Na Pamela Mollel,Arusha
Taasisi za Fedha zimeombwa kurahisisha huduma za kifedha Kwa watu wenye ulemavu hususan wa macho.
Hayo yamesemwa kwenye Mkutano wa wiki ya azaki unaoendelea jijinibl Arusha ambapo wameomba kupatiwa mfumo shirikishi utakaowasaidia kwenye utumiaji wa Teknolojia katika eneo la kifedha.
Mmoja wa walemavu wa macho Renatusi Rupoli kutoka Iringa amesema watu wasioona huwa wanatumia mitandao kwa njia ya sauti ambapo alihoji kwanini kusiwepo na Software kama hizo ambazo zinajumlishwa kwenye Mashine za Kutolea pesa (ATM) Benki Ili kupunguza usumbufu wakutafuta wasaidizi wakati wa kutumia huduma hizo.
Akizungumza katika Mkutano huo Amali Baziadi kutoka Benki ya Stanbic amesema changamoto hiyo ameichukua na kwamba wataona namna gani yakulifanyia kazi ili kupata ufumbuzi.
"Ninaimani kuwa siyo tu Stanbic pekee ambao hatuna huduma hii lakini naichukua kama changamoto na tuone namna gani tunaifanyia kazi ili kuwawezesha wateja wetu kupata huduma rafiki kwao"amesema Baziadi.
Aidha wadau hao wameshauri kuwepo kwa huduma rafiki Kwa wazee na wananchi waishio Vijijini namna ambavyo wanaweza kufungua akaunti za Benki kwa kutumia mitandao badala ya kufuata huduma hizo kwa mawakala wa Benki ambao mara nyingi hupatikana mijini.
Mwishooo.