KILIMANI FC NA COASTAL UNION -20 1-1.

August 10, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
TIMU ya Kilimani FC ya Zanzibar na Coastal Union U-20 juzi zilishindwa kutambiana baada ya kufungana bao 1-1, katika mchezo wa kirafiki uliofanyika jana kwenye uwanja wa mkwakwani mjini hapa.

Mchezo huo ulikuwa ni miongoni mwa michezo ya maandalizi kwa timu ya Kilimani FC ambayo inashiriki ligi daraja la kwanza visiwani humo kabla ya kuanza msimu mpya.

Timu hiyo ipo mkoani Tanga katika ziara ya kimichezo kwa michezo minne lengo lao likiwa ni kuimarisha undugu kwa timu watakazo cheza nazo wakiwa mkoani hapa kabla ya kuondoka kwenda Mombasa ambapo watacheza mechi nyengine za kirafiki.

Kocha wa timu Kilimani FC ,Bakari Mchunga alisema baada ya kumalizika mechi hiyo ya juzi wataelekea Duga Stars wilayani Mkinga na kuelekea Mombasa kucheza na timu ya Dunga ya Msambweni pamoja na timu ya Nzuri ya Kenya na baadae kurejea mkoani hapa kwenda Maramba wilayani Mkinga kucheza mechi moja ya kirafiki.

Kwa upande wake,Kocha wa timu ya U-20 Coastal Union,Joseph Lazaro alisema mchezo huo ulikuwa ni kukipa makali kikosi hicho ambacho kinajiandaa na msimu mpya wa mashindano ya vijana.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »