WAJUMBE WA BODI YA JKCI WAKUTANA JIJINI DAR ES SALAAM

December 06, 2023




Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina ambaye pia ni Mratibu wa huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto Mkoa wa Rukwa akiongoza kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu wa Bodi hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge.

Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge akiwaonesha mfano wa jengo litakalojengwa katika Hospitali ya JKCI Dar Group wajumbe wa bodi hiyo wakati wa kikao cha tano cha Bodi kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof. Appolinary Kamuhabwa akichangia mada wakati wa kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kulia ni mjumbe wa Bodi hiyo CPA.Godfrey Kilenga ambaye pia ni Mtendaji Mkuu kutoka ofisi ya TAB Consult Audit Firm Partner.

Baadhi ya Viongozi wa Menejimenti ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge wakati akitoa taarifa ya utendaji wa kazi zilizofanywa na taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Oktoba katika mwaka wa fedha wa 2023/24 wakati wa kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
- Advertisement -


Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Harun Matagane kutoka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali akichangia mada wakati wa kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge akitoa taarifa ya utendaji wa kazi zilizofanywa na taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Oktoba katika mwaka wa fedha wa 2023/24 wakati wa kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »