UDHAMINI WA PUMA NDANI YA IFA UTASAIDIA KUINUA VIPAJI VYA SOKA MKOANI IRINGA

April 30, 2018

Mkurugenzi wa kituo cha kuendeleza soka cha Iringa (IFA) Ally Msigwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake akielezea mipango yake ya kuinua soka la vijana mkoani Iringa na Nje ya mkoa wa Iringa.

Mkurugenzi wa kituo cha kuendeleza soka cha Iringa (IFA) Ally Msigwa akionyesha jinsi ambavyo nembo ya puma iatapoa kwenye jezi za kituo hicho

Mkurugenzi wa kituo cha kuendeleza soka cha Iringa (IFA) Ally Msigwa akiwa na kocha mkuu wa kituo hicho mwalimu Saleh molelikatika ofisi za IFA mkoani Iringa

NA FREDY MGUNDA, IRINGA

KITUO cha kuendeleza soka cha Iringa (IFA) kimefanikiwa kuingia mkataba wa udhamini wa wa jezi na vifaa vya michezo kwa muda wa miaka miwili na kampuni ya mafuta ya Puma Energy.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mkurugenzi wa kituo cha kuendeleza soka cha Iringa (IFA) Ally Msigwa, alisema kuwa kituo hicho kimepata udhamini wa vifaa vya michezo kutoka kampuni hiyo na udhamini huo utakijita kwenye safari zote za timu inapoelekea katika michezo mbalimbali ndani na nje ya mkoa wa Iringa.

Msigwa alisema kuwa kituo hicho kimekuwa kimbilio la vijana wengi wenye vipaji na kimefanikiwa kupata ufadhili wa kudumu kutoka kwa kampuni ya Alishati Investment ambayo itafadhili mahitaji mbalimbali katika kituo hicho.

Alisema kuwa kituo hicho ambacho kimekuwa kikubwa kwa sasa kina mahitaji mengi ambayo yanahitajika katika kujikimu na kwa sasa kinatarajia kuwa na uwanja wake maeneo ya Ifunda kata ya Lumuli wilaya ya Iringa ambapo ujenzi wake uko katika mchakato kuanza baada ya kila kitu kukamilika.

Msigwa ambaye alikuwa mchezaji wa zamani wa Yanga alisema kuwa katika ujenzi wa uwanja wanatarajia kujenga uwanja wa kisasa utakaochukua watu zidi 5000 hivyo kuwa moja ya viwanja bora kabisa kwa upande wa Nyanda za Juu Kusini.

Msigwa Aliongeza kuwa uongozi wa kituo hicho umeeamua kuunda bodi ya wakurugenzi ambao watasaidiana katika kufanikisha ndoto mbalimbali za kukuza soka la vijana nchini Tanzania ambapo Dk. Mshindo Msola ameteuliwa kuwa mkurugenzi wa ufundi wa kituo hicho na kocha Salehe Molel kuwa kocha wa vijana chini ya miaka 15 hadi 17.

Aidha Msigwa alisema kuwa IFA imefanikiwa kuteua wajumbe wa bodi ambapo itaongozwa na Augustino Mahiga Waziri wa Mambo Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu ofisi ya Msajili Hazina Wizara ya Fedha Gerald Mwanilwa.

Wengine watakaounda wajumbe wa bodi ni Ezra Chomete mtanzania mwenye makazi Marekani, Abdul Mapembe ambaye ni Meneja TRA Ilala, Mhindisi Patrick Mbendule na Mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Iringa, Cyprian Kuyava.

Naye kocha mkuu wa kituo hicho mwalimu Saleh moleli alisema kuwa amepata sehemu sahihi ya kuujenga upya mpira wa mkoa wa Iringa kwa kuwa hapo awali alikuwa kocha anayefundisha timu za wakubwa tu.

“Kupata nafasi hii kwangu kama kocha mzoefu nimefarijika sana,nitakikisha naitumia vilivyo kwa kuahikisha mpira wa vijana unakuwa na kuzailisha kizazi cha soka hapa mkoani Iringa na duniani kwa ujumla” alisema Moleli

Moleli alisema kuwa watahakikisha vijana wote watakokuwa kwenye kituo hicho watapata elimu bila wasisi wowote ule.

“Wazazi wengi wamekuwa wakiwazuia watoto wao kukuza vipaji vyao kwa kuhofia kutoendelea na masomo yao lakini kwenye mpingo yetu kutakuwa na shule ambayo itawasaidia wanafunzi kusoma wakiwa hapo kituoni” alisema Moleli

DK. KIGWANGALLA ATOA OFA YA MAPUMZIKO YA FUNGATE YA ALI KIBA KATIKA HIFADHI ZA WANYAMAPORI

April 30, 2018

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ametoa ofa maalum kwa Mwanamuziki, Ally Kiba, mke wake na wasaidizi wake ambao ni mdogo wake Abdu Kiba na mkewe kupumzika katika Hifadhi ya Taifa atakayoichagua wakati wa fungate yake ili aweze kufurahi vivutio vya utalii vilivyopo na hivyo kuhamasisha utalii wa ndani. Ametoa ofa hiyo jana wakati wa harusi ya msanii huyo iliyofanyika katika ukumbi wa Serena Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa sherehe hiyo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde na Mbunge wa Viti Maalum, Neema Mgaya.

Picha ya pamoja katika sherehe hiyo iliyojumuisha Bwana Harusi, Ali Kiba, mke wake na wapambe wake na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali akiwemo Mbunge wa Viti Maalum, Mama Salma Kikwete, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimum, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde na Mwenyekiti wa UVCCM Kheri James.

Picha ya pamoja ya maharusi na viongozi wa chama na Serikali pamoja na Gvana wa Jiji la Mombasa, Rashid Bedzima (wa pili kulia).

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiteta jambo na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde na Wanamuziki, Ommy Dimpoz na Hamisi Mwanjuma MwanaFA.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akifurahia jambo na Msemaji wa Klabu ya Simba, Haji Manara na Mbunge wa Chalinze, Ridhiwan Kikwete wakati wa sherehe hiyo.

MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI(WCF) UMEKUWA MSHINDI WA PILI KATIKA MASUALA YA USALAMA NA AFYA MAHALA PA KAZI

April 30, 2018


Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba (kulia), akipokea tunzo na cheti kutoka kwa Bw. Eric Shitindi katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu baada ya MFuko kushinda nafasi ya pili katika masuala ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi katika maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani tarehe 28 Aprili katika Uwanja wa Kichangani Iringa.

MFUKO wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umeibuka mshindi wa pili katika masuala ya usalama na afya mahala pa kazi katika maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi nchini ambayo huadhimishwa duniani kote tarehe 28 Aprili kila mwaka.

Maadhimisho haya huratibiwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) nchini na kwa mwaka huu yamefanyika Mkoani Iringa yakitanguliwa na maonyesho kutoka kwa wadau kuanzia tarehe 26 Aprili na kufikia kileleni leo tarehe 29.

Mgeni Rasmi katika kilele cha Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu ameipongeza WCF kwa ushindi walioupata na kuwasihi kuendelea kutoa elimu kwa wadau wake.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa WCF Masha Mshomba, amefafanua kuwa moja ya malengo ya uanzishwaji wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni kukuza na kuendeleza mbinu za kuzuia ajali, magonjwa ama vifo mahala pa kazi. Mshomba ametoa ufafanuzi huo leo katika viwanja vya Kichangani mkoani Iringa baada ya kupokea tuzo na cheti cha Mshindi wa pili katika masuala ya afya ya usalama mahala pa kazi.

Aidha, akikabidhi tunzo hiyo kwa niaba ya Mgeni Rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw. Eric Shitindi ameupongeza Mfuko kwa kuendelea kufanya kazi vizuri katika nyanja tofauti tofauti pamoja na kwamba hauna miaka mingi sana toka uanzishwe. “Tunajivunia sana kuona ya kwamba Mfuko umeweza kulipa fidia stahiki kwa wakati, kitu ambacho kilikuwa changamoto hapo awali” Aidha, pongezi zangu ziwafikie kwa kuanzisha mifumo inayoboresha huduma kwa waajili na waajiliwa wote ikiwemo mifumo ya ki- electroniki inayowazezesha waajili kujisajili, kulipia michango na kufuatilia michango yao.

Mfuko umehitimisha maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi katika Mkoa wa Iringa na unajiandaaa na semina ya wadau itakayofanyika tarehe 30 Aprili na hatimaye kushiriki katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Tarehe 01 May 2018.

Katikati Bw. Eric Shitindi Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Mfuko baada ya kupokea tunzo na cheti katika maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi katika Uwanja wa Kichangani Iringa. (Akishikilia kombe pamoja na Bw. Shitindi ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Bw. Masha Mshomba

Bw. Ibrahim Mussa Afisa Madai Mwandamizi – WCF akimhudumia mteja aliyetembelea banda ya WCF katika maonyesho yaliyofanyika katika viwanja vya Kichangani Iringa.

Bw. Masha Mshomba akionyesha tuzo na cheti ambavyo Mfuko umetunukiwa.

Mkurugenzi wa Tiba na Tathmini wa WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar (wapili kushoto), Mkurugenzi wa Uendeshaji Bw. Anselim Peter wakiwa ameshika tuzo hiyo huku, Meneja Tathmini ya Usalama na Afya mahala pa Kazi wa Mfuko huo, Bi. Naanjela Msangi, (kulia) na Afisa Mkuu wa Matekelezo, Bi. Amina Likungwala, wakionyesha vyeti vya ushindi wa pili na cha ushiriki.

Mkurugenzi wa Tiba na Tathmini wa WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar (katikati), akiwa ameshika tuzo hiyo huku, Meneja Tathmini ya Usalama na Afya mahala pa Kazi wa Mfuko huo, Bi. Naanjela Msangi, (kulia) na Afisa Mkuu wa Matekelezo, Bi. Amina Likungwala, wakionyesha vyeti vya ushindi wa pili na cha ushiriki.


Afisa Uhusiano Mwandamizi wa WCF, Bw. Fulgence Sebera, akizungumza

MAAFISA UHAMIAJI NGAZI YA KATA WATASAIDIA KUPUNGUZA WIMBI LA UINGIAJI WAHAMIAJI HARAMU MKOANI TANGA

April 30, 2018
UWEPO wa Maafisa Uhamiaji Ngazi ya Kata umetajwa kuwa mwarobaini wakuzibiti kwa kiasi kikubwa kwa kupunguza wimbi la uingiaji wa wahamiaji haramu ambao wamekuwa wakiingia mkoani Tanga kutokana na kuwepo kwa ushirikiana baina yao na wananchi wa maeneo husika.

Hayo yalisemwa juzi na Kaimu Afisa Uhamiaji Mkoani Tanga (DCI) Salum Farahan Pichani Juu wakati akizungumza na mtandano huo ambapo alisema kwani maafisa hao wamekuwa wakishirikiana kwa ukaribu na wananchi .

Alisema hatua hiyo itakuwa suluhisho la kuhakikisha wanatokomeza vitendo vya wahamiaji hao kuingia mkoani hapa kwani itawasaidia kuweza kuwabaini kutokana na kuwepo kwa maafisa hao kwenye ngazi hizo.

“Labda niseme tu mipango ya kuhakikisha tunakabiliana kwa vitendo wimbi la wahamiaji haramu nchini tumeanza mikakati yake kwa kuimarisha kwenye kata na sasa tuna Afisa Uhamiaji kwenye kila kata nah iiitasaidia kuweza kushirikiana na wananchi kuzuia vitendo vya uingiajiwao “Alisema.

Alisema maafisa uhamiaji hao wanafanya kazi zaidi kwani wakati mwengine wanalazimika kwenda kwa wananchi hususani vijijini ambapo wahamiaji wamekuwa wakitumia njia za mipakani.

Hata hivyo alisema hivi sasa pia wameweka vizuizi kwenye maeneo mbalimbali mkoani Tanga kwa lengo la kuzibiti uingiaji wao ambavyo ni eneo la Vijinga, Horohoro wilayani Mkinga, Mkata wilayani Handeni na Kilapura wilaya ya Tanga.

PROFESA KABUDI AFUNGUA BARAZA LA WAFANYAKAZI TUME YA KUREKEBISHA SHERIA

April 30, 2018


Na Munir Shemweta, Morogoro

Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi amesisitiza umuhimu wa kuwashirikisha watumishi katika mipango ya uendeshaji Taasisi kwa kuwa suala hilo lipo kisheria.

Aidha, alisema kwa miaka yote Serikali imekuwa ikisisitiza Taasisi kujenga na kutekeleza utaratibu wa kushirikisha watumishi na hali hiyo inatokana na ukweli kuwa palipo na watumishi wengi pana mawazo mengi.Profesa Kabudi alisema hayo mwishoni mwa wiki wakati akifungua mkutano wa kumi na tatu wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) mkoani Morogoro.

‘’Ushirikishwaji watumishi kwenye mipango ya uendeshaji ofisi unasaidia kupata mawazo mengi na mapya yanayoweza kurahisisha uendeshaji wa ofisi na kutoa fursa ya kusikiliza kero na changamoto kwenye uendeshaji wa Taasisi na kushirikiana katika kutafuta ufumbuzi’’ alisema profesa Kabudi.

Aliongeza kuwa, kwa kushirikiana na watumishi ni dhahiri wanapata morari wa kushiriki kikamilifu kwenye utekelezaji wa mipango ya taasisi ambayo wao wenyewe walishiriki kuiandaa.Waziri huyo wa Katiba na Sheria alisema, ushirikishwaji unafanywa kupitia baraza la wafanyakazi kwa kuwa baraza ni chombo kinachowashirikisha wafanyakazi katika kupanga , kusimamia na kutekeleza mipango mbalimbali inayohusu shughuli za kazi za Taasisi kama zilivyoainishwa katika sheria za nchi.

Kwa mujibu wa Profesa Kabudi, Mabaraza hutoa fursa kwa wafanyakazi kushiriki katika maamuzi mbalimbali na kuboresha uhusiano baina ya wafanyakazi na uongozi pamoja na mazingira ya utendaji hasa mahala pa kazi hivyo baraza ni chombo cha kuimarisha na kuboresha demokrasia mahala pa kazi.

Amewataka wajumbe wa baraza wa Tume ya Kurekebisha Sheria kuzingatia suala la nidhamu kazini, misingi ya kazi na kutekeleza majukumu kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu. Aidha, alitaka uzembe kazini upigwe vita na suala la kufanya kazi kwa mazoea kukomeshwe na kubainisha kuwa,vipaumbele viwekwe katika kulinda rasilimali za Tume na kuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha na mali zake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Kurekebisha Sheria ambaye ni Katibu Mtendaji Tume Casmir Kyuki alisema katika kipindi cha Julai 2017 hadi Machi 2018 Tume yake imeweza kutekeleza majukumu yake kama yalivyoainishwa katika bajeti.

Ameyataja majukumu hayo kuwa ni kufanya mapitio ya Mfumo wa Sheria Unaosimamia Haki Jinai, Sheria ya Ushahidi, Uchambuzi wa Kesi za Mahakama ya Rufaa, Mfumo wa Sheria Unaosimamia Huduma ya Ustawi wa Jamii, Mfumo wa Sheria za Ufilisi pamoja na kutoa elimu ya sheria kwa umma.

Ameishukuru serikali kwa mabadiliko makubwa iliyoyafanya katika sekta ya sheria kupitia tangazo la serikali namba 48,49 na 50 ambapo yameleta muundo mpya kwa kuanzishwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka ya Jinai na ile ya Wakili Mkuu wa Serikali ili kuongeza tija na ufanisi katika utendaji kazi.

Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Kurekebisha Sheria uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, kushoto ni Katibu Mtendaji wa Tume Casmir Kyuki na kulia ni Katibu wa Baraza Ambokile Mwakasungula (Picha na Munir Shemweta-TUMESHERIA)

Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Casmir Kyuki (Kushoto) akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi kufungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine mkoani Morogoro, kulia ni Katibu wa Baraza Ambokile Mwakasungula (Picha na Munir Shemweta-TUMESHERIA)

Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akimsikiliza Katibu Msaidizi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Khalist Luanda mara baada ya kufunguka mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Tume ya Kurekebisha Sheria uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine mkoani Morogoro, katikati ni Katibu Msaidizi wa Tume (Idara ya Mapitio) Angelah Bahati (Picha na Munir Shemweta-TUMESHERIA)




Sehemu ya Wajumbe Baraza la Wafanyakazi la Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania wakimsikiliza Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi (hayupo pichani) wakati akifungua mkutano huo uliofanyika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine mkoani Morogoro.

Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Tume ya Kurekebisha Sheria katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine mkoani Morogoro.

UN YATAKA VYOMBO VYA HABARI KUKAZANIA UWAJIBIKAJI

April 29, 2018


Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Deodatus Balile akifungua kikao kati ya Jukwaa hilo na Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofadhiliwa na UN pamoja wadau mbalimbali uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.
Mkuu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa, Hoyce Temu akisoma hotuba kwa niaba ya Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez wakati wa mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofadhiliwa na UN pamoja wadau mbalimbali uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.

Mtaalamu wa Mawasiliano wa Shirika linaloshughulikia Watoto la Umoja wa Mataifa, Usia Nkhoma-Ledama akizungumzia uhusiano na ushirikiano kati ya TEF na mashirika ya Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofadhiliwa na UN pamoja wadau mbalimbali uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.


Washiriki wa kikao cha Jukwaa la Wahariri (TEF) wakifuatilia kwa umakini mada ya Malengo ya Dunia na ushirikiano wa kuwezesha malengo hayo kutekelezeka wakati wa mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofadhiliwa na UN pamoja wadau mbalimbali uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.

Allan Lawa wa Mwananchi Communications akizungumzia ushirikiano kati ya TEF na UN wakati wa mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofadhiliwa na UN pamoja wadau mbalimbali uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.

Mwenyekiti wa zamani wa Jukwaa la Wahariri (TEF) ambaye pia ni mmoja wa waanzilishi wa TEF, Theophil Makunga akitoa maoni yake kuhusu namna ambavyo Umoja wa Mataifa na TEF wanavyoweza kushirikiana wakati wa mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofadhiliwa na UN pamoja wadau mbalimbali uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.

Zourha Malisa wa Mwananchi Communications akielezea umuhimu wa ushirikiano wa UN na Jukwaa la Wahariri kuhusisha pia Vyombo vya Mitandaoni na Bloggers wakati wa mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofadhiliwa na UN pamoja wadau mbalimbali uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.

Katibu wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Neville Meena akielezea kwa undani namna ambavyo mafunzo yaliyo katika mkataba wao na UN yatakavyoendeshwa wakati wa mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofadhiliwa na UN pamoja wadau mbalimbali uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.

Mkuu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa, Hoyce Temu akisaini kanuni za ushirikiano kati ya TEF na UN kwa niaba ya Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Alvaro Rodriguez wakati wa mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofadhiliwa na UN pamoja wadau mbalimbali uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.

Mkuu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa, Hoyce Temu na Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Deodatus Balile wakibadilishana nakala za ushirikiano kati ya TEF na UN wakati wa mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofadhiliwa na UN pamoja wadau mbalimbali uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.


Na Mwandishi Wetu, Morogoro

Umoja wa Mataifa (UN) umetaka Vyombo vya Habari nchini kuweka mkazo katika kuandika na kutangaza masuala ya maendeleo na ya kiutu, hasa yale yanayoweza kujenga uelewa zaidi na kuchochea vitendo na uwajibikaji kwa manufaa ya Watanzania walio wengi.

Kauli hiyo imetolewa na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez, katika mkutano wa ndani wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) uliofanyika mwishoni mwa juma mjini Morogoro.

Katika hotuba yake hiyo iliyosomwa na Mkuu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini Hoyce Temu alisema, kwa kuwa Vyombo vya habari ndiyo kiunganishi kikuu kati ya watu, serikali na mashirika ya kimataifa hivyo ni wajibu wao kuandika habari zinazochochea maendeleo.

Aidha alisema kwa namna ya pekee, angependa kusisitiza umuhimu wa kuandika habari za hatua zinazopigwa katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) na Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano na vilevile MKUZA II na III.

“Haya ni maeneo muhimu kwa sababu aina ya mabadiliko tunayotaka kuyaona nchini Tanzania katika miaka michache ijayo yatawezekana tu ikiwa mipango hii mitatu itatekelezwa kwa ufanisi na kikamilifu kwa kuzingatia muda uliopangwa. Ni wajibu wenu, kama waandishi wa habari wanaojua kazi yao kushiriki kikamilifu katika wajibu huu wa kusimamia na kutolea taarifa masuala haya ili kuimarisha uwajibikaji” alisema Rodriguez.

Aidha alisema kwa kuwa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania unatekeleza mpango wa UNDAP II, ambao ni mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo unaolenga kuainisha vema programu ya ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Timu ya UN ya Nchi, ambao hatimaye utaimarisha fursa za maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa, vyombo vya habari vitaweza kusaidia kuhakikisha kwamba hakuna yeyote anayeachwa nyuma.

Serikali ya Tanzania na Timu ya Nchi ya UN zinashirikiana Dira ya Taifa na SDGs kwa kushughulikia maeneo matano ya kimaudhui ambayo ni Utawala wa Kidemokrasi, Haki za Binadamu & Usawa wa Jinsia—kuleta taasisi zenye uwazi na zenye kuwajibika na kuleta usawa wa jinsia.

Maeneo mengine ya kimaudhui ni Uwezo wa kujinusuru kwa kuimarisha usimamizi wa mazingira, upatikanaji wa nishati na kusaidia usimamizi wa wakimbizi na wahamiaji na kujenga taifa lenye ustawi kwa kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya, maji safi, usafi wa mazingira; kuimarisha lishe kwa wanawake na watoto wa chini ya umri wa miaka mitano.

Aidha maeneo mengine ni Ukuaji jumuishi ambao unasaidia, kupunguza umaskini na kuongeza fursa za kuongeza ajira, upatikanaji wa elimu ya msingi na usalama wa kijamii hasa kwa makundi ya maskini/wanyonge na mwisho ni kuwezesha mawasiliano, Huduma za Uwandani, Utetezi na Ushirika

Wakati huo huo UN na TEF wametiliana saini mkataba utakaowezesha kujenga uwezo kwa waandishi wa habari kufuatilia utekelezaji wa malengo ya Dunia yalihuishwa katika Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano na Mkuza III.

Mpango huo ambao umo ndani ya UNDAP ll unashirikisha maarifa, uvumbuzi mpya, utetezi na kutomwacha yeyote nyuma na kuunga mkono sera mpya ambazo zitasaidia utekelezwaji wa Malengo ya Dunia.

“Tuna matumaini makubwa na ushirikiano huu na TEF ili kuhakikisha mpango wetu kama unavyoelewa katika Kanuni za Ushirikiano ambao tumetia saini leo unatekelezwa kikamilifu na kuleta matokeo yanayotakiwa.” Alisema Zaman.


Ushirikiano kati ya TEF na UN kwa sasa una miaka mitano.
Usalama Mahala pa Kazi, TANESCO yaibuka Kidedea yakabidhiwa Ngao, IRINGA

Usalama Mahala pa Kazi, TANESCO yaibuka Kidedea yakabidhiwa Ngao, IRINGA

April 29, 2018
Shirika la Umeme TANESCO, limeibuka Kidedea Kwa Kupata Ushindi Kwenye Shindano la Usalama Mahali pa Kazi lililoendeshwa na Taasisi ya OSHA katika Viwanja vya Kichangani Manispaa ya IRINGA.

TANESCO imepata Ushindi huo Kupitia Sekta ya Huduma, ambapo imekabidhiwa Ngao na Cheti ikiwa ni Heshima ya Kutambuliwa Kama Taasisi ambayo imefanya Vizuri Kwa Kuzingatia Usalama Mahala pa Kazi.

Baada ya Shirika hilo la Umeme Kutangazwa Mshindi na Kukabidhiwa Ngao, Afisa Afya na Usalama Makao makuu NELSON MNYANYI amesema Elimu ya Afya na Usalama imekuwa Kichocheo Kikubwa katika Kupunguza Ajali kwa Wafanyakazi wa TANESCO pamoja na Wananchi kwa Ujumla.

Kwa Upande wake Afisa Afya na Usalama FRED KAYEGA akielezea Ushindi huo amesema licha ya Kupokelewa kwa Faraja, ni Motisha kwa TANESCO kuendelea Kufanya Vizuri zaidi Kwenye Sekta ya huduma Kwa Kuzingatia Usalama Mahala pa Kazi.

Katika Banda la TANESCO elimu mbalimbali kuhusu Afya na Usalama na Elimu Kuhusu Matumizi Bora na Sahihi ya Umeme iliweza Kutolewa kwenye Viwanja vya Kichangani Manispaa ya Iringa.

Waziri wa Viwanda, Biashara ya Uwekezaji CHARLES MWIJAGE akiangalia Baada la TANESCO mara Baada ya Kulitembelea Katika Viwanja vya Kichangani Manispaa ya Iringa, ambapo Shirika hilo limeibuka Mshindi Kwenye Sekta ya Huduma Kupitia Mashindano ya Usalama Mahala pa Kazi yaliyoendeshwa na Taasisi ya OSHA.
Maaofisa wa Shirika la Umeme TANESCO, Kutoka Kushoto Sylvester Matiki ( Afisa Masoko ), Nelson Mnyanyi ( Afisa Usalama ), Fred Kayenga ( Afisa Muandamizi Usalama na Afya Mahali pa kazi ) pamoja na Hassan Athumani (Mwenyekiti wa majadiliano TUICO TANESCO) wakifurahia Ushindi wa Ngao na Cheti Baada ya Kukabidhiwa Kama Washindi Kwenye Sekta ya Huduma Kupitia Mashindano yaliyoendeshwa na Taasisi ya OSHA katika Viwanja vya Kichangani Manispaa ya Iringa.



Wananchi Mbalimbali Katika Manispaa ya Iringa Waliofika Katika Banda la TANESCO katika Viwanja vya Kichangani Wakipewa Elimu Kuhusu Afya na Usalama pamoja na Matumizi Bora na Sahihi ya Umeme.
Afisa wa TANESCO, Kitengo cha Huduma kwa Wateja ENIDY ELSON akitoa Elimu ya matumizi Bora ya Umeme kwa Wanafunzi na Wananchi Waliofika Kwenye Banda la Shirika hilo Wakati wa Shindao la Usalama Mahala pa Kazi lilioendeshwa na Taasisi ya OSHA katika Viwanja vya Kichangani Manispaa ya Iringa.

MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI(WCF) UMEKUWA MSHINDI WA PILI KATIKA MASUALA YA USALAMA NA AFYA MAHALA PA KAZI

April 29, 2018
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba (kulia), akipokea tunzo na cheti kutoka kwa Bw. Eric Shitindi katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu baada ya MFuko kushinda nafasi ya pili katika masuala ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi katika maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani tarehe 28 Aprili katika Uwanja wa Kichangani Iringa.


                          NA MWANDISHI WETU, IRINGA

MFUKO wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umeibuka mshindi wa pili katika masuala ya usalama na afya mahala pa kazi katika maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi nchini ambayo huadhimishwa duniani kote tarehe 28 Aprili kila mwaka.

Maadhimisho haya huratibiwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) nchini na kwa mwaka huu yamefanyika Mkoani Iringa yakitanguliwa na maonyesho kutoka kwa wadau kuanzia tarehe 26 Aprili na kufikia kileleni leo tarehe 29.

Mgeni Rasmi katika kilele cha Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu ameipongeza WCF kwa ushindi walioupata na kuwasihi kuendelea kutoa elimu kwa wadau wake.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa WCF Masha Mshomba, amefafanua kuwa moja ya malengo ya uanzishwaji wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni kukuza na kuendeleza mbinu za kuzuia ajali, magonjwa ama vifo mahala pa kazi.

Mshomba ametoa ufafanuzi huo leo katika viwanja vya Kichangani mkoani Iringa baada ya kupokea tuzo na cheti cha Mshindi wa pili katika masuala ya afya ya usalama mahala pa kazi.

Aidha, akikabidhi tunzo hiyo kwa niaba ya Mgeni Rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw. Eric Shitindi ameupongeza Mfuko kwa kuendelea kufanya kazi vizuri katika nyanja tofauti tofauti pamoja na kwamba hauna miaka mingi sana toka uanzishwe. “Tunajivunia sana kuona ya kwamba Mfuko umeweza kulipa fidia stahiki kwa wakati, kitu ambacho kilikuwa changamoto hapo awali” Aidha, pongezi zangu ziwafikie kwa kuanzisha mifumo inayoboresha huduma kwa waajili na waajiliwa wote ikiwemo mifumo ya ki- electroniki inayowazezesha waajili kujisajili, kulipia michango na kufuatilia michango yao.

Mfuko umehitimisha maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi katika Mkoa wa Iringa na unajiandaaa na semina ya wadau itakayofanyika tarehe 30 Aprili na hatimaye kushiriki katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Tarehe 01 May 2018.

Katikati Bw. Eric Shitindi Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Mfuko baada ya kupokea tunzo na cheti katika maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi katika Uwanja wa Kichangani Iringa. (Akishikilia kombe pamoja na Bw. Shitindi ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Bw. Masha Mshomba

Bw. Ibrahim Mussa Afisa Madai Mwandamizi – WCF akimhudumia mteja aliyetembelea banda ya WCF katika maonyesho yaliyofanyika katika viwanja vya Kichangani Iringa.
 Bw. Masha Mshomba akionyesha tuzo na cheti ambavyo Mfuko umetunukiwa.
  Mkurugenzi wa Tiba na Tathmini wa WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar (wapili kushoto), Mkurugenzi wa Uendeshaji Bw. Anselim Peter wakiwa ameshika tuzo hiyo huku, Meneja Tathmini ya Usalama na Afya mahala pa Kazi wa Mfuko huo, Bi. Naanjela Msangi, (kulia) na Afisa Mkuu wa Matekelezo, Bi. Amina Likungwala, wakionyesha vyeti vya ushindi wa pili na cha ushiriki.
Mkurugenzi wa Tiba na Tathmini wa WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar (katikati), akiwa ameshika tuzo hiyo huku, Meneja Tathmini ya Usalama na Afya mahala pa Kazi wa Mfuko huo, Bi. Naanjela Msangi, (kulia) na Afisa Mkuu wa Matekelezo, Bi. Amina Likungwala, wakionyesha vyeti vya ushindi wa pili na cha ushiriki.







Afisa Uhusiano Mwandamizi wa WCF, Bw. Fulgence Sebera, akizungumza