CHAMA
cha Demokrasia na Maendeleo wilaya ya Tanga kimesema ushindi walioupata
kwenye kata nne za Mkoa wa Arusha katika uchaguzi mdogo wa udiwani
mkoani Arusha uliofanyika hivi karibuni ni ishara tosha kuwa chama hicho kinakubalika na wananchi wa mkoa huo.
Uchaguzi huo ulifanyika hivi
karibuni kwenye kata za Kaloleni,Themi,Kimandulu na Elirahi ambapo chama
hicho kiliweza kuchukua nafasi hizo kwa ushindi wa kushindo na
kuwabwaga wapinzani wao.
Akizungumza na Blog hii, Katibu wa Chama hicho wilaya ya Tanga,Khalid Rashid amesema
kuwa licha ya chama hicho kukubalika mkoani humo lakini pia ni ishara
tosha kuwa katika ujazo mkuu ujao wa mwaka 2015 vyama vyengine visahau
kuchukua nafasi kwenye ukanda wa kaskazini ambapo ndio ngome ya chama
hicho.
Rashid amewapongeza
wananchi wa Arusha kwa kazi kubwa ya kukiamini chama hicho pamoja na
kukupa ridhaa ya kuwaongoza kwani nafasi hiyo inaonyesha ushirikiano ma
umoja baina ya viongozi wa kanda na Taifa ilivyoweza kutengeneza
mazingira mazuri kuhakikisha wanapata ushindi kwenye uchaguzi huo.
Ameongeza kuwa
wanaimani kuwa kwa siku zijazo Meya wa Jiji la Arusha atapatikana
kupitia chama hicho kutokana na wingi wa idadi ya madiwani waliopo
kwenye baraza la madiwani ambapo alisisitiza mshikamano wao ndio
ulioleta matokeo mazuri kwa chama hicho.
Aidha amesema katika
wilaya ya Tanga chama hicho walifanya mikutano sana ya kuhamasisha
wananchi kujiunga na chama hicho lengo lilikuwa ni kutengeneza chadema
msingi kwa kila mtaa,vijiji na vitongoji ambapo mikutano hiyo waliifanya
kwenye kata 7 ambazo ni Mabawa,Msambweni,Duga,
Makorora, Central, Chumbageni na Nguvumali lengo likiwa ni kutembelea kata
zote 24 za halmashauri ya Jiji la Tanga.
Amesema mikutano hiyo ilikuwa na malengo matatu ya
kuzungumzia suala la chadema ni msingi na kuzungumzia kuhusu bajeti ya
halmashauri ya Jiji la Tanga ikiwemo kupinga kauli ya waziri mkuu ambayo
aliitoa bungeni ya sasa hivi watu watakaoleta vurugu wapigwe tu ambapo
chama hicho kinaona kitendo hicho serikali haikutenda haki kwa wananchi.
Mwisho.
EmoticonEmoticon