KIWANDA CHA CHOKAA CHAPUNGUZA UZALISHAJI

July 18, 2013

Na Pascal Mbunga,Tanga.

KIWANDA maarufu cha kutengeneza chokaa cha Kneelkant kilichopo nje kidogo ya jiji la Tanga kimewaachisha kazi idadi kubwa ya wafanyakazi wake baada ya kupunguza uzalishaji mali kiwandani hapo.
  
Akizungumza  na Blogi ya Tanga Raha Meneja wa Kiwanda, Rashid Hamoud alisema hali ya biashara imekuwa mbaya baada ya nchi zinazonunua bidhaa hizo kuingia katika machafuko ya kivita.
Meneja huyo ameyataja masoko ya bihaa zake kuwa ni nchi za maziwa makubwa ambazo ni pamoja na Kongo, Burundi, Zimbabwe, Zambia na Malawi.
Amesema kukosekana kwa hali  ya usalama katika baadhi ya nchi hizo kumesababisha usafirishaji wa bidhaa kuwa katika hatari ya kutekwa wakati na sehemu yeyote njiani.
Hamoud amefahahmisha kuwa kutokanana hali hiyo, uongozi wa kiwanda ulilazimika kuwaachisha kazi zaidi ya nusu ya idadi ya wafanyakazi wote kiwandani hapo.
Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, kiwanda cha Kneelkanth kimeweza kuliingizia taifa pato la shs.bilioni 45 baada ya kuuza bidhaa tani 12,000 za chokaa katika nchi za maziwa makubwa.
Kiwanda cha Kneelkanth ni mradi ulioanzishwa mwaka 2009 na Mtanzania Rashid Hamoud akishirikiana na mwekezaji wa India , Kumar  Pajara na kuanza kazi rasmi mwaka 2010.
(Mwisho)
  

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »