RC GAWALA AKABIDHI ZAWADI ZA RAIS KIKWETE KWA VITUO VIWILI TANGA.

October 15, 2013

MKUU WA MKOA WA TANGA ,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA KULIA AKISALIMIANA NA AFISA MFAWIDHI WA MAHABUSU YA WATOTO JIJINI TANGA NG'WANZA MUHANGWA LEO KABLA YA KUWAKABIDHI ZAWADI KUTOKA KWA RAIS WA JAMHURI WA MUUNGANO WA TANZANIA JAKAYA MRISHO KIKWETE ZA SIKUKUU YA  IDD EL HAJI

KULIA MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIMKABIDHI MBUZI AFISA MFAWIDHI WA MAHABUSU YA WATOTO  NGWANZA MUHANGWA WA KWANZA KUSHOTO ANAYESHUHUDIA NI MKUU WA WILAYA YA TANGA,HALIMA DENDEGO NA DIWANI WA KATA YA USAGARA CARLOS HIZZA

KULIA MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIKABIDHI MBUZI KWA KITUO CHA KUTUNZA WAZEE MWANZANGE

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA ALIYESIMAMA AKIZUNGUMZA NA WAZEE WANAOISHI KATIKA KITUO CHA KUTUNZIA WAZEE MWANZANGE WA KUSHOTO KWANZA NI MKUU WA WILAYA YA TANGA,HALIMA DENDEGO NA KULIA KWAKE NI DIWANI WA KATA YA DUGA MH.KOMBO

WAZEE WAKIMSIKILIZA MKUU WA MKOA KWA UMAKINI MKUBWA LEO

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WAZEE WANAOISHI KATIKA KITUO CHA KUWATUNZA WAZEE MWANZANGE MARA BAADA YA KUWAKABIDHI ZAWADI ZA IDDI EL HAJ KUTOKA KWA MH RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAKAYA MRISHO KIKWETE.
MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIKABIDHI ZAWADI ZA SIKUKUU YA IDDI EL HAJI ZILIZOTOLEWA NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,MH JAKAYA MRISHO KIKWETE WAZEE WANAOISHI KWENYE KITUO CHA KUWALEA MWANZANGE JIJINI TANGA.

PICHA ZOTE NA PASKAL MBUNGA,TANGA.
TANGA.
MKUU wa Mkoa wa Tanga ,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa leo amekabidhi zawadi zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwet kwa vituo viwili kwa ajili ya sikukuu ya Idd El Haji.

Zawadi zilizotolewa ni pamoja na mbuzi mmoja kwa kila kituo,mchele,mafuta ya kupikia,chumvi na sabuni.

Vituo hivyo ni kituo cha mahabusu nya watroto cha barabara ya 15/16 na kituo cha kutunzia wazeee cha mwanzange vyote vya jijini Tanga.

Awali akisoma kwa mkuu wa mkoa wa Tanga,Afisa Ustawi wa Jamii kwenye kituo hicho,Clara Kibanga walimshukuru Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kikwete kwa kuwapatia msaada huo na kuwakumbuka wazee.

Katika msafara huo kulikuwa na viongozi mbalimbali akiwemo mkuu wa wilaya ya Tanga, Halima Dendego,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga,Juliana Malange na wakuu wa idara kutoka halmashauri ya Jiji la Tanga.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »