Na Oscar Assenga, Tanga.
MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tanga, Kassim
Mbuguni amewataka vijana kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele kukulinda na
kukitumikia chama hicho pamoja na kujenga mshikamano miongoni mwao.
Mbuguni alitoa rai hiyo mwishoni mwa wiki wakati akifungua
kikao cha baraza la Jumuiya ya Vijana Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tanga
(UVCCM) kilichofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa chama hicho uliopo
barabara 20 jijini Tanga.
Alisema ili kuweza kuhakikisha chama hicho kinazirudisha kata
tisa zilizochukuliwa na vyama vya upinzani katika uchaguzi mkuu ujao lazima
umoja huo unapaswa kuwa macho kujua kinachotakiwa kwenye kata zao ili kuyafanyia kazi
kwani chama hicho kipo kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wote.
“Jumuiya ya umoja wa vijana lazima wawe macho ndani ya chama
kwa kutoa taarifa na kinachotokea ndani ya chama lengo likiwa kuzifanyia kazi
na kusukuma gurudumu la maendeleo kwenye maeneo yao “Alisema Mbuguni.
Katika kikao hicho Jumuiya hiyo kilipitisha majina ya wajumbe
wa kamati ya mipango, uchumi na fedha itakayokuwa na kazi ya kuhakikisha wanabuni
miradi ambayo itaiwezesha jumuiya hiyo kuwa na vitega uchumi vyao wenyewe ili
iweze kusimama imara lakini pia itawasaidia kujiendesha katika shughuli
mbalimbali za maendeleo.
Majina ya wajumbe ambao wataunda kamati hiyo yalipitishwa na
kikao cha baraza la Vijana wilaya ya Tanga ni Mwenyekiti,Ameet Ranjit,Katibu
Akida Machai, ambao watakuwa wakishirikiana na wajumbe Mbaruku Asilia,Khalid
,Yazidu Msika,Abdul Ahmed Kassim Kassim,huku wajumbe wengine wakina mama
wakitarajiwa kuongeza kwenye kamati hiyo.
Awali akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa UVCCM
wilaya ya Tanga, Salim Perembo aliwataka vijana kuendeleza mshikamao na umoja
ili kuweza kusukuma gurudumu la maendeleo kwenye umoja huo lengo likiwa
kukiimarisha chama hicho huku akiwataka vijana kutokubali kutumiwa kama ngazi.
Kikao hicho kilihudhuriwa na wajumbe 60 kutoka kata za
Chongoleani, Tangasisi, Kiomoni, Usagara, Maweni, Duga,Msambweni,Majengo,Mzingani,Marungu,Chumbageni,Kirare,Ngamiani
kusini,Nguvumali,Central ,Mzizima,Pongwe na Ngamiani .
Mwisho.
EmoticonEmoticon