Uhamiaji waanza kuwaandikisha walowezi wa Malawi na Msumbiji.

May 28, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
IDARA ya Uhamiaji Mkoa wa Tanga imeanza kuwaandikisha walowezi wa Malawi na Msumbiji waliokuja mkoani hapa katika kipindi cha miaka ya nyuma ambao walikuwa wakifanya kazi kwenye mashamba ya mkonge na kazi za majumbani.

Akizungumza na blog hii, Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga, Sixtus Nyaki alisema uandikishwaji watu hao unafanyika baada ya kuzungumza nao katika mkutano wa kuwaelimisha kwa kushirikiana na wenyeviti wa mitaa, vitongoji na maafisa watendaji wa kata  na vijiji.

Nyaki alisema wakati wakiwa wanaendesha zoezi hilo wanakumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo baada yao kutokukubali kuandikishwa kwa kuona kama wanafukuzwa hapa nchini hali ambayo inapelekea kuwa na ugumu kiasi.

Alisema katika kupambana na wimbi la uhamiaji haramu mkoani hapa idara hiyo imefungua ofisi ya uhamiaji wilayani Korogwe lengo likiwa ni kuzibiti ongezeko la wahamiaji wanaoingia mkoani hapa kutoka nchi mbalimbali duniani.

Ofisa huyo alisema ofisi hiyo itakuwa na kazi ya kuwahudumia wilaya ya Korogwe na wilaya ya Lushoto wakati idara hiyo ikiendelea kujipanga kwa ajili ya kufungua ofisi nyengine wilayani humo ikiwa ni mkakati wa kupambana na wahamiaji haramu.

Aidha alisema tayari wameshapata ofisi hiyo na ukarabati wake unaendelea ambapo unatarajiwa kukamilika muda sio mrefu ili iweza kufanya kazi zake ambapo aliongeza kuwa idara hiyo pia imeweka vizuizi katika barabara za Tanga-Horohoro, Tanga-Arusha na Tanga-Dar.

Hata hivyo aliogeza kuwa wataendelea kutoa elimu ya uhamiaji shirikishi kwa wananchi katika maeneo mbalimbali lengo likiwa ni kupunguza wimbi la wahamiaji haramu mkoani hapa pamoja na kuweza mikakati ya kupunguza uwepo wapo.

   Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »