MECHI YA STAND, KIMONDO NAYO KUPIGWA JUMAPILI

July 11, 2013
Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam.
Mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kati ya Stand United FC ya Shinyanga na Kimondo SC ya Mbeya iliyokuwa ichezwe Jumamosi  imesogezwa mbele kwa siku moja.

Akizungumza na Blog hii,Ofisa habari wa shirikisho la soka hapa nchini TFF,Ipichani kulia)Boniface Wambura alisema timu hizo sasa zitacheza Jumapili  kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.


Kimondo ilishinda bao 1-0 mechi ya kwanza iliyochezwa Julai 6 mwaka huu Uwanja wa Kumbukumbu ya
Sokoine jijini Mbeya.
 
Mechi nyingine ya ligi hiyo itakuwa kati ya Friends Rangers ya Dar es Salaam na Polisi Jamii ya Mara, na itafanyika kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Mwamuzi wa mechi hiyo ni Hans Mabena kutoka Tanga.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »