TANZANIA YAPIGA HATUA KATIKA VIASHIRIA VYA AFYA YA MAMA NA MTOTO, TAKWIMU ZA VIFO ZASHUKA

January 05, 2024

 



Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu amesema taarifa za utafiti wa Demographia ya Afya ya Uzazi na Viashiria vya Malaria (TDHS/MIS) ya mwaka 2022 zinaonesha kuwa Tanzania imepiga hatua katika viashiria vingi vya afya ya mama na mtoto.

Ametoa mfano kuwa Vifo vitokanavyo na Uzazi vimeshuka kutoka 556 kwa kila vizazi hai 100,000 mwaka 2015/16 hadi 104 kwa kila vizazi hai 100,000 na vifo vya Watoto chini ya miaka mitano vimeshuka kutoka 67 kati ya vizazi hai 1000 mwaka 2015/16 hadi 43 kwa kila vizazi hai 1000. Hii ni sawa na kupunguza vifo vya kinamama wajawazito kutoka 11,000 hadi vifo 2,500 kwa mwaka.

Waziri Ummy Mwalimu ameyasema hayo Leo wakati usinduzi wa usambazaji wa vifaa vya uboreshaji wa huduma za mama na motto uliofanyika kwenye makao Makuu ya Bohari ya Dawa MSD jijini Dar es Salaam Leo Ijumaa Januari 5,2024.

Amesema hizi ni jitihada zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wadau wa afya katika kuhakikisha kuwa Nchi yetu inafikia malengo ya kitaifa na kimataifa kama vile malengo endelevu ya Milenia 2030 yanayotutaka kupunguza athari za vifo vitokanavyo na uzazi hadi kufikia vifo chini ya 70 katika kila vizazi 100,000 vifo vya Watoto chini ya 38 katika kila vizazi hai 1,000 pamoja na vya Watoto chini 12 katika vizazi hai 1,000.


Ummy Mwalimu ameongeza kuwa serikali imeendelea kuwekeza katika afya ya mama na mtoto kwa kujenga vituo vya huduma za upasuaji wa kumtoa mtoto tumboni (CEmONC) kutoka vituo 340 mwaka 2021 hadi kufikia vituo 523 mwaka 2023. Maboresho ya upatikanaji huduma hizi katika vituo vya kutolea huduma za afya yamesogeza huduma hizo za upasuaji karibu na wananchi. zaidi ya asilimia 75 85 ya wananchi wanapata huduma za Afya ndani ya Kilometa 5 ndani ya maeneo wanayoishi.

Amesema hali kadhalika Serikali imeendelea kuwekeza katika Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto kwa kujenga Wodi za uangalizi maalumu (NCU za watoto wachanga) zinazohudumia watoto wachanga walio mahututi kwa mara mbili zaidi kutoka 99 mwaka 2021 hadi 189 mwaka 2023. Hizi ni hatau zinazochukuliwa na Serikali katika kutoa huduma bora za afya na kuokoa maisha ya watoto wanaozaliwa wakiwa chini ya kilo moja.
Sambamba na kuboresha huduma hizo Serikali imeendelea kununua na kusambaza vifaa tiba na dawa hivyo kuongeza wigo wa upatikanaji bidhaa za afya ya uzazi kutoka asilimia 82.5 mwaka 2022 hadi kufikia asilimia 88.2 mwaka 2023.

Aidha amesema Serikali imeendelea kuajiri na kupeleka watumishi wenye sifa katika Vituo vya kutolea huduma za afya nchi nzima kuajiri watumishi wa afya wapatao 28,759 hadi kufikia mwaka 2023.

Akizungumza kuhusu kuhusu Vitanda vua kutolea huduma za afya ya Uzazi, Serikali kwa kushirikiana na wafau amesema selikali imeendelea kuboresha upatikanaji wa vifaatiba hivyo kwa ajili ya huduma za afya ya uzazi ambapo hali ya vitanda vya kutolea huduma kwenye vituo vya afya imeongezeka kutoka vitanda 84,162 (mwaka 2021) hadi vitanda 104,687 (mwaka 2023).

Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ununuzi wa vifaa tiba hivi ambavyo vina thamani ya TZS 14,953,854,357 ambavyo ni vitanda vya wagonjwa (3080), vitanda vya kujifungilia (1000), magodoro (5500), mashuka (36808), meza za vitanda (overbed table) 306. Vifaa hivi vitasambazwa katika Majimbo yote 214 nchini Tanzania Bara.

Aidha wizard inategemea kupokea vifaa tiba vingine hivi karibuni ambavyo ni vitanda vya kujifungulia (4280), vitanda vya kufanyia uchunguzi (examination table) 4280, mkoba wa vifaa vya kujifungulia (delivery kit) 4280, kabati za vitanda (bed side lockers) 6420 na stendi ya dripu (6420).

Amesema wizara itagawa kila jimbo vifaa hivyo ambapo Kila jimbo litapata Vitanda 30; Magodoro 30; Mashuka 60; Bed side locker 30; Drip Stand 30; Meza ya kulia chakula 15; Vitanda vya kujifungulia 10; Delivery set 10 pamoja na Examination bed 10. Waheshimiwa Wabunge watavikuta vifaa hivi kwenye vituo viwili katika kila jimbo ambako MSD watashusha mzigo.

Waziri Ummy amesema ana imani kwamba, vifaa hivi vilivyotolewa leo vitachangia katika kuboresha zaidi huduma hizi za mama na mtoto. Aidha ametoa rai kwa Bohari ya dawa kuhakikisha vifaa tiba hivi vinasambazwa kwa wakati.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »