WAZIRI UMMY MGENI RASMI MATEMBEZI YA KILOMITA 5 JIJINI TANGA

February 28, 2023




Na Mwandishi Wetu,Tanga


Waziri wa Afya Ummy Mwalimu anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika  mazoezi ya viungo na matembezi ya umbali wa kilomita tano (5km) yenye kauli mbiu " Tembea na JKCI - Linda Afya ya Moyo Wako" yatafanyika Machi 11 mwaka huu yatakayoanzia kwenye viwanja vya NIMR Bombo Hospitali.


Matembezi hayo yameandaliwa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo ya JKCI 


Akizungumza kuhusu matembezi hayo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Naima Zakaria alisema maandalizi yamekamilika.


Dkt Naima alisema  matembezi hayo yataanza saa 12:30 asubuhi hadi saa 2:30 asubuhi yatakayokwenda sambamba na ufungaji wa kambi upimaji.


Alisema matembezi hayo yataanzia kwenye viwanja vya NIMR Bombo Hospitali kupitia Mkonge Hotel, Raskazone Polisi hadi Nyinda Classic kuelekea Ukuta wa Mbolea (GBP), Masai Utalii College, Lulu Image,Tanga International School, Splended, Tanesco, Toyota Mataa na kumalizikia Bombo Hospitali Viwanja vya Mapokezi.


Hata hivyo Dkt Naima alivitaka vilabu vya mazoezi viweze kushiriki nao pamoja katika ufanyaji wa mazoezi ili kulinda Afya ya Moyo sambamba na kupunguza athari zinazotokana na  magonjwa yasiyo ambukiza kwa jamii.


Mwisho


SHULE YA SEKONDARI COASTAL YA JIJINI TANGA KUANZA KUNUFAIKA NA MKONGE

February 28, 2023

 

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) ,Saad Kambona akizungumza wakati wa maafali ya kidato cha sita shule ya Sekondari Coastal High School ya Jijini Tanga yaliyofanyika kwenye Hotel ya CBA Jijini Tanga

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) ,Saad Kambona akimkabidhi cheti mmoja wa wahitimu wa kidato cha sita katika shule ya Sekondari Coastal High School ya Jijini Tanga kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Coastal High School Andrew Gasper akifuatiwa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo,Lulu George



Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) ,Saad Kambona akimkabidhi cheti mmoja wa wahitimu wa kidato cha sita katika shule ya Sekondari Coastal High School ya Jijini Tanga kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Coastal High School Andrew Gasper akifuatiwa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo,Lulu George




Na Oscar Assenga,Tanga.

Shule ya Sekondari Coastal ya jijini Tanga,itaanza kunufaika na uwekezaji wa sekta ya mkonge baada ya Bodi ya Mkonge Tanzani (TSB) kuahidi kuiingiza katika majaribio ya klabu za vijana watakaoendelezwa.

Pia shule hiyo imeahidiwa kupewa ekari 100 kwa ajili ya kilimo cha mkonge ikiwa ni sehemu ya kuiongezea kipato .

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mko n ge nchini,Saad Kambona alitoa ahadi hiyo wakati wa mahafali ya kuwaaga wahitimu wa kidato cha sita walioanza mtihani ya kitaifa.

Alisema bodi hiyo imeandaa programu maalumu itakayowawezesha vijana kujiinua kiuchumi kuptia kilimo cha mkonge na bidhaa zitoakanazo na zao hilo.

Alisema kama inavyofahamika Bodi ya Mkonge ni taasisi ambayo kwa muda mrefu ilikuwa ni kama imekufa sasa imeshafungua rasmi ofisi katika jengo lake na kuwezesha kuinua sekta ya mkonge kwa ujumla wake.

“Lakini tunategemea tunapokwenda mbele vijana wengi sana kutoka kwenye shule za Tanga ndiyo wahusike kwenye mpango mzima wa kuleta mapinduzi kwenye zao la mkonge kwani sasa hivi tunapozungumzia mkonge tunazungumzia bidhaa moja tu ya nyuzi za mkonge zitengeneze vikapu, makapeti, magunia, kamba na bidhaa nyingine zitokanazo na zao hilo ,lakini kuna bidhaa nyingti zinahitajika kama sukari,mbolea mvinyo na hata vyakula vya kunenepesha mifugo” alisema Kambona

Mkuu wa shule hiyo,Joseph Gaspar alisema ilianza rasmi mwaka 2000 na kwamba kwa miaka mitatu mfululizo imekuwa ikitoa ufaulu wa daraja la kwanza A na pili kwa wanafunzi wote wa kidato cha sita wote katik a mitihani ya kitaifa ya mchepuo wa sayansi.

“Hadi sasa shule hii imetimiza miaka 22 lakini kwa kipindi cha miaka miatatu mfululizo i mekuwa ikitoa wanafunzi wenye ufaulu wa daraja la kwanza na la pili katika mitihani ya kitaifa ya kidato cha sita...tunatarajia mitihani hii ufaulu utakuwa wajuu zaidi”alisema Gasper.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo,Lulu George alisema kuwa miongoni mwa mambo yanayotiliwa mkazo ni masomo ya sayansi wakiamini kuwa jukumu lao ni kupata wataalamu watakaoiendeleza nchi katika sekta ya uhandisi,udaktari na utafiti mbalimbali ikiwamo sekta ya kilimo na ufugaji.

MATUNDA YA UWEKEZAJI BANDARI YA TANGA YAIWEZESHA MELI KUBWA YA MZIGO KUTOKA NCHINI URUSI KUTIA NANGA GATINI

February 27, 2023

 Meli kubwa ya Mzigo kutoka nchini Urusi yenye urefu wa mita 150 ikiwa imetia nanga katika Bandari ya Tanga mapema leo

 Meli kubwa ya Mzigo kutoka nchini Urusi yenye urefu wa mita 150 ikiwa imetia nanga katika Bandari ya Tanga mapema leo

Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha akizungumza na waandishi wa habari leo
Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Bandari ya Tanga Rose Tandiko akizungumza 




Na Oscar Assenga,TANGA.

Matunda ya uwekezaji wa Bandari ya Tanga yameanza kuonekana mara baada ya Meli kubwa ya Mzigo kutoka nchini Urusi yenye urefu wa mita 150 kutia nanga katika Bandari hiyo

Hatua hiyo ni baada ya kukamilika kwa gati lenye urefu wa mita 300 ambao umeiwezesha meli hiyo kuweza kutia nanga gatini na kuandika historia kwa mara ya kwanza kupokea meli kubwa mpaka gatini na hivyo kuandika historia ya kipekee baada ya maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali.

Akizungumza leo wakati wa mapokezi ya meli hiyo ambayo ilikuwa imebaba shehena ya Mbolea kwa ajili ya viwanda ,Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha alisema ujio wa meli hiyo ni matunda makubwa ya uwekezaji ambao umefanywa na Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu kwenye Bandari hiyo.

Alisema kwamba meli hiyo ilikuwa imebeba mzigo wa tani 6909 unaokwenda nchini Kongo ambapo utapakuliwa kwa muda wa siku mbili kuanzia leo Jumatatu.

Aidha Meneja huyo aliwataka wafanyabiashara kwamba Bandari ya Tanga imeanza kufunguka kutokana na maboresho makubwa hali ambayo imepelekea huduma kuimarika zaidi.

Awali akizungumza Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Bandari ya Tanga Rose Tandiko alisema kwamba matunda ya ujio wa meli hiyo ni kutokana na uwekezaji mkubwa ambao umefanywa na Rais Samia Suluhu.

Alisema uwekezaji huo umewezesha kuandika histoiria katika Bandari hiyo kwa kuanza kuhudumia meli ya kichele gatini jambo ambalo awali lilikuwa halifanyiki.

Hata hivyo alisema kwamba wanamshukuru Rais Samia Suluhu kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika katika Bandari hiyo na matokeo yake yameanza kuonekana .

TCDC kuja na mkakati wa kukuza biashara kidijitali

February 27, 2023
Kamisheni ya Maendeleo ya Ushirika hapa nchini (TCDC) imeanza kutekeleza mpango ya kubadili namna ya kuendesha vyama vya ushirika na kuviwezesha kutumia teknolojia za kisasa katika kufanya shughuli zao

Mwenyekiti wa Kamisheni ya Maendeleo ya Ushirika hapa nchini Abdulmajid Nsekela ametoa taarifa hiyo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa ushirika kujadili maendeleo ya ushirika na kuweka mkakati wa kuimarisha sekta ya hiyo hapa nchini

Nsekela amesema uwekezaji katika mifumo ya kisasa ya kidijitali itaongeza ufanisi wa kiutendaji katika Vyama vya Ushirika, pamoja na Mamlaka za Usimamizi wa sekta hiyo.
Ameongeza kuwa pamoja na mambo mengine lakini mapendekezo yatakayotolewa katika mkutano huo yatasaidia kuuboresha mfumo wa ushirika kuwa wa kisasa zaidi na ili kuwawezesha wananchi kushiriki ipasavyo kwa ustawi wao na wa Taifa kwa ujumla.

“Ni matumaini yangu kuwa Maazimio yatakayofikiwa kupitia Mkutano huu yatapaswa kutekelezwa ipasavyo na kila mdau na kwamba taarifa ya utekelezaji itakuwa inatolewa na kujadiliwa mara kwa mara”-amesema Nsekela.
 
Kwa upande wake Mrajisi wa Ushirika nchini Dkt. Benson Ndiege amesema lengo kubwa la mkutano huo wa wadau wa ushirika ni kujadili maendeleo ya ushirika na kuweka mkakati wa kuimarisha sekta hiyo hapa nchini.  

“Mkutano huu ni muhimu kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya Ushirika hapa nchini, lakini pia tumekutana wadau wote ili kuja na mapendekezo ya pamoja ya kuendeleza sekta hii kwa maendeleo ya Taifa”- amesema Ndiege.
 Mwenyekiti wa Kamisheni ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Abdulmajid Nsekela akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa ushirika uliolenga kujadili maendeleo ya ushirika na kuweka mkakati wa kuimarisha sekta hiyo nchini, uliofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Benki ya CRDB, jijini Dar es salaam, Februari 27, 2023. 
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya  Ushirika Tanzania (TFC), Charles Jishuri akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa ushirika uliolenga kujadili maendeleo ya ushirika na kuweka mkakati wa kuimarisha sekta hiyo nchini, uliofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Benki ya CRDB, jijini Dar es salaam, Februari 27, 2023.


Sehemu ya wadau wa Kamisheni ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), wakifatilia mkutano uliolenga kujadili maendeleo ya ushirika na kuweka mkakati wa kuimarisha sekta hiyo nchini, uliofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Benki ya CRDB, jijini Dar es salaam, Februari 27, 2023.







MIKABATA NANE YA MIRADI YA MAJI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 10 YASAINIWA NA RUWASA TANGA

February 25, 2023





Na Oscar Assenga,TANGA

JUMLA ya Mikataba 8 ya miradi ya maji yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 10 itakayotekelezwa katika wilaya tano za mkoa Tanga imesainiwa mwishoni mwa wiki na Wakala wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa huo pamoja na mkataba mmoja wa mhandisi mshauri .

Miradi hiyo ya maji itakwenda kuwa mkombozi na kwa wananchi kwenye vijiji 20 wapatao 39, 226 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2023 sawa na asilimia 1.5 ya wakazi wote wa mkoa huo.

Akizungumza wakati wa halfa hiyo Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upenndo Lugongo alisema miradi hiyo ambayo ni mipya yenye jumla ya vituo 92 vya kuchotea maji na matangi 9 yenye ujazo wa jumla ya mita za ujazo 1,830.

Mhandisi Upendo alisema pamoja na mtandao wa mabomba kilometa 162.2 inatarajiwa kuongeza hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa asilimia 1.5 kwa wananchi wanaoishi vijijini.

Alisema kwamba lengo la kusainiwa kwa mikataba hiyo ni kuingia makubaliano ya pamoja na wakandarasi pamoja na mhandisi mshauri ambayo yataleta ufanisi na tija ya utekelezaji wa miradi hiyo kwa kufuata kanuni , taratibu na sheria mbalimbali zitakazofuatwa kwa nia ya kukamilisha utekelezaji huo.

Alisema licha ya miradi hiyo mipya kusainiwa ipo mingine minne inatekelezwa ikiwa ni mkakati wao wa kuhakikisha wanaondosha changamoto ya ukosefu wa maji vijijini katika wilaya mbalimbali za mkoa wa Tanga ambapo jumla ya wananchi 2, 310000 wanatarajiwa kunufaika mara baada itakapokamilika.

Hata hivyo alisema katika miradi hiyo inayoendelea itakapokamilika itaweza kusaidia kuwahudumia wananchi wapatao 2, 31000 sawasawa na asilimia 9 ya wakazi wa mkoa wa Tanga ukilinganisha na ile ya mwaka 2022, tunaenda kusaini mikataba 9 ambayo ni ndani ya ujenzi lakini pia kuna mkataba mmoja wa mhandisi mshauri na katika mikataba hii nane tunaweka kwanza mabomba yenye jumla kilometa 1, 68, 000 ambayo ina thamani yabshilingi bilion 10 na inaenda kujenga vituo 110 ambavyo tutakuwa tunahudumia wakazi 31, 0000 "

"Lengo kuu la serikali ni kuhakikisha tunamtua mama ndoo kichwani na kuona kwamba huduma ya maji tunaenda kuitoa na kupunguza muda wa utafutaji maji kwa wananchi ili waweze kushiriki kwenye kazi nyingine za kiuchumi , serikali inaelekeza kuwa ifikapo 2025 tuwe tumefikia asilimia 85 ya upatikanaji wa maji vijijini" alisema Lugongo

Alisema kwamba wakala huo umeingia makubaliano na makambuni mbalimbali ambayo ni kampuni ya Nipo Africa engineering Co.ltd atakayetekeleza miradi katika wilaya ya Kilindi , Lukedan Company Limited wilaya ya Handeni, Wraptec engineering ltd Handeni, Planet water Geographycs ltd (Mkinga), Wraptec engineering ltd (Korogwe), Buzubona and Sons Company na Hinry Company (Lushoto) pamoja na kampuni ya Env Consultant

Akizungumza wakati wa halfa hiyo Mkuu wa mkoa wa Tanga Omari Mgumba amewataka wakandarasi wote watakaotekeleza miradi hiyo ambao wengi wao ni wazawa kuwa wazalendo na kukamilisha kazi kwa wakati ili iweze kuleta tija kwa wananchi ikiwemo kuwataka kuwatumia wananchi wa maeneo husika wakati wa utekelezaji wa mradi huo

"Fedha hizi ni nyingi sana ambazo ni kodi za watanzania hivyo zinatakiwa zionyeshe matokeo makubwa yenye tija kwa miundombinu ya maji inayotumiwa na wananachi ili kukidhi malengo ya serikali, nimeelezwa kuwa sehemu kubwa ya wakandarasi wanaotekeleza miradi hii ni wazawa hivyo nawataka kuwa wazalendo kwa kufanya kazi weledi na ufanisi mkubwa katika utekelezaji wa mikataba hii nasisitiza wakandarasi kuwatumia wananchi wa maeneo inayotekelezwa miradi hii katika kazi za vibarua ambazo hazihitaji utaalam mkubwa" alisema Mgumba.

Rc Mgumba amewataka wananchi wa mkoa wa Tanga kuendelea kuyatunza mazingira sambamba na kujiepusha na kufanya shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji ambapo kwa kiasi kikubwa zimekuwa zikichangia kukosekana kwa huduma hiyo na hatimaye kusababisha athari mbalimbali ikiwemo changamoto ya maji ya kutosha pamoja na ukame katika vyanzo vikubwa vinavyotegemewa na mamlaka husika.

"Kuna changamoto ya upatikanaji wa maji safi na yamekuwa haba ni kwa sababu ya ukame ambao umesababishwa na uharibifu wa mazingira na ukame ikiwemo shughuli za kibinadamu na kuvamia vyanzo vya maji nitoe wito kwa wananchi tutunze mazingira ili nayo yatutunze ili kuondokana na uhaba huu wa maji ili mito yetu iwe na maji muda wote"

"Tuna tatizo kubwa la uhaba wa maji katika mkoa wetu wa Tanga na moja wapo ya sababu ni kutokana na umeme mdogo tuliokuwa nao unakatika mara kwa mara na hautabiriki kwahiyo tuna uhaba zaid ya Mega wat 20 zinazohitajika mahitaji yetu yalikuwa zaid ya megawa 136 lakini sasa zimeshuka hadi 80" alibainisha Mgumba


BMH, BOMBO KUENDESHA KAMBI YA HUDUMA MBALIMBALI ZA KIBINGWA JIJINI TANGA

February 24, 2023


Na Oscar Assenga, Tanga

HOSPITALI ya Benjamini Mkapa (BMH) ikishirikiana na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo wanatarajia kufanya kambi ya huduma mbalimbali za kibingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kuanzia February 27 hadi Machi 3 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo Dkt Naima Yusuf alisema kwamba maandalizi ya kuelekea kambi hizo yanaendelea vizuri huku akieleza huduma za kibingwa zitakazotolewa.

Dkt Naima alisema huduma zitakazotolewa ni Upasuaji Mishipa ya Fahamu ,Mifupa, Mfumo wa Haja ndogo (Mkojo),Magonjwa ya ndani,Tiba ya Figo,Tiba ya Moyo kwa watoto na watu wazima.

Alizitaja huduma nyengine zitakazotolewa ni Magonjwa ya watoto Magonjwa ya macho,Tiba ya Kinywa na Meno pamoja na Magonjwa ya Uzazi kwa akina Mama.

Hata hivyo Dkt Naima alisema kwamba katika kambi hiyo wateja wa bima ambao watapokelwa ni wa Jubilee Insurance,Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Assemble Insurance na Strategis Insurance.


WACHIMBAJI WA MADINI MZINGATIE SHERIA,USALAMA,MAZINGIRA NA MATUMIZI SALAMA YA BARUTI-PROFESA KIKULA

February 23, 2023






Mwenyekiti wa Tume wa Madini Profesa Idris Kikula amewataka Wachimbaji na Wafanyabiashara wa madini nchini kuzingatia Sheria, Usalama, Utunzaji wa Mazingira na Matumizi Salama ya Baruti katika uendeshaji wa shughuli za uchimbaji madini migodini, ambapo kila mchimbaji  ana wajibu wa kusimamia mazingira kwa mujibu wa Sheria zilizowekwa.

Profesa Kikula ameyasema hayo leo Februari 23, 2023 kwenye ufunguzi wa mafunzo ya Usalama, Afya, Utunzaji wa Mazingira na Matumizi Salama ya Baruti kwa Wachimbaji wadogo wa madini, yaliyofanyika Mkoani  Mara ambayo yamekutanisha Wakurugenzi, Mameneja, na Watumishi kutoka Tume ya Madini, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara, Viongozi wa Wachimbaji wadogo na Wachenjuaji wa Madini, pamoja na Wafanyabiashara na Wamiliki wa Migodi wa Mkoa wa Mara.

Profesa Kikula amesema kuwa mafunzo hayo ya siku mbili, yanalenga kuhakikisha kuwa shughuli za uchimbaji, uchenjuaji na biashara ya madini zinafanyika kwa kuzingatia Usalama, Afya na Utunzaji wa Mazingira kwa kufuata Sheria, Kanuni na miongozo mbalimbali iliyowekwa.


Amesema kuwa mafunzo hayo yatazingatia pia utaratibu wa utoaji leseni za uchimbaji, uchenjuaji, biashara ya madini hususan kwenye usimamizi wa masoko ya madini na vituo vya ununuzi wa madini nchini.


“Kupitia mafunzo haya naamini mna wajibu mkubwa wa kuimarisha mfumo wenu wa utendaji kazi kwa kuangalia usalama katika maeneo mnayochimba ili kuhakiksha kuwa taifa halipotezi nguvu kazi ili tuwe na uchimbaji endelevu wa kuimarisha maisha yetu na jamii inayotuzunguka,” amesema Profesa Kikula.

ORYX GAS YAGAWA BURE MAJIKO NA MITUNGI KWA WANAWAKE WAJASIRIAMALI MKOANI TANGA, MBUNGE UMMY AWASHUKURU KWA KUWAWEZESHA WAKINA MAMA HAO

February 21, 2023
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Duka la Kuuzia Gesi Kampuni ya Oryxs lililopo barabara ya 7 Jijini Tanga kulia Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Duka la Kuuzia Gesi Kampuni ya Oryxs lililopo barabara ya 7 Jijini Tanga kulia Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kulia akiwa amebeba mtungi wa Gesi ya Oryx 
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kushoto akifurahia jambo wa pili kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akipokea Mitungi ya Gesi ya kampuni ya Oryx


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo



Na Oscar Assenga, Tanga


KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imekabidhi mitungi ya gesi pamoja na majiko yake 600 kwa wanawake 600 kutoka vikundi mbalimbali vikiwemo vya wajasiriamali katika Mkoa wa Tanga ikiwa ni mkakati wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa yanayoharibu mazingira.

Huku Mbunge wa Jimbo la Tanga ambaye pia ni Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akiishukuru Kampuni ya Oryxs Gas Tanzania kwa kuridhia ombi lake la kukubali kuwasaidia wanawake wajasiriamali kutoka vikundi mbalimbali vilivyopo kwenye Kata zote za Jimbo lake 

Akizungumza wakati wa kukabidhi mitungi hiyo ya gesi mbele ya Waziri wa Afya ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu, Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite amesema kutokana na madhara ya gesi ya ukaa duniani, kampuni ya Oryx Tanzania (OGTL) iko mstari wa mbele kusaidia kuhamasisha matumizi ya gesi safi ya kupikia kwa kutoa mchango mwingine wa vifaa vya gesi mkoani Tanga ambako matumizi ya mkaa ni makubwa.

Amesema matumizi ya mkaa yana athari kubwa kwa mazingira na husababisha jangwa huku akifafanua Tanga ni miongoni mwa mikoa hapa nchini ambayo ina hali ya juu ya ukataji miti kwa ajili ya mkaa, hivyo wao wanaamini mpango huo wa kusaidia vifaa utasaidia wakazi wa Tanga, hasa wanawake ambao wanaathirika na moshi utakanao na kuni na mkaa.

"Kampuni inawekeza kwa kutekeleza miradi ya kutoa elimu juu ya gesi safi ya kupikia, inachangia vifaa vya gesi ya kupikia katika baadhi ya mikoa.Pia tunahamasisha matumizi ya gesi kwa kufanya mauzo makubwa ya mitungi kwa bei nafuu.

"Juhudi zote hizi zinalenga kufanya Watanzania wengi wanaanza kutumia gesi safi ya kupikia kama alivyoahidi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan.

Rais Samia ambaye ameweka malengo kuwa ifikapo mwaka 2030 asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia gesi safi ya kupikia.

"Kampuni ya Oryx Gas Tanzania pia imeitikia wito wa kidunia ya kupunguza hewa ukaa kutoka viwandani na shughuli za kibinadamu Kupitia promosheni ya LPGOGTL kampuni is furaha kuungana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika juhudi za kuboresha Maisha ya Watanzania kwa kupunguza hewa ukaa. Tunasikia faraja kusaidia utekelezaji wa ajenda ya LPG ambayo inainufaisha Tanzania,amesema Benoit.

Awali akizungumza Waziri wa Afya na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu alimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Oryx Tanzania kuwa kuwasaidia kuwezesha majiko ya gesi kwa wanawake wajasiriamali kwenye Jiji hilo.

Alisema kwamba msaada huo umekuja wakati na hivyo kuwa mkombozi mkubwa kwa wana Tanga kutokana na kwamba lazima lifanane na watu na hali halisi hivyo mahitaji ya gesi ni muhimu na hayaweze kukwepeka kwa wananchi.

“Ndugu zangu wana Tanga Oryxs Gas ni Kampuni Bora na nzuri na labda niwaambie kwamba hawapunyi kwenye vipimo vyao lakini niwashukuru kwa kufungua duka hilo na wao kama Tanga Jiji wamepata mlipa kodi mpya “Alisema

Hata hivyo Waziri Ummy alimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Oryxs Gas Tanzania baada ya kumwambia kwamba Tanga kuna wasiriamali na wangependa kuwasadia majiko ya gesi kwa ajili ya kurahisisha shughuli zao kujipatia kipato na kuandaa chakula .

“Hivyo tunamshukuru Mungu kwa kutuwezesha jambo hilo,alisema kwamba yeye anataka kuwasaidia na kuwainua wananchi wa kipato cha chini na kuwaambia kwamba atamsaidia kufanikisha hilo lakini pia matumizi ya gesi yataweza kusaidia kuondokana na matumizi ya mkaa ambayo ni gharama kubwa “Alisema

Naye kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa alisema kitendo kilichofanywa na Mbunge huyo kitaacha alama na wanaona wanakwenda kutibua sehemu ya changamoto kwenye jamii ya ukataji wa miti ambayo mwisho wa siku inapelekea kuharibu mazingira.

“Matumizi ya gesi nchini bado yanakwenda kwa kusuasua kwa hiyo kupitia hili kutakuwa na ushawishi mkubwa kwa kuhakikisha jamii inatumia nishati mbadala ya gesi ambayo itasaidia kutunza mazingira na kuondoa uharibifu wa mazingira” Alisema

Hata hivyo kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Tanga Al- Shaymaa Kweygir alisema kwamba wanashukuru Mbunge Ummy Mwalimu kwa kuwajali wakina mama kwa sababu wao wana mchango mkubwa kwa maendeleo .

Kweygir alisema kwamba kitendo cha kuwezeshwa majiko ya Gesi kwa wajasiriamali wanawake itawasaidia kuwakomboa kichumi kwa sababu wanapokuwa kwenye shughuli zao watakuwa wakitumia muda mchache kuandaa na kuwahuduma wateja wao.

Naye kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shiloo alimshukuru Mbunge Ummy kwa kuendelea kuwajali wananchi na Baraza la Madiwani linamshukuru kwa kuhakikisha maendeleo kwenye Jimbo hilo yanaendelea kupaa.

Hata hivyo alisema kwamba Mbunge huyo ni wa kipekee kutokea tokea Jimbo hilo lilipoanzishwa ameacha alama na kuvunja rekodi ya wabunge wengine waliowahi kuliongoza Jimbo hilo .

Mwisho