WENZA WA VIONGOZI WAZINDUA HUDUMA ZA TAULO ZA KIKE MASHULENI

August 08, 2023

 

Mama Zakhia Bilal akigawa taulo za kike kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Mtoni wilayani Temeke. (Picha kwa hisani ya Manispaa ya Temeke).

Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akikata utepe kuzindua mradi wa ukarabati wa vyoo vya wasichana na uwekaji wa taulo za kike katika Shule ya Msingi Mtoni wilayani Temeke.
Wenza wa viongozi wakiongozwa na Mama Tunu Pinda (wa kwanza kushoto) na Mama Mary Majaliwa (wa tatu kutoka kushoto mstari wa mbele).
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Mobhare Matinyi, akimshukuru Mama Celina Retala, Afisa Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha HQ Psds cha taulo za kike kilichopo wilayani Temeke.

 

Na Khadija Kalili

ASASI ya wenza wa Viiongozi nchini iitwayo Ladies of New Millenium, leo Agosti 7, 2023, imezindua mradi wa choo kwa ajili ya kusaidia watoto wa kike ili waweze kujisitiri na kupata huduma zote wanazozihitaji wakiwa kwenye hedhi.

Uzinduzi huo umefanywa na mlezi wa asasi hiyo, Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa, umefanyika katika Shule ya Msingi Mtoni, Wilayani Temeke, na kushuhudiwa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mheshimiwa Mobhare Matinyi.

Mheshimiwa Matinyi ametoa shukrani za dhati kwa taasisi hiyo kwa kukikarabati choo cha watoto wa kike na kuwezesha kupata huduma hiyo muhimu.
Mheshimiwa Matinyi amewashukuru pia wadau mbalimbali akiwemo Bi Celina Godfrey Retala, Afisa Mtendaji Mkuu wa HQ Pads kwa kuchangia katoni 100 za taulo za kike kwa ajili ya watoto kujihifadhi wakati wa hedhi.

DC  Matinyi ametoa wito kwa watu na wadau wengine kuunga mkono juhudi hizi ili kumuwezesha mtoto wa kike kupata elimu bora bila usumbufu na kuleta mafanikio hapo baadaye kwa jamii.

 Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, ndugu Victor Kangati, ameipongeza asasi hiyo kwa kuleta mradi huo kwani ni miongoni mwa mbinu kubwa zinazosaidia kupunguza utoro kwa watoto wa kike.

Taasisi hiyo yenye lengo la kuwawezesha vijana na watoto kupitia elimu yenye ufanisi na ujumuishwaji katika ngazi zote za maamuzi, imeendesha hafla hiyo na kuhudhuriwa na wake wa viongozi  akiwemo mlezi wa taasisi, Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa, Mwenyekiti wa taasisi Mama Tunu Pinda na wenza wengine wa viongozi wakiwemo Mama Zakhia Bilal, Mama Asha Bilal, Mama Asina Kawawa na Mama Asha Balozi na Mama Mwantumu Mahiza.

Wadau wa maendeleo Aga Khan Foundation, HQ Pads, na Tosh Cargo .

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »