Benki ya CRDB yazindua huduma ya bima yenye misingi ya sharia kwa Watanzania wote

February 29, 2024

 


Dar es Salaam. Tarehe 28 Februari 2024: Ikiwa na uzoefu wa takriban miaka minne sasa Benki ya CRDB imezindua huduma za bima zinazozingatia misingi ya shariah zijulikanazo kama Takaful kwa ajili ya wateja wanaofuata imani ya Kiislamu na wananchi wengine wanaozingatia misingi ya dini hiyo.

Akizindua huduma hizo, Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania, Dkt. Abubakar Zubeir ameipongeza Benki ya CRDB kwa kuonyesha njia katika huduma zake kwa kutambua kwamba wapo baadhi ya wateja ambao hushindwa kupata huduma kutokana na imani zao za kidini.
“Hongereni sana kwa ubunifu huu. Shariah ni sehemu muhimu kwa waumini wa Kiislamu ingawa wapo watu wa imani nyingine wanaozipenda na kuzitekeleza kanuni na misingi ya shariah. Kwa bima hizi za Takaful, naamini mtakuwa mmekata kiu ya wengi nami nawaomba Waislamu wenzangu na watu wote wanaoifuata misingi ya shariah kulinda mali na maisha yao kwa bima za Takaful,” amesema Sheikh Zubeir.

Kwa upande wake, Kamshna wa Bima na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Dkt. Baghayo Saqware amesema ubunifu unaotatua changamoto zinazowakwamisha Watanzania kutumia huduma za bima unahitajika ili kuikuza sekta hiyo na kuwawezesha wananchi wengi kuwa na uhakika wa mipango na miradi wanayoitekeleza.
“Takaful ni huduma inayowakaribisha watu wenye imani ya Kiislamu ambao hawaridhishwi na huduma za bima ya kawaida ambazo zina riba. Takaful sio tu ni huduma za bima bali uwekezaji unaomnufaisha mteja pamoja na kampuni inayotoa huduma hizo. Kwa kutumia mtandao wenu mpana wa matawi, naamini Benki ya CRDB mtazifikisha huduma hizi kila kona ya nchi,” amesema Dkt. Saqware. 

Mwaka 2021 Benki ya CRDB ilianzisha kitengo maalum cha huduma zinazofuata misingi ya Shariah yaani CRDB Al Barakah Banking hali iliyoifanya kuwa benki ya kwanza nchini kufikisha huduma zinazozingatia shariah nchi nzima. Katika kipindi hicho chote mpaka sasa, CRDB Al Barakah inao wateja zaidi ya 135,000 na kufanya uwezeshaji wa zaidi ya Shilingi bilioni 125, sehemu kubwa ikielekezwa kwa wajasiriamali wadogo na wa kati.
Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Boma Raballa amesema siku zote benki inaendelea kuboresha huduma na bidhaa zake na mwaka jana ilianzisha huduma maalum ya uwezeshaji wa safari za Ibada ya Hijja na Umrah.

“Katika mwendelezo wa kuboresha huduma zetu, Benki ya CRDB kwa kushirikiana na wenzetu, Zanzibar Insurance Corporation (ZIC) Takaful, leo tunazindua huduma za bima zinazofuata misingi ya shariah maarufu kama Takaful. Hii inapelekea kwa mara nyingine CRDB kuwa Benki ya kwanza nchini kuleta huduma hizi kwa wateja wake nchi nzima,” amesema Raballa.
Akieleza tofauti ya Takaful na bima za kawaida, Raballa amesema Takaful haina malipo ya riba, imeundwa katika misingi ya kusaidiana (taawun) pale baadhi ya wahusika wanapokumbwa na majanga na inahusisha uwekezaji wa sehemu ya michango ya wateja na faida inayopatikana hugawanywa kwa wateja kwa kuzingatia taratibu zilivyoainishwa na kampuni husika ya Takaful.

“Kupitia ushirikiano huu tunakwenda kutoa huduma za bima za jumla (general insurance) ikiwamo bima za magari, bima ya nyumba, moto, biashara, bima ya usafirishaji, na bima ya mitambo. Nichukue fursa hii kuwakaribisha Watanzania wote kuchangamkia fursa hii ya bima inayofuata misingi ya shariah (Takaful) inayoenda kutolewa rasmi kupitia Benki yetu pendwa ya CRDB. Takaful ni kwa ajili ya mtu yoyoye anayetamani kupata bima inayofuata misingi ya Shariah na inapatikana katika matawi yetu yote yaliyosambaa nchi nzima,” amesema Raballa. 
Afisa Mtendaji Mkuu wa ZIC Takaful, Said Abdallah Basleym amesema ni furaha kwao kushirikiana na Benki ya CRDB, taasisi kubwa nchini kusambaza huduma za Takaful kwa Watanzania.

“Mshikamano huu naamini utasaidia kuzifikisha kwa wananchi wengi zaidi huduma za Takaful. Tutaendelea kushirikiana na wadau wengine wenye nia ya dhati ya kueneza huduma hizi kwa manufaa ya kila Mtanzania. Bima ndio namna pekee ya kulinda mali, biashara au afya ya mtu hivyo kila mmoja wetu anastahili kuwa nayo bila kikwazo cha aina yoyote,” amesema Basleym.

Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Al Barakah, Abdul Mohamed (kushoto) akizungumza wakati wa hafla yaa uzinduzi wa huduma za bima zinazozingatia misingi ya shariah zijulikanazo kama Takaful kwa ajili ya wateja wanaofuata imani ya Kiislamu na wananchi wengine wanaozingatia misingi ya dini hiyo, iliyofanyika kwenye makao makuu ya Benki hiyo, jijini Dar es salaam leo.
Mkuu wa Kitengo cha CRDB Al Barakah, Rashid Rashid akizungumza wakati wa hafla yaa uzinduzi wa huduma za bima zinazozingatia misingi ya shariah zijulikanazo kama Takaful kwa ajili ya wateja wanaofuata imani ya Kiislamu na wananchi wengine wanaozingatia misingi ya dini hiyo, iliyofanyika kwenye makao makuu ya Benki hiyo, jijini Dar es salaam leo.





SERIKALI KUJENGA CHUO CHA UFUNDI,VETA LIGANGA- SONGEA VIJIJINI

February 29, 2024

Na Mwandishi wetu - Ruvuma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Peramiho amesema Serikali imefanya Maboresho makubwa katika sekta ya elimu katika kipindi cha miaka mitatu.

Kauli hiyo ameitoa Wakati alipoongozana na Wenyeviti wa Mashina wa CCM katika kata ya Parangu, Mpandangido, Kilagano na Maposeni kujionea utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwenye ujenzi wa Miundo Mbinu ya Mambweni na Madarasa uliyofanyika katika shule ya sekondari Maposeni na Mtopesi katika Halmashauri ya Songea Mkoani Ruvuma.

Waziri Mhagama amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongoza Rais Samia imetoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu ya elimu, ili kupunguzia wananchi adhaa ya kuchangishana michango kwa ajili ya ujenzi.

Katika shule ya Sekondari Maposeni kuna ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya 40, ambapo kuna madarasa ambayo ujenzi umekamilika na mengine yako mbioni kujengwa.

"Hivyo basi jamii inawajibu wa kumlinda mtoto wa kike na kumlinda mtoto wa kiume kwa kuwapatia elimu bora itakayosaidia kujenga Jamii yenye weledi," alisema.

Ameongeza kusema zawadi nyingine aliyotupatia Rais ni kuhakikisha anafuta ada na kusaidia watoto wengi kwenda shule.

"Kutokana na ongezeko la wanafunzi, tunahitaji kuongeza miundo mbinu ya elimu kwa ajili ya vijana wetu, Serikali inaandaa mitaala mpya ambayo itasaidia kuwapa elimu ya ufundi vijana wetu waweze kupata ujuzi " alibainisha

Sambamba na hilo Halmashauri ya Songea Vijijini, serikali itajenga chuo kikubwa cha Ufundi cha VETA katika Kata ya Liganga ili kuwezesha vijan kupata elimu ya ujuzi katika chuo hicho.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Songea Vijijini Menace Komba amesema tayari wameshaanza utaratibu wa kuomba wizara ya elimu ili kupata kibali cha kubomoa majengo ya zamani ya shule ya sekondari Maposeni na Mpitimbi ili kujenga Madarasa mapya.

"Uamuzi huo umeafikiwa na Halmashauri ya Songea Vijijini ili kuipatia shule ya sekondari Maposeni pamoja na Mpitimbi muonekano mzuri na wakuvutia,"alisema.

Awali Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari Mwalimu Dismass Nchimbi akizungumza mbele ya ujumbe wa wenyeviti wa Mashina alisema serikali imefanya mambo mengi katika shule ya sekondari Maposeni.

"Tumepata mradi wa ujenzi wa Mambweni 2, na Madarasa 4 na vyoo matundu 10 mradi unaofadhiliwa na Barick katika Jimbo la Peramiho, " alisema.

Serikali kwa kupitia Mbunge wa Peramiho amesaidia pia ujenzi wa jengo jipya la utawala ambalo limegharimu kiasi cha shilingi million 74 na ujenzi wake umefikia kwenye lenta.

Akitoa neno la shukrani Mwanafunzi, Ahad Antony Bugari umeshukuru serikali kwa kuimarisha Miundo Mbinu ya elimu katika shule ya sekondari Maposeni.

Amemshukuru walimu wa Maposeni kwa kusimamia vizuri ujenzi wa Miundo Mbinu ya elimu katika sekondari ya Maposeni.



Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Peramiho akizungumza na Mabalozi wa kata ya Mpandangido, Peramiho, Parangu, Maposeni na Kilagano katika Halmashauri ya Songea Vijijini Mkoani Ruvuma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Peramiho, akiongozana na Wenyeviti wa Mashina wakikagua Mradi wa ujenzi wa Bweni katika shule ya sekondari Maposeni katika Halmashauri ya Songea Vijijini Mkoani Ruvuma.



Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Peramiho akiwa katika Picha ya Pamoja na wenyeviti wa Mashina Katika shule ya sekondari Mtopesi Halmashauri ya Songea Vijini Mkoani Ruvuma.

BENKI YA CRDB YAZINDUA HUDUMA YA BIMA YENYE MISINGI YA SHARIA KWA WATANZANIA WOTE

February 29, 2024


Dar es Salaam. Tarehe 28 Februari 2024: Ikiwa na uzoefu wa takriban miaka minne sasa Benki ya CRDB imezindua huduma za bima zinazozingatia misingi ya shariah zijulikanazo kama Takaful kwa ajili ya wateja wanaofuata imani ya Kiislamu na wananchi wengine wanaozingatia misingi ya dini hiyo.

Akizindua huduma hizo, Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania, Dkt. Abubakar Zubeir ameipongeza Benki ya CRDB kwa kuonyesha njia katika huduma zake kwa kutambua kwamba wapo baadhi ya wateja ambao hushindwa kupata huduma kutokana na imani zao za kidini.
“Hongereni sana kwa ubunifu huu. Shariah ni sehemu muhimu kwa waumini wa Kiislamu ingawa wapo watu wa imani nyingine wanaozipenda na kuzitekeleza kanuni na misingi ya shariah. Kwa bima hizi za Takaful, naamini mtakuwa mmekata kiu ya wengi nami nawaomba Waislamu wenzangu na watu wote wanaoifuata misingi ya shariah kulinda mali na maisha yao kwa bima za Takaful,” amesema Sheikh Zubeir.


Kwa upande wake, Kamshna wa Bima na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Dkt. Baghayo Saqware amesema ubunifu unaotatua changamoto zinazowakwamisha Watanzania kutumia huduma za bima unahitajika ili kuikuza sekta hiyo na kuwawezesha wananchi wengi kuwa na uhakika wa mipango na miradi wanayoitekeleza.
“Takaful ni huduma inayowakaribisha watu wenye imani ya Kiislamu ambao hawaridhishwi na huduma za bima ya kawaida ambazo zina riba. Takaful sio tu ni huduma za bima bali uwekezaji unaomnufaisha mteja pamoja na kampuni inayotoa huduma hizo. Kwa kutumia mtandao wenu mpana wa matawi, naamini Benki ya CRDB mtazifikisha huduma hizi kila kona ya nchi,” amesema Dkt. Saqware.


Mwaka 2021 Benki ya CRDB ilianzisha kitengo maalum cha huduma zinazofuata misingi ya Shariah yaani CRDB Al Barakah Banking hali iliyoifanya kuwa benki ya kwanza nchini kufikisha huduma zinazozingatia shariah nchi nzima. Katika kipindi hicho chote mpaka sasa, CRDB Al Barakah inao wateja zaidi ya 135,000 na kufanya uwezeshaji wa zaidi ya Shilingi bilioni 125, sehemu kubwa ikielekezwa kwa wajasiriamali wadogo na wa kati.
Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Boma Raballa amesema siku zote benki inaendelea kuboresha huduma na bidhaa zake na mwaka jana ilianzisha huduma maalum ya uwezeshaji wa safari za Ibada ya Hijja na Umrah.


“Katika mwendelezo wa kuboresha huduma zetu, Benki ya CRDB kwa kushirikiana na wenzetu, Zanzibar Insurance Corporation (ZIC) Takaful, leo tunazindua huduma za bima zinazofuata misingi ya shariah maarufu kama Takaful. Hii inapelekea kwa mara nyingine CRDB kuwa Benki ya kwanza nchini kuleta huduma hizi kwa wateja wake nchi nzima,” amesema Raballa.
Akieleza tofauti ya Takaful na bima za kawaida, Raballa amesema Takaful haina malipo ya riba, imeundwa katika misingi ya kusaidiana (taawun) pale baadhi ya wahusika wanapokumbwa na majanga na inahusisha uwekezaji wa sehemu ya michango ya wateja na faida inayopatikana hugawanywa kwa wateja kwa kuzingatia taratibu zilivyoainishwa na kampuni husika ya Takaful.


“Kupitia ushirikiano huu tunakwenda kutoa huduma za bima za jumla (general insurance) ikiwamo bima za magari, bima ya nyumba, moto, biashara, bima ya usafirishaji, na bima ya mitambo. Nichukue fursa hii kuwakaribisha Watanzania wote kuchangamkia fursa hii ya bima inayofuata misingi ya shariah (Takaful) inayoenda kutolewa rasmi kupitia Benki yetu pendwa ya CRDB. Takaful ni kwa ajili ya mtu yoyoye anayetamani kupata bima inayofuata misingi ya Shariah na inapatikana katika matawi yetu yote yaliyosambaa nchi nzima,” amesema Raballa.
Afisa Mtendaji Mkuu wa ZIC Takaful, Said Abdallah Basleym amesema ni furaha kwao kushirikiana na Benki ya CRDB, taasisi kubwa nchini kusambaza huduma za Takaful kwa Watanzania.


“Mshikamano huu naamini utasaidia kuzifikisha kwa wananchi wengi zaidi huduma za Takaful. Tutaendelea kushirikiana na wadau wengine wenye nia ya dhati ya kueneza huduma hizi kwa manufaa ya kila Mtanzania. Bima ndio namna pekee ya kulinda mali, biashara au afya ya mtu hivyo kila mmoja wetu anastahili kuwa nayo bila kikwazo cha aina yoyote,” amesema Basleym.


Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Al Barakah, Abdul Mohamed (kushoto) akizungumza wakati wa hafla yaa uzinduzi wa huduma za bima zinazozingatia misingi ya shariah zijulikanazo kama Takaful kwa ajili ya wateja wanaofuata imani ya Kiislamu na wananchi wengine wanaozingatia misingi ya dini hiyo, iliyofanyika kwenye makao makuu ya Benki hiyo, jijini Dar es salaam leo.
Mkuu wa Kitengo cha CRDB Al Barakah, Rashid Rashid akizungumza wakati wa hafla yaa uzinduzi wa huduma za bima zinazozingatia misingi ya shariah zijulikanazo kama Takaful kwa ajili ya wateja wanaofuata imani ya Kiislamu na wananchi wengine wanaozingatia misingi ya dini hiyo, iliyofanyika kwenye makao makuu ya Benki hiyo, jijini Dar es salaam leo.









NHIF YABORESHA KITITA CHA MAFAO,YAONGEZA HUDUMA 247

February 29, 2024



Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF Bernard Konga akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Maboresho ya Kitita cha Mafao jijini Dar es Salaam.


Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF Bernard Konga akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Maboresho ya Kitita cha Mafao jijini Dar es Salaam.



*Kitita cha Mafao chenye maboresho kuanza Machi Mosi


Na Chalila Kibuda,Michuzi TV
MFUKO wa Taifa wa bima ya Afya NHIF umesema imefanya maboresho ya kitita cha mafao kwa wanachama wake pamoja kuangalia madai yaliyokuwapo kwa madaktari ikiwa ni kutaka wanachama wanapata huduma bora na Mfuko kuwa na uendelevu.


Katika maboresho hayo wanachama watapata huduma za kibingwa bobezi kuanzia ngazi ya Hospitali za kanda.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Bw. Bernard Konga amesema kitita cha mafao ni orodha ya huduma za matibabu ambazo zimetolewa kwa wanufaika na bei zake nchini huku kitita hicho kikabaki vilevile bila kuongeza fedha nyingine .


Amesema maboresho ya mwisho ya kitita cha mafao hayo kimezingatia maoni ya wadau na kuweka milango kuendelea kuboresha lengo ni wanachama wasipate usumbufu.


Hata hivyo amesema kuwa katika maboresho wameongeza ulinzi wa mfuko katika kudhibiti mianya ya udanganyifu juu ya kupata huduma wasio wanachama.


“Ni miaka Nane sasa tangu maboresho ya hiki kitita cha mafao kinachotumika kufanyika hivyo ni muhimu wa kufanya marejeo kutokana na mahitaji ya sasa.


"Umuhimu wa kufanya marejeo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuboresha upatikanaji wa huduma bora kwa wanachama na kuongeza huduma ambazo hazikuwepo kwenye kitita cha mafao”,amesema Konga.


Amesema wanachama wanaotumia dawa za shinikizo la damu na sukari sasa wanaweza kupata huduma kuanzia ngazi ya chini huku wanachama wanaopata huduma ya uchujaji damu gharama zikiwa zimepunguzwa.


“Huduma za kibigwa na bingwa bobezi kama matibabu ya Moyo,Saratani na Figo sasa zinaweza kutolewa kuanzia ngazi ya kanda na sio lazima mwanachama kwenda ngazi ya Taifa”,Amesema.


Aidha ameongeza kuwa changamoto ya ukosefu wa dawa sasa imeisha kwani dawa mpya zaidi ya 247 zimeongezwa kwenye kitita kwenye maboresho yaliyofanyika.


Konga amesema maeneo yaliyofanyiwa maboresho ili kuleta unafuu ni gharama za usajili na ushauri wa daktari huduma za dawa na tiba za upasuaji na vipimo huku akisisitiza kuwa gharama za maboresho hayo hazimgusi mwanachama bali kati ya NHIF na mtoa huduma.


Amesema maboresho ya kitita hicho yanatarajia kuanza rasmi Marchi Mosi,2024 huku mfuko huo unaendelea kupokea maoni kutoka kwa wadau kuhusu maboresho zaidi ya kitita hicho.

MAAFISA HABARI WAPIGWA MSASA KUHUSU AKILI HISIA

February 29, 2024


Maofisa Habari na mawasiliano nchini wametakiwa kuelewa dhana nzima ya akili hisia na namna ya kukabiliana na changamoto wanazokutana nazo sehemu za kazi na katika familia.

Hayo yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel wakati akiwasilisha mada kwenye mkutano wa mwaka wa Chama cha Maofisa Mawasiliano Serikalini unaofanyika kwenye ukumbi wa AICC jijini Arusha.

Prof. Gabriel amesema kwamba dhana ya akili hisia hivi sasa imeanza kupata kasi kwenye ngazi ya Serikali hivyo inasaifia ni namna gani unaweza kufanya kazi pamoja na kuwajibika sehemu ya kazi.

“Watu wa Mawasiliano mna umuhimu mkubwa sana katika dhana hii kwani inawasaidia muwasiliane vipi na watu”.

Aidha, alisema ni vyema kuweka mazingira mazuri sehemu ya kazi na kwenye maisha yao ya kawaida kwa familia kwani muda zaidi ya 90% ya maisha yao wanayatumia kazini

“Ni lazima mjitahidi kukabiliana na changamoto katika majukumu yenu na hata katika familia zetu ,pia epukeni kuwa chanzo cha msongo wa mawazo kwa watumishi wengine ili isiwaletee tatizo katika afya zenu”.

Hata hivyo amewataka maofisa hao kuwasaidia viongozi na jamii inayowazunguka kuzuia akili hadi ili isiwaletee madhara katika utendaji wao wa kazi wa kıla siku




RC MTAKA AISHUKURU TAASISI YA JAKAYA MRISHO KIKWETE KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA UTAPIAMLO NA UDUMAVU KWA WATOTO MKOANI NJOMBE

February 28, 2024

Na Issa Michuzi

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka, ameishukuru Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) kwa kukubali kushiriki katika kukabiliana na changamoto za utapiamlo na udumavu wa watoto mkoani humo.

Mkuu huyo wa Mkoa alitoa kauli hiyo baada ya mkutano wake na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya JMKF, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika Makao Makuu ya Taasisi hiyo jijini Dar es salaam uliofanyika Jumanne jioni.

Katika mkutano huo, Mkuu wa Mkoa Mtaka ambaye aliambatana na Katibu Tawala wake Bi. Judica Omary na Mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt. Juma Mfanga, alisema msaada wa JMKF utasaidia pakubwa katika kupambana na changamoto hiyo.

“Hivi sasa tuko katika kampeni ya kuelimisha umma kuhusu tatizo hilo na kutoa majibu ya nini kifanyike kuepukana na janga hilo….

"Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari ametuelekeza tufanye juu chini kutafuta suluhu ya kudumu ya changamoto hii na ahadi ya Taasisi ya JMKF kusaidia jitihada za serikali kupambana na tatizo hilo ni jambo la kushukuriwa sana.

“Kwa kuchangisha rasilimali, utaalamu, na kujenga ushirikiano wa kimkakati, kuna matumaini ya kupatikana maendeleo makubwa yanayoweza kuboresha hali ya lishe na ustawi wa watoto wa mkoa wetu", alisema Mkuu huyo wa Mkoa.

Wengine walioshiriki katika mkutano huo ni pamoja na Patrick Codija, Mkuu wa Lishe pamoja na Bi. Ophilia Karumuna, Afisa, wote kutoka Shirika la Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF).

Wengine ni Vanessa Anyotti, Afisa Mtendaji Mkuu na Dkt. Catherine Sanga kutoka Taasisi ya JMKF, Germana Leyna wa Kituo cha Chakula na Lishe Tanzania, na Dkt. Nyambura Moremi, Kiongozi wa Idara ya Utafiti wa Maabara ya Afya ya Umma ya George Mwita, Mkurugenzi Mkazi wa Taasisi ya Lishe ya Kimataifa (Nutrition International), pia alishiriki pamoja na Bernard Makene kutoka Taasisi hiyo yenye makao yake makuu nchini Canada.

Awali, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Mfanga alimweleza Dkt. Kikwete kwamba licha ya uwezo mkubwa sana wa kuzalisha mazao ya chakula, bado zaidi ya asilimia 50 ya watoto wa Mkoa wa Njombe wanakabiliwa na tatizo la utapiamlo, na hivyo kuwasababishia udumavu, unyafuzi na ukondefu.

Katika maelezo yake, RMO aliongeza kuwa chanzo kikuu cha tatizo hilo ni kwamba wazazi wengi hawana muda wala maarifa ya kuandaa lishe bora kwa ajili ya watoto wao.

"Hali hii inapelekea wazazi kutegemea zaidi unga wa mahindi kuandaa chakula cha kila siku licha ya kuwepo kwa matunda na mboga za lishe mbalimbali."

“Kwa hiyo, unakuta watoto wanakoseshwa virutubisho muhimu hali inayosababisha udumavu, kinga dhaifu, na kuongezeka kwa hatari ya kupata maambukizi ya magonjwa mbalimbali", alifafamua Dkt. Mfanga.

Aidha, alibainisha changamoto hiyo hujidhihirisha katika kiwango cha juu cha udumavu kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano, ambapo takribani nusu yao wameathirika.

"Hali hii haidumazi tu ukuaji wa kimwili wa mtoto bali pia inaathiri ukuaji wa kiakili, kinga, na ustawi wa jumla," alisema Dkt. Mfanga.

Kwa upande wake Rais Mstaafu Dkt. Kikwete alieleza kuwa ameguswa na takwimu za hivi karibuni zinazoonesha ukubwa wa tatizo hilo, hususan katika Mkoa wa Njombe.

Aidha, alieleza pia kufurahishwa na juhudi za makusudi zinazofanywa na uongozi wa Mkoa wa Njombe katika kukabiliana na changamoto hiyo.

Alitumia pia fursa hiyo kueleza kuwa miongoni mwa malengo ya Taaisi yake ya Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) ni kulinda na kukuza afya ya uzazi na Watoto.

Hiivyo, alibainisha, mkutano huo umetoa fursa nzuri kwa upande wa Taasisi yake kupata taarifa muhimu zitakazosaidia kupanga mikakati ya kuweza kushirikiana na Serikali na wadau wengine katika kukabiliana na tatizo hilo la utapiamlo nchini.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF), Rais Mstaafu wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka kabla ya kuanza kwa mkutano wao katika makao makuu ya JMKF Masaki jijini Dar Jumanne jioni. Kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Bi Judica Omary.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF), Rais Mstaafu wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, katika mkutano na  Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka na ujumbe wake katika makao makuu ya JMKF Masaki jijini Dar Jumanne jioni. Kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Bi Judica Omary.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF), Rais Mstaafu wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akipokea Ripoti ya hali ya Lishe Pamoja na Kalenda toka kwa  Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka baada ya mkutano wao katika makao makuu ya JMKF Masaki jijini Dar Jumanne jioni. Kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Bi Judica Omary.



Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF), Rais Mstaafu wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akipokea Ripoti ya hali ya Lishe Pamoja na Kalenda toka kwa  Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka baada ya mkutano wao katika makao makuu ya JMKF Masaki jijini Dar Jumanne jioni. Kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Bi Judica Omary.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka akimkabidhi Ripoti ya Lishe Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF) , Bi. Vanessa Anyoti, baada ya mkutano  katika makao makuu ya JMKF Masaki jijini Dar Jumanne jioni.

Picha na JMKF

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF), Rais Mstaafu wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, katika

Picha ya Pamoja na na  Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka na ujumbe wake katika makao makuu ya JMKF Masaki jijini Dar Jumanne jioni.

WADAU SEKTA YA AFYA WAKABIDHI VITENDEA KAZI VYA THAMANI YA MILIONI 800 KWA SERIKALI

February 28, 2024

` 
Serikali kupitia Wizara ya Afya imepokea vitendea kazi vyenye thamani ya Milioni 800 kutoka kwa wadau wa CDC kupitia THPS kwa ajili ya mapambano dhidi ya UKIMWI na Kifua Kikuu katika Mkoa wa Tanga.


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amepokea vitendea kazi hivyo leo Februari 23, 2024 Mkoani Tanga ambavyo ni pikipiki 50, friji 72, Centrifuges 56, Compyuta 50, UPS 50 na printa 50 ambavyo vitendea kazi hivyo vitaimarisha huduma za Afya katika Mkoa huo.


Aidha, wakati akipokea vitendea kazi hivyo Waziri Ummy amewataka wote watakaokabidhiwa vifaa hivyo kuvitumia Kama ilivyo elekezwa ikiwa ni pamoja na kuwafikia wateja wanaoishi katika mazingira magumu na mbali na vituo vya kutolea huduma za Afya ili kuwafikishia huduma.


“Lakini pia tunaamini kwamba mtaongeza idadi ya huduma mkoba ‘outreach services’, kuwafikia wateja walio katika mazingira hatarishi ya kuambukizwa ugonjwa wa UKIMWI na kuwapatia huduma za kinga zikiwemo kinga dawa na kusafirisha sampuli kwa ajili ya kupima wingi wa Virusi vya UKIMWI.” Amesema Waziri Ummy


Pia, amewataka kutunza vifaa hivyo na kunifanyia matengenezo ya mara kwa mara ili viweze kudumu kwa muda mrefu na kutimiza lengo la kudhiiti UKIMWI na VVU ambapo ametoa onyo kwa yeyote atakae fanya kinyume na maelekezo hayo kuchukuliwa hatua za kinidhamu.


Pia, Waziri Ummy ameyataka mashirika yote ya kiraiya yanayofanya kazi katika Sekta ya Afya kuzingatia ya ( katika fedha zote wanazozipata angalau watenge kiasi kisichopungua asilimia 10 kwa ajili ya ya kuajiri watumishi wa Afya katika vituo vya kutoa huduma za Afya ngazi ya msingi


“Tunaposema kupambana na masualaya ya UKIMWI lakini kuna upungufu wa wauguzi, hakuna madaktari, hakuna watu wa maabara, hakuna wafamasia, angalau ajiri wauguzi wawili na watumishi wengine wa mikataba.” Amesema Waziri Ummy