TANESCO TANGA YAPATA HASARA YA MILIONI 200 NDANI YA KIPINDI CHA MIAKA MIWILI ULIOTOKA NA WIZI WA MIUNDO MBINU.

July 22, 2013

(Meneja wa Tanesco Mkoa wa Tanga,Johnson Mwigune akiwa ofisni mwake leo mara baada ya kuzungumza na waandishi wa habari)

Na Oscar Assenga, Tanga.
SHIRIKA la Umeme Mkoa wa Tanga (TANESCO)limepata hasara ya shilioni milioni 200 ndani ya kipindi cha miaka miwili iliyopita kutokana na wizi wa miundombinu yake ikiwemo wezi wa nyaya na mafuta ya transfoma unaofanyika katika maeneo mbalimbali mkoani hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo ofisini kwake ,Meneja wa Tanesco Mkoa wa Tanga,Meneja wa Tanesco Mkoa wa Tanga,Johson Mwigune alisema wizi huo unafanyika hasa katika wilaya tatu ambazo ni sugu kwa matukio ya aina hiyo ambazo ni Muheza,Korogwe na Lushoto.

Mwigune alisema wizi huo unaliletea athari kubwa shirika hilo ikiwemo kulikosesha mapato wakati umeme huo ukipotea bure bila ya kutumika na kuwasababishia watumiaji wa nishati hiyo usumbufu mkubwa na uharibifu wa mali zao.

Meneja huyo alisema kwa upande wao wamejipanga vilivyo ili kuweza kuhakikisha wanakabiliana na wezi wa miundo mbinu hiyo kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na ushirikishwaji wa wanakijiji katika maeneo husika ili kulitokomeza suala hilo.

Aidha alisema katika siku za hivi karibuni kumetoka wizi wa nyaya za umeme za shirika hilo ambao ulifanyika eneo la Kerenge Makaburini wilayani Korogwe ambapo walifanya jitihada za kuwasaka na baadae kufanikiwa kuwakamata na kuwahukumu na kufanikiwa kumuhukumu Twaha Dege miaka 18 katika kesi iliyosikilizwa kwenye mahakama ya wilaya ya Korogwe.

Aliongeza kuwa tukio lengine ambalo limetokea ni watu kujiunganishia huduma ya umeme bila kufuata taratibu ambapo walilifuatilia na kufanikiwa kuwakamata watu wawili mmoja akiwa ni mfanyakazi mwengine akiwa sio mfanyakazi ambapo hukumu yao ilitoka kwa kila mmoja kutumikia kifungo cha miaka minne ambapo aliyekuwa mfanyakazi wao alifariki dunia.

Hata hivyo,Mwigune alitoa wito kwa wananchi kushirikiana na shirika hilo kwenye kulinda miundombinu yake kwa kutoa taarifa hasa pale ambapo watabaini kuwepo kwa vitendo vya wizi ,uharibifu vinafanyika kwenye maeneo yao.

Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »