin   Sandewa  alisema kuwa mafunzo hayo yamefanyika baada ya  kuonekana kuwepo kwa tatizo la kiuelewa na kulieleza suala zima la HIV kwa viongozi hao..
Sendewa  alieleza kuwa  mtandao  umetoa elimu hiyo kwa viongozi wapatao  30  kati ya  waliyopangwa  kupata elimu hiyo katika Wilaya ya  Korogwe  na kwamba  huo ni mpango mkakati wa Mtandao huo  wa kuwawezesha viongozi kuwa mabalozi wazuri wa mapambano zidi ya ukimwi na kupima unaondelea nchini nzima.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »