Na Pascal Mbunga,Tanga.
KIWANDA
maarufu cha kutengeneza chokaa cha Kneelkant kilichopo nje kidogo ya
jiji la Tanga kimewaachisha kazi idadi kubwa ya wafanyakazi wake baada
ya kupunguza uzalishaji mali kiwandani hapo.
Akizungumza
na Blogi ya Tanga Raha Meneja wa Kiwanda, Rashid
Hamoud alisema hali ya biashara imekuwa mbaya baada ya nchi zinazonunua
bidhaa hizo kuingia katika machafuko ya kivita.
Meneja
huyo ameyataja masoko ya bihaa zake kuwa ni nchi za maziwa makubwa
ambazo ni pamoja na Kongo, Burundi, Zimbabwe, Zambia na Malawi.
Amesema
kukosekana kwa hali ya usalama katika baadhi ya nchi hizo
kumesababisha usafirishaji wa bidhaa kuwa katika hatari ya kutekwa
wakati na sehemu yeyote njiani.
Hamoud
amefahahmisha kuwa kutokanana hali hiyo, uongozi wa kiwanda ulilazimika
kuwaachisha kazi zaidi ya nusu ya idadi ya wafanyakazi wote kiwandani
hapo.
Katika
kipindi cha miaka miwili iliyopita, kiwanda cha Kneelkanth kimeweza
kuliingizia taifa pato la shs.bilioni 45 baada ya kuuza bidhaa tani
12,000 za chokaa katika nchi za maziwa makubwa.
Kiwanda
cha Kneelkanth ni mradi ulioanzishwa mwaka 2009 na Mtanzania Rashid
Hamoud akishirikiana na mwekezaji wa India , Kumar Pajara na kuanza
kazi rasmi mwaka 2010.
(Mwisho)
EmoticonEmoticon