WABUNGE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI WATEMBELEA IDARA YA UHAMIAJI

November 03, 2016
uv
Mwenyekiti wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki Tawi la Tanzania, Makongoro Nyerere(kulia) akizungumza wakati wa mkutano na Wakuu wa Idara ya Uhamiaji(hawapo pichani).Wabunge hao walitembelea idara hiyo kujifunza  shughuli zinazofanywa na idara  hiyo . Wengine ni Wabunge  Shyrose Bhanji(kulia) na   Angela Kizigha(kushoto). Mkutano huo umefanyika   jijini Dar es Salaam.( Picha na Abubakari Akida)
uv5
 
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Shyrose Bhanji akizungumza wakati wa mkutano na Wakuu wa Idara ya Uhamiaji(hawapo pichani).Wabunge hao walitembelea idara hiyo kujifunza  shughuli zinazofanywa na idara .Kulia ni Mbunge Makongoro Nyerere  na Kushoto ni  Angela Kizigha.Mkutano huo umefanyika   jijini Dar es Salaam.( Picha na Abubakari Akida)
uv1
Kaimu Kamishna  Jenerali   wa  Uhamiaji, Victoria Lembeli  akizungumza wakati wa mkutano na Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki waliotembelea idara  hiyo, ikiwa ni ziara yao ya kujifunza shughuli  mbalimbali zinazofanywa  na idara  hiyo ikiwemo suala la pasi za kusafiria katika nchi hizo.Ziara hiyo imefanyika  jijini Dar es Salaam.(Picha na Abubakari Akida
uv2
Kaimu Kamishna  Utawala  na  Fedha  wa Idara ya Uhamiaji, Naibu Kamishna Abbas Irovya,  akizungumza wakati wa mkutano na Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki waliotembelea idara ya Uhamiaji kujadili shughuli zinazofanywa na idara hiyo, ikiwa ni ziara yao ya kujifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na nchi za Afrika Mashariki ikiwemo  suala la pasi za kusafiria katika nchi hizo.Ziara hiyo imefanyika  jijini Dar es Salaam.( Picha na Abubakari Akida)
uv3
 Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Abdullah Mwinyi akizungumza wakati wa mkutano na Wakuu wa Idara ya Uhamiaji(hawapo pichani).Wabunge hao walitembelea idara hiyo kujifunza  shughuli mbalimbali zinazofanywa  ikiwemo utoaji wa pasi za kusafiria katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kushoto ni  Katibu wa Wabunge wa Afrika Mashariki Twaha Taslima. Mkutano huo umefanyika  jijini Dar es Salaam. (Picha na Abubakari Akida)
uv4
Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Victoria Lembeli(wanne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wabunge  wa Bunge la Afrika Mashariki Tawi la Tanzania baada ya kutembelea Makao Makuu ya Idara hiyo katika kujifunza mambo mbalimbali yanayofanywa na idara .Watatu kulia ni Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania katika Bunge hilo, Makongoro Nyerere.Ziara hiyo imefanyika   jijini Dar es Salaam.(Picha na Abubakari Akida)

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »