JUMLA ya timu 43 zinatarajiwa kushiriki
mashindano ya Umoja wa michezo shule za Sekondari nchini (Umiseta) ngazi wilaya
ya Tanga ambayo yanatarajiwa kuanza Machi 22 mwaka huu.
Mratibu wa Mashindano hayo, Damiani
Mabena aliiambia blogi hii kuwa mashindano hayo yatachezwa viwanja
saba ambavyo zimeteuliwa na kamati ya inayoratibu mashindano hayo.
Mabena alisema
vituo vitakavyochezewa ni shule za sekondari
Popatlaly, Usagara, Galanosi,Rosimini, Kiomoni, Tanga Ufundi pamoja na kituo
maalumu kilichopo Ndaoya na Marungu
Aliitaja michezo
ambayo itashindaniwa katika mashindano hayo msimu huu kuwa ni mchezo wa mpira wa
miguu,mchezo wa mpira wa wavu,mchezo wa riadhaa,mchezo wa kikapu,mchezo wa mpira
wa mikono,mpira wa meza na mpira wa pete.
Mratibu huyo
alizitaka shule ambazo zimethibitisha kushiriki kuwa ni Pande,Kirare,Pongwe,
Marungu,Mwapachu,
Chumbageni, Mnyanjani,Mikanjuni,Kihere,Toledo,Macechu,Nguvumali,Old Tanga, Haki,
Besha, Japani,Eckernforde Girls, Rosmini, Horten, Chongoleani, Mabokweni,
Tongoni,Maweni,Maawal na Arafah.
Alizitaja shule
nyingine kuwa ni Eckernforde, Popatlaly, Usagara, An
–Noor,Al-Kheir,St.Christina,Tanga Ufundi, Kiomoni,Sahare, Jumuiya, Mkwakwani,
Galanosi, Eckernforde Cambridge, Ndaoya, Coastal, Elohim, Msambweni na Don
Bosco.
Mabena alizitaka
timu za shule zinazotarajiwa kushiriki mashindano hayo zianze maandalizi mapema
ili kuweza kuleta msisimuko zaidi wakati wa mashindano hayo.
Mwisho.
EmoticonEmoticon