SHIRIKISHO la
soka nchini (TFF) limeshauriwa kuangalia namna ya kuzitafutia ufadhili timu
zinazoshiriki michuano ya Ligi daraja la kwanza nchini ili kuweza kuongeza
ushindani na ladha ya mashindano hayo kama ilivyokuwa kwa ligi kuu soka
Tanzania.
Hatua hiyo
inatokana na timu nyingi zinazoshiriki ligi hiyo kutokuwa na uwezo wa kutosha
jambo ambalo linapunguza ushindani na kuzifanya timu zinazojiweza kucheza vema
na kuweza kufikia malengo waliojiwekea.
Hayo yalisemwa hivi karibuni na Kocha Mkuu wa timu ya African Lyon Charles Ottieno mara baada ya
kumalizika kwa mechi yao dhidi ya African Sports ambapo timu hiyo ilikubali
kichapo cha bao 1-0,mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini
hapa.
Katika mchezo
huo bao la African Sports liliwekwa wavuni na Hassani Materema kunako dakika ya
10 baada ya kumalizia kazi nzuri iliyokuwa imefanywa na Ayoub Masoud ambapo bao
hilo lilidumu mpaka timu zote zinakwenda mapumziko.
Kipindi cha pili
kilianza kwa kasi ambapo kila timu iliingia uwanjani hapo ikiwa na lengo la
kutaka kupanda ushindi ambapo African Lyon walionekana kubadilika na kuanza
kulisakama lango la wapinzani wao bila mafanikio ya aina yoyote yale.
Naye kwa upande
wake,Kocha wa African Sports,Ally Maliki alisema wanamshukuru mungu kwa kupata
pointi tatu muhimu kwenye mechi hiyo na kuhaidi kujipanga vema ili kufanya
vizuri kwenye michezo yao iliyosalia lengo likiwa kuipandisha timu hiyo kucheza
Ligi kuu msimu ujao.
Kwenye mechi
hiyo kikosi cha African Sports kiliwakilishwa na Yusuph Yusuph,Ayoub
Masoud,Issa Shabani,Juma Shemvuni,Mwaita Ngereza,Hussein Issa,Evarigestus
Munjwahuka,Daudi Milandu,Hassani Materema,Ally Ramadhani na James Mendy.
Kwa upande wa
African Lyon wao waliwakilishwa na Abubakari Hashim,Omari Kindamba,Kassim
Simbaulanga,Baraka Jaffari,Yusuph Mlipili,Hamadi Manzi,Miraji Athuman,John
Simbeta,Omary Ramadhani,Kashakala Ndere na Abdallah Mguihi.

EmoticonEmoticon