Ashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kukutwa na Bunduki mbili kinyume cha Sheria

July 18, 2013
Na Hamisi Ramadhani,Handeni.
MKULIMA mmoja wa kijiji cha Sua Wilayani Handeni Mkoani Tanga, anashikiliwa na Polisi Wilayani hapa kwa tuhuma za kukutwa na Bunduki mbili aina ya magobole alizokuwa akizimiliki kinyume na sheria.
 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe, alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi saa 11.30 jioni katika kijiji hicho baada ya raia wema kutoa taarifa polisi.
 
Alisema kuwa kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo ni baada ya wananchi kuwa na hofu na ndipo raia wema wakatoa taarifa polisi kwa kuhofia kuwa mtuhumiwa huyo anaweza kufanya uharifhu wakati wowote. 
 
Alilitaja jina la mtuhumiwa huyo kuwa ni Hamadi Ally Waziri (43) mkazi wa kijiji cha Sua ambaye alikamatwa nyumbani kwake baada ya polisi kufanyiwa upekuzi ndani kwake na ndipo wakazikuta bunduki mbili aina ya Magobole.
 
Kamanda Massawe aliwapongeza raia wema kwa kutoa taarifa hizo na kuwataka kuwa na ushirikiano na jeshi la polisi ili kuweza kutokomeza uhalifu ambayo mkoani hapa.
 
Mwisho

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »