Nsekela aongoza harambee shule za Marian, Bagamoyo

April 29, 2023

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kulia) akilisalimiana na Askofu Mkuu mstaafu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Kadinali Polycarp Pengo wakati alipowasili kwenye viwanja vya michezo vya Bongololo vya Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Marian mjini Bagamoyo, alipokuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Marian inayojengwa pamoja na zahanati, katika eneo la Mlingotini, wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani. Kushoto ni Mwanzilishi wa Shule za Marian, Father Valentino Bayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela ameongoza harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Marian inayojengwa pamoja na zahanati, katika eneo la Mlingotini, wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani.

Harambee hiyo iliyofanyika leo katika viwanja vya michezo vya Bongololo vya Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Marian mjini Bagamoyo ilisindikizwa na shughuli tofauti ikiwamo riadha, ibada maalumu ya kumshukuru Mungu pamoja na maonyesho ya wanafunzi.
Katika mchango wake, Nsekela alisema kuwa Benki ya CRDB imetoa Sh20 milioni kama sehemu ya mchango wa kufanikisha ujenzi huo huku yeye mwenyewe akichangia Sh10 milioni na marafiki zake wakitoa zaidi ya Sh10 milioni zitakazotumika kumalizia ujenzi wa madarasa shuleni hapo na miundombinu ya zahanati.

“Elimu ni moja ya kipaumbele cha Benki ya CRDB. Kila mwaka, tunatenga asilimia moja ya faida yetu baada ya kodi kusaidia utekelezaji wa miradi ya kijamii ikiwamo ya elimu na afya. Mwaka jana, tulitumia zaidi ya Sh366 milioni kwenye elimu na zaidiya Sh403 milioni kwenye afya. Tunafanya hivi tukiamini Serikali pekee haiwezi kukidhi mahitaji makubwa yaliyopo nchini hivyo ushiriki wa taasisi za dini na sekta binafsi ni muhimu,” amesema Nsekela.

Nsekela aliyekuwa mgeni rasmi kwenye harambee hiyo, alitoa mchango huo baada ya Father Valentino Bayo, mwanzilishi wa shule za Marian kumweleza kuwa jitihada zao za kuielimisha jamii hasa watoto wa mwambao wa Pwani zinakwama kidogo kutokana na ukosefu wa fedha.
“Sekondari ya Wasichana Marian ilijengwa Februari 1997 ili kuwapa fursa wasichana wa Mkoa wa Pwani na maeneo jirani kupata elimu bora. Mpaka sasa tumetanua huduma na sasa tunajenga Sekondari ya Wavulana hapa Mlingotini. Pia, tunajenga zahanati kuwahudumia wananchi. Ili kukamilisha miundombinu muhimu kwa huduma hizi, tuna upungufu wa fedha ambazo tunawaomba wadau mtusaidie kwa michango ya hali na mali,” alisema Father Bayo.

Baada ya harambee hiyo iliyokamilika kwa mafanikio, Mwalimu Super Vedasto, mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Marian Mlingotini aliishukuru Benki ya CRDB na wazazi waliojitokeza.

“Tunamshukuru Nsekela na marafiki zake kwa kujitoa kwao kufanikisha harambee hii. Wazazi na wananchi waliokuja leo wametupa faraja na tunaamini tutafanikiwa kukamilisha ujenzi huu hivyokutoa elimu bora kwa vijana wetu,” amesema Mwalimu Vedasto.
Naye Askofu Mkuu mstaafu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Kadinali Polycarp Pengo aliyeshiriki harambee hiyo aliipongeza Benki ya CRDB kwa kujitoa kushirikiana na kanisa kuboresha huduma za jamii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kulia) akizungumza jambo na Askofu Mkuu mstaafu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Kadinali Polycarp Pengo, wakati wa harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Marian inayojengwa pamoja na zahanati, katika eneo la Mlingotini, wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani leo.
Sehemu ya wanafunzi waanzilishi wa Shule za Marian, wakiwa katika hafla hiyo.
Sehemu ya wanafunzi wa sasa wa Shule za Marian.
Burudani kutoka kwa Wanafunzi.


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akimkaidhi hundi kwa Mwanzilishi wa Shule za Marian, Father Valentino Bayo.




 


OSHA YAIMWAGIA SIFA BENKI YA CRDB KWA KUZINGATIA USALAMA MAHALI PA KAZI

April 29, 2023

 

 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako akimkaidhi tuzo Mkuu wa kitengo cha Ulinzi, Usalama na Mwendelezo wa Biashara wa Benki ya CRDB, Misana Mutani wakati Benki ya CRDB ikitunukiwa tuzo tatu ambazo ni mshindi wa kwanza katika kundi la benki na taasisi za fedha katika utekelezaji wa sera za Osha, Tuzo nyingine ni ya ufanisi katika utoaji huduma bora unaozingatia afya na usalama wa kazi kwa benki na ile ya kamati bora ya Osha katika huduma za kibenki, wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani ambayo kitaifa yalifanyika mkoani Morogoro.
Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi nchini (OSHA) umeipongeza Benki ya CRDB kwa kuwa mfano kwa taasisi za fedha katika kuzingatia na kujali usalama na afya kwa wafanyakazi wake.

Pongezi hizo zimetolewa na Mtendaji Mkuu wa OSHA Bi Khadija Mwenda kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani ambayo kitaifa yalifanyika mkoani Morogoro. Kwenye kilele cha maadhimisho hayo Benki ya CRDB ilipewa tuzo kwa kuzingatia viwango vinavyokubalika kwa usalama na afya za wafanyakazi wake.

“Naipongeza taasisi hii kubwa ya fedha nchini kwa kuwa mfano katika kuzingatia suala zima la usalama mahali pa kazi. Napenda kuchukua nafasi hii kuzitaka taasisi nyingine nazo kuiga mfano huu ili kuimarisha usalama na afya mahali pa kazi kwa wafanyakazi wao,” alisema Bi Khadija.
 Aidha, alisema lengo la maadhimisho hayo ni kuuhamasisha umma kuhusu usalama na afya mambo wanayoyasimamia chini ya sheria namba tano ya mwaka 2003 na kuhakikisha hilo linazingatiwa OSHA imekuwa ikifanya maadhimisho yanayohusisha kuwakumbuka wafanyakzi waliopoteza maisha au kuathirika wakiwa kazini na kuonyesha namna ya kuboresha usalama sehemu za kazi na jinsi zinavyoweza kusimamiwa katika kuhakikisha usalama kwa wafanyakazi wote.


Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako aliyekuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo alisema serikali inatambua na kuthamini usalama na afya mahali pa kazi.

“Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua usalama na afya mahali pa kazi ni haki ya msingi ya kila mfanyakazi nchini na ndiyo sababu Rais amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha nguvukazi ya taifa inalindwa,” alisema Profesa Ndalichako.

Waziri Ndalichako alisema kutokana na hilo serikali kupitia OSHA inaendelea kusimamia kwa karibu sheria namba tano ya afya na usalama mahali pa kazi ya mwaka 2003 kuhakikisha maeneo yote ya kazi yanakuwa na mifumo madhubuti ya kuwalinda wafanyakazi kutopata ajali au kuambukizwa magonjwa.

Aidha aliwapongeza wadau walioshiriki maadhimisho hayo ikiwemo Benki ya CRDB na kuwataka kuongeza usimamizi wa usalama na afya mahali pa kazi kwenye taasisi zao.

Mkuu wa kitengo cha Ulinzi, Usalama na Mwendelezo wa Biashara wa Benki ya CRDB, Misana Mutani alisema ufanisi mzuri wa benki hiyo ndiyo uliozaa matunda ya wao kupewa tuzo tatu katika kuzingatia afya na usalama mahali pa kazi kwa wafanyakazi.
Mutani alisema CRDB sio tu inazingatia usalama wa wafanyakazi wake pekee bali jamii inayowazunguka kwa maana ya wateja na wageni wanaotembelea maeneo ya benki hiyo kwani inahakikisha wapo salama wakati wote. Mbali na kuzingatia afya na usalama mahali pa kazi, alisema benki pia huendesha mbio za hisani maarufu kama CRDB Marathon ambazo hufanyika kila mwaka kwa mafanikio makubwa ili kukusanya fedha ambazo husaidia matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo au wanawake wenye fistula.

Mutani alisema fedha zilizokusanywa zimewezesha upasuaji wa watoto waliotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), kuwatibu wanawake waliokuwa na fistula waliotibiwa katika Hospitali ya CCBRT na kujenga kituo cha huduma kwa njia za simu “Call Center” katika Hospitali ya Ocean Road Ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa sahihi kwa mgojwa kupata huduma bila kulazimika kusafiri kuja kupata taarifa.
“Kwa ujenzi wa kituo kile sasa wagonjwa wanaweza kuweka miadi au kupata taarifa za awali bila kulazimika kusafiri umbali mrefu hivyo kuwapunguzia gharama ambazo hapo awali walikuwa wanashindwa kuzimudu," alisema Mutani.

Naye Meneja na Usaidizi wa Huduma wa CRDB, Elia Mnonjela alisema wakati anaongea na wadau waliotembelea banda  lao katika maonyesho hayo wamefahamishwa kuhusu huduma nafuu zinazowapa fursa ya kujikwamua kiuchumi.

"Tunayahudumia makundi yote yaani wafanyakazi na wafanyabiashara. Kwa unafuu uliopo, wafanyakazi wana wigo mpana zaidi wa kukopa katika benki yetu na kukuza uchumi wao kwa riba nafuu tofauti na awali," alisema Mnonjela.

Kwenye maadhimisho hayo  Benki ya CRDB ilitunukiwa tuzo tatu. Ya kwanza ni mshindi wa kwanza katika kundi la benki na taasisi za fedha katika utekelezaji wa sera za Osha. Tuzo nyingine ni ya ufanisi katika utoaji huduma bora unaozingatia afya na usalama wa kazi kwa benki na ile ya kamati bora ya Osha katika huduma za kibenki.


PSSSF YAPITA "BANDA KWA BANDA" KUWAFIKIA WANACHAMA WAKE KWENYE MAOENSHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA USALAMA NA AFYA MAHALI PA KAZI

April 27, 2023

 

 

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MOROGORO.

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) pamoja na kutoa elimu kwa wanachama na wananchi wanaotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, viwanja vya Tumbaku mjini Morogoro, pia unapita “Banda kwa Banda” ili kuwafikia wanachama wake, Afisa Uhusiano Mkuu wa Mfuko huo Bw. Abdul Njaidi amesema.

Bw. Njaidi amesema Mfuko unashiriki Maonesho hayo kwa lengo la kutoa elimu na kuwahudumia wanachama wake ambao ni wastaafu lakini pia watumishi wa Umma na Mashirika ambayo Serikali inamiliki hisa asilimia 30.

“Lakini tukumbuke kuwa watumishi walio kwenye viwanja hivi nao pia wanawahudumia wananchi kwenye mabanda yao, hivyo tumeona tugawane majukumu, baadhi yetu wako bandani kutoa elimu na huduma kwa watakaofika na sisi tunapita banda kwa banda kuwahudumia." Alifafanua Bw. Njaidi ambaye alifuatana na Afisa Matekelezo Mwadamizi wa Mfuko huo Bw. Charles Mahanga.

Akifafanua alisema kwakuwa huduma nyingi za Mfuko zinapatikana kiganjani (PSSSF Kiganjani) hivyo ni rahisi kuwapatia elimu kwenye mabanda yao ya jinsi ya kutumia huduma hiyo.

Kilele cha Maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya mahali pa kazi hufanyika Aprili 28 kila mwaka ambapo Tanzania huungana na mataifa mengine duniani kuiadhimisha siku hii, lengo kubwa ni kuendeleza kampeni za kuhamasisha uwepo wa mazingira salama na yenye kulinda afya za watu katika sehemu za kazi ambapo kauli mbiu ya maadhimisho kwa mwakam huu ni “Mazingira salama na afya ni kanuni na haki ya msingi mahali pa kazi.”.

Afisa Uhusiano Mkuu wa PSSSF Bw. Abdul Njaidi akiwa na Afisa Matekelezo Mwandamizi PSSSF, Charles Mahanga akimkabidhi kipeperushi cha PSSSF Msimamizi Mkuu wa banda la Jeshi la Polisi, Mkaguzi Msaidizi Zuwena Mwita.
Meneja wa PSSSF Kanda ya Masahariki, Bi. Zaida Mahava (kulia) akimuhudumia mwanachama

Bw. Njaidi (kushoto), akitoa elimu kwa maafisa wa polisi.

Banda la NMB
Banda la NSSF
Banda la CRDB
Banda la CRDB
Banda la WCF

Banda la OSHA

RAIS SAMIA SULUHU PAMOJA NA RAIS WA RWANDA PAUL KAGAME WAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI,IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

April 27, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame mara baada ya mazungumzo yao Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023. Rais wa Rwanda Mhe. Kagame amewasili nchini kwa ajili ya ziara ya Kikazi ya Siku 2.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza ujumbe wa Tanzania katika Mazungumzo Rasmi na Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame wakati wakizungumza na Waandishi wa Habari, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na mgeni wake Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame mara baada ya kuzungumza na Waandishi wa Habari Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023

 

JIJI LA TANGA LAMPONGEZA RAIS DKT SAMIA SULUHU KWA KUONYESHA UONGOZI ULIOTUKUKA

April 27, 2023



Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shillow akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani la Robo tatu kilichoketi leo kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema na kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Dkt Sipora Liana


Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Hamisi Mkoba akizungumza wakati wa kikao hicho


Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Dkt Sipora Liana akizungumza wakati wa kikao hicho
Sehemu ya madiwani wakiwa kwenye kikao hicho
Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga wakiwa kwenye baraza hilo
Sehemu wa madiwani wakifuatilia hoja mbalimbali



Na Oscar Assenga, Tanga. 

HALMASHAURI ya Jiji la Tanga limepongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa kutimiza miaka miwili madarakani kwa kuonyesha uongozi uliotukuka katika mambo mbalimbali ikiwemo kuendeleza miradi mikubwa iliyoacha na mtangulizi wake hayati Dkt John Magufuli. 

Pongezi hizo zimetolewa leo na Mshtahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shilloo wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani cha Robo ya tatu ambapo alisema licha ya kuendeleza miradi lakini pia ameanzisha mingine mikubwa ikiendana na kupelekea fedha nyingi kwenye ngazi ya Halmashauri ikiwemo Tanga Jiji ambao pia wamenufaina nazo. 

Shillow alisema pamoja na hayo lakini Rais Dkt Samia Suluhu amefungua upya milango ya ajira kwa watumishi wa umma baada ya kuingia madarakani kuongeza mishahara kwa watumishi wa umma na kuwapatia unaafuu katika kodi mbalimbali ili waweze kukidhi mahitaji yao na kudumu masiaha yao.

“Lakini jambo jingine ni Rais Dkt Samia Suluhu kuongeza mikopo ya elimu ya juu, kuondosha riba kwa wanafunzi kwenye mikopo hiyo sambamba na kufungua milango ya demokrasia kwa kuenzi utanzania umoja, mshikamano na undugu kwa watanzania bila kujali tofauti za kiitikadi “Alisema Mshtahiki Meya huyo.

Hata hivyo alisema kwamba wanampongeza pia kwakutoa matokeo ya sensa ya watu na makazi iliyofanywa kidigitali kwa mara ya kwanza tokeo nchi ipate uhuru ikiwemo kugawa vishikwambi vilivyotumika katika sensa kwenye idara ya elimu sekondari na msingi za Halmashauri nchini ili kuimarisha elimu na uwekaji wa takwimu za elimu pamoja na kuifungua nchi kwenye mambo ya utalii na mahusiano ya kikanda na kimataifa.

Mwisho.