ADC YAJIWEKA MGUU SAWA UCHAGUZI WA 2024/2025

December 29, 2023

Na Oscar Assenga,TANGA

CHAMA cha Alliance For Democratic Change (ADC-Dira ya Mabadiliko ) kimeanza kujiweka sawa kuelekea kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani na ule Mkuu mwaka 2025 baada ya kutangaza kufanyika kwa uchaguzi wa ndani wa chama hicho kwa mwaka 2024.

Akizungumza leo Katibu Mkuu wa ADC Taifa Doyo Hassan Doyo (Pichani kulia) alisema kwa mujibu wa katiba ya chama hicho toleo la tatu la mwaka 2019,Uchaguzi wa viongozi ndani ya chama hufanyika kila baada ya miakaa mitano.

Alisema kwamba tamko hilo linaonyeshwa katika katiba yao kwenye sura ya nane ibara ya 53(i) “Ukomo wa uongozi ni miaka mitano” na sasa ni wakati wa kufanyika chaguzi ambazo zitawapa fursa ya kupatikana viongozi wapya katika ngazi mbalimbali.

Katibu huyo alisema kutokana na chama kufanya uchaguzi ndani ya chama mnamo mwaka 2019 ambapo ulifanyika Mkutano mkuu mwezi Aprili katika ukumbi wa Hotel ya Madinat Bahri iliyopo Zanzibar.

Aidha alisema kwamba mwaka 2024 viongozi waliopo madarakani wanatimiza miaka mitano tangu kufanyika uchaguzi na mkutano mkuu husika kwa madhumuni ya kuchagua viongozi ambao wako madarakani hadi muda huu.

“Kwa kuzingatia utekelezaji wa miongozo kutoka katika katiba yetu Ofisi ya chama makao makuu inatoa ratiba ya uchaguzi wa ndani ya chama hicho kwa mwaka 2024”Alisema Katibu huyo.

Katibu huyo alisema kwamba uchaguzi huo ngazi ya Tawi utaanza Januari Mosi hadi Januari 31 mwakani wakati ule wa kata utafanyika kati ya Februari Mosi hadi February 29 mwaka 2024 utakaokwenda sambamba na ule wa majimbo.

Alisema baada ya hapo kutafanyika chaguzi ngazi ya wilaya utaanza Machi 1 mpaka Machi 31 mwakani utakaoambatana na ule ngazi ya Kanda huku akiwataka wanachama kuchangamkoa fursa za kuwania nafasi mbalimbali.

Katibu huyo alisema baada ya hapo kutafanyika uchaguzi Mkuu wa chama chicho ambao unatarajiwa kwisha mwezi Mei mwakani na hatimaye kuweza kupata safu mpya za uongozi.

Hata hivyo Katibu huyo alitoa agizo kwa viongozi wote wa chama hicho nchi nzima kusimamia zoezi hilo kwa ufanisi na kushirikisha wanachama wote wa ADC ili kukamilisha chaguzi hizo kwa mafanikio.




WATALI 54 KUTOKA CHINA WASHIRIKI TAMASHA LA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO

December 28, 2023

 Pamela Mollel ,Arusha


Watalii zaidi 54 kutoka nchini China wamewasili Mkoani Arusha kwaajili ya kushiriki Tamasha la kupanda Mlima Kilimanjaro

Akizungumza katika hafla ya kuwapokea watalii hao,Mkuu wa Mkoa wa Arusha John V.K Mongella alisema ujio huo umetokana na mahusiano mazuri kati ya Tanzania na China

Alisema kuwa msimu wa mwisho wa mwaka ni msimu mzuri zaidi kwa kupanda mlima Kilimanjaro hali itakayowafanya wafurahi zaidi lakini pia kutangaza Tanzania kupitia mlima huo

Pia Mh.Mongella aliwatunuku vyeti vya pongezi kwa uamuzi mzuri wa kuja kupanda mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu zaidi Duniani

"Nawapongeza sanaaa kwa ujio wenu naamini mtafurahia sanaaa tamasha la kupanda mlima Kilimanjaro lakini pia niwapongeze kampuni ya kitalii ya Gosheni Safari kwa kuandaa tamasha hili"alisema Mongella

Ikumbukwe kuwa ujio wa watalii hao ni matokeo ya Filamu ya Royal Tour iliyoongozwa na Rais MaMa Samia Suluhu Hassan




 

 

BARAZA LA UUGUZI NA UKUNGA TANZANIA KUENDESHA MTIHANI KWA WATAHINIWA 4165

December 28, 2023

 Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania linatarajia kuendesha zoezi la Mtihani kwa watahiniwa 4165, ambao wamekidhi vigezo vya kufanya Mtihani huu, wakiwemo waombaji 3917 ambao wanafanya mtihani kwa mara ya kwanza na 248 wanaorudia. Kati yao, Wanaume ni 1647 na wanawake ni 2518.


Hayo yamesemwa na Kaimu Msajili Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, Bi. Happy Masenga, leo Disemba 28, 2023, wakati akizungumza na vyombo vya habari katika ukumbi wa ofisi za Baraza hilo Jijini Dodoma.

Aidha, Mtihani huu utafanyika katika vituo vilivyotambuliwa na kukubaliwa na Baraza katika Mikoa ya Mwanza, Dar es Salaam, Dodoma, Kilimanjaro, Mbeya, Iringa, na Tabora siku ya Ijumaa 29/12/2023, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 7:00 mchana.

Lengo la Mtihani huu ni kupima umahiri wa watahiniwa ili kupata wataalamu wa Afya wenye sifa za kusajiliwa na kupewa leseni ya kutoa huduma kama Muuguzi au Mkunga kwa mujibu wa kifungu cha 15 (1) (a-b) cha Sheria ya Uuguzi na Ukunga.

Mtihani wa usajili na leseni umekuwa ukifanyika tangu kuanzishwa kwa Baraza mwaka 1953 kwa mujibu wa kifungu 6 (a) cha Sheria, ambapo hapo awali mtihani huu uliendeshwa kwa ushirikiano kati ya Baraza na Wizara ya Afya.

Baraza la Uuguzi na Ukunga Nchini lina jumla ya wauguzi na wakunga wenye leseni wapatao 49,994, ambao wanatoa huduma kwenye Hospitali za Rufaa, Mikoa, Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati. 

Idadi hii inajumuisha wauguzi na wakunga walioajiliwa Serikalini pamoja na sekta binafsi kwa ngazi ya Astashahada, Stashahada, Shahada, Uzamili na Uzamivu.




RAIS DKT. MWINYI AZUNGUMZA NA BALOZI WA TA NZANIA NCHI UGANDA

December 28, 2023
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Balozi wa Tanzania Nchini Uganda Mhe.Meja Jenerali Paul Kisesa Simuli, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo na kujitambulisha, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar leo 28-12-20213..(Picha na Ikulu)  
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Balozi wa Tanzania Nchini Uganda Mhe.Meja Jenerali Paul Kisesa Simuli, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo na kujitambulia akielekea Kituo chake cha kazi, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar leo 28-12-2023.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Balozi wa Tanzania Nchini Uganda Mhe.Meja Jenerali Paul Kisesa Simuli, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar leo 28-12-2023  kwa mazungumzo na kujitambulia akielekea Kituo chake cha kazi,  na (kushoto kwa Rais) Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said,mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.(Picha na Ikulu) 

PUMA ENERGY TANZANIA YATOA VIFAA VYA UJENZI KUSAIDIA WAATHIRIKA MAFURIKO YA MATOPE KATESHI

December 28, 2023


Na Mwandishi Wetu, Hanang



KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Energy Tanzania imekabidhi msaada wa vifaa vya ujenzi zikiwemo nondo 1000, mabati 800 na saruji mifuko 600 kwa ajili ya kusaidia waathirika wa mafuriko ya matope yaliyotokea Kateshi wilayani Hanang mkoani Manyara.

Vifaa hivyo vya ujenzi vyenye jumla ya thamani ya Sh.milioni 70 vimekabidhiwa leo Desemba 28,2023 wa Serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Hanang mkoani Manyara Janeth Mayanja.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo Mkuu wa Wilaya ya Hanang Janeth Mayanja ameishukuru Kampuni ya Puma Energy Tanzania kwa kutoa vifaa vya ujenzi ambavyo kwa sasa ndivyo vinahitahika zaidi.

“Kwa niaba ya Serikali anachukua nafasi hiyo kuupongeza uongozi wa Puma Energy Tanzania kwa kufika Kateshi kutoa misaada wa vifaa vya ujenzi.Tumepokea mifuko ya saruji 600, bati pisi 800 na nondo 1000.

“Vifaa hivi vya ujenzi vitasaidia eneo la ujenzi kwani tunakusudia kuanza ujenzi hivi karibuni kujenga nyumba za waathirika wale ambao wamepoteza makazi na mchango huu una thamani ya Sh.milioni 75,”amesema Mayanja.

Ameongeza kuwa msaada huo wa nondo, bati na saruji unakwenda kuongeza nguvu katika jitihada za Serikali za Awamu ya Sita chini ya ya Dk.Samia Suluhu Hassan ambayo imeamua kujenga nyumba kwa waathirika baada ya kutokea mafuriko Desemba 3, 2023

Aidha amesema msaada huo umekuja wakati muafaka kwani wamekuwa wakipokeza zaidi msaada wa mahitaji ya chakula na dawa lakini kwa sasa wako kwenye hatua za mwisho kuanza ujenzi wa nyumba za waathirika kwa kutambua baada ya mafuriko kuna baadhi ya makazi yameharibiwa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania, Bi Fatma Mohemed Abdallah, Meneja Uhusiano wa Puma Energy Tanzania Limited Godluck Shirima amesema bodi ya wakurugenzi chini ya Mwenyekiti wake Dk.Selemani Majige, Menejimenti ya Kampuni chini ya uongozi wa Bi Fatma Mohamed Abdallah, wafanyakazi na wadau wote wameguswa na kuhuzunishwa na mafuriko yalio wakuta wananchi wa Katesh.

“Hivyo viongozi wetu wakatuelekeza kuleta msaada huu wa vifaa vya ujenzi ili kuunga mkono juhudi na jitihada za Serikali kuwajengea makazi waathirika waliopoteza makazi yao kwenye mafuriko.

“Puma Energy pia ni muathirika wa mafuriko haya, ambapo kituo chao cha Kateshi kiliharibiwa na mafuriko, kwa hiyo kama waathirika na mkazi wa Kateshi, kampuni iliona ni vyema kutoa mchango wake kwa jamii ya Katesh,”amesema Shirima.


Mkuu wa Wilaya ya Hanang mkoani Manyara Janeth Mayanja (wa pili kulia )akipokea mfuko wa saruji ukiwa ni sehemu ya mifuko 600 ya saruji kutoka kwa Mwakilishi wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania ambaye ni Meneja Uhusiano Godluck Shirima( wa tatu kushoto) Meneja Masoko Lilian Kanora(wa kwanza kulia) na Meneja Rasilimali Watu Bw. Joseph Jaruma ( wa pili kushoto).Wa kwanza kulia ni Ofisa Ugavi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang mkoani Manyara Methew Giramisi .

Mkuu wa Wilaya ya Hanang mkoani Manyara Janeth Mayanja (wa tatu kushoto) akipokea bati kutoka kwa Mwakilishi wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania ambaye ni Meneja Uhusiano Godluck Shirima( wa pili kulia).Wanaoshuhudia Meneja Masoko Lilian Kanora(wa pili kushoto) na Meneja Rasilimali Watu Bw. Joseph Jaruma ( wa kwanza kulia).Wa kwanza kushoto ni Ofisa Ugavi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang mkoani Manyara Methew Giramisi .













RAIS SAMIA ATUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA YA UZAMIVU YA USIMAMIZI WA UTALII NA MASOKO CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR (SUZA).

December 28, 2023

 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Viongozi wengine akiwa kwenye maandamano ya Kitaaluma wakati walipokuwa wakiingia kwenye Ukumbi wa Dkt. Ali Mohamed Shein Kampasi ya Tunguu kwa ajili ya kushiriki Hafla ya Mahafali ya 19 ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) ambapo Chuo hicho kimemtunuku Shahada ya Heshima ya Uzamivu kwa kutambua mchango wake wa kuifungua nchi kiuchumi kupitia Sekta ya Utalii tarehe 28 Desemba, 2023.


 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Dkt. Aman Abeid Karume katika Ukumbi wa Dkt. Ali Mohamed Shein Kampasi ya Tunguu walipohudhuria Hafla ya Mahafali ya 19 ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) tarehe 28 Desemba, 2023.

WAZIRI WA UCHUMI WA BULUU NA UVUVI AZUNGUMZA NA WAANDISHI ZANZIBAR.

WAZIRI WA UCHUMI WA BULUU NA UVUVI AZUNGUMZA NA WAANDISHI ZANZIBAR.

December 28, 2023





Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Suleimana masoud Makame akijibu maswali alioulizwa na Waandishi wa Habari kuhusiana na Mafanikio na Changamoto za Wizara yake kuelekea Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar,Hafla iliofanyika katika Ukumbi wa ZBC TV Mnazi mmoja Zanzibar.



Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Suleimana masoud Makame akisisitiza jambo wakati akijibu maswali alioulizwa na Waandishi wa Habari kuhusiana na Mafanikio na Changamoto za Wizara yake kuelekea Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar,Hafla iliofanyika katika Ukumbi wa ZBC TV Mnazi mmoja Zanzibar.

Mwandishi wa Habari Mwandamizi Salum Vuai akiuliza maswali katika Mkutano na Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Suleimana masoud Makame alipokua akizungumzia kuhusiana na Mafanikio na Changamoto za Wizara yake kuelekea Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar,Hafla iliofanyika katika Ukumbi wa ZBC TV Mnazi mmoja Zanzibar. PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

Na Takdir Ali – Habari Maelezo.

Waziri wa Uchumi wa buluu na Uvuvi Suleiman Massoud Makame amesema miradi ya maendeleo imeongozeka katika wizara hiyo kutoka miradi 10 ya maendeleo mwaka 2020 hadi kufikia 17 mwaka 2023.

Ameyasema hayo wakati alipokuwa akilezea makakati na mafanikio ya Wizara hiyo, ikiwa ni maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Amesema miradi hiyo imejumuisha sekta mbalimbali ikiwemo Uvuvi, Mwani, Ufugaji, Viwanda vya kusarifu madagaa na mwani, masoko na madiko, uhifadhi wa Bahari na utafiti.

Ameeleza kuwa mafanikio hayo ya kimaendeleo yanaifffiisha Serikali katika shabaha za kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi, Dira ya Maendeleo ya Mwaka 2050, na Mpango wa Maendeleo ya Zanzibar (ZADEP).

Aidha amesema Serikali inaendelea kuwawezesha wajasiriamali kwa kuwapatia elimu, ubunifu na zana za kujiongezea ajira katika maeneo yao.

Amefahamisha kuwa Serikali imeweka mkakati wa kuwawezesha wakulima wa mwani na wafugaji wa mazao ya baharini 23,000 ambao zaidi ya asilimia 90 ni wanawake wa vijijini.

Mbali na hayo amesema, Usafirishaji wa mwani nje ya Nchi umeongezeka kutoka Tani 11,382 zenye thamani ya Tzs Bilioni 11.70 mwaka 2020 hadi kufikia Tani 12,563 zenye thamani ya Tzs Bilioni 12.581 kwa mwaka 2023.

Sambamba na hayo amesema maendeleo ya kiuchumi na kijamii ni lazima yazingatie uhifadhi wa maliasili hivyo amewaomba Wananchi kuunga Mkono juhudi za Serikali katika kuleteleza mikakati iliojipangia.

Mbali na hayo amesema Serikali imetilia mkazo utafiti na sayansi ya bahari ili kupata taarifa sahihi zinazoimarisha utekelezaji wa sera za Uchumi wa Buluu.

MZUMBE YAPOKEA RASIMU YA MICHORO YA UJENZI WA MIUNDOMBINU KUPITIA MRADI WA HEET.

MZUMBE YAPOKEA RASIMU YA MICHORO YA UJENZI WA MIUNDOMBINU KUPITIA MRADI WA HEET.

December 28, 2023

 


Uongozi wa chuo kikuu Mzumbe umeitaka kampuni ya Y & P Architect yenye mkataba wa Huduma ya Ushauri elekezi, usanifi na usimamizi wa ujenzi wa miundombinu ya chuo hicho kuongeza kasi katika utekelezaji wa shughuli hiyo kuwezesha kuendelea kwa hatua nyingine ikiwemo kumpata Mkandarasi wa ujenzi mapema mwakani.


Akizungumza wakati wa kikao baina ya menejimenti ya Chuo hicho Kikuu Mzumbe na Kampuni hiyo ya Y & P Architect kupokea na kupitisha rasimu ya michoro ya ujenzi wa miundombinu ya majengo unaotekelezwa na serikali kupitia mradi wa HEET Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. William Mwegoha amesema pamoja na kuzingatia ubora mradi huo unapaswa kukamilika kwa wakati.

“Hii ni kazi muhimu katika chuo chetu kwa sababu itakapo kamilika itatuongezea huduma kwenye chuo chetu ambayo mwisho wa siku ni mkakati wa kuongeza masuala ya Udahiri , mifumo ya TEHAMA, masuala ya kuendeleza bunifu na matumizi ya Mtandao kuwezesha mafunzo ya masafa” . Alisema Prof. William Mwegoha makamu mkuu wa chuo kikuu Mzumbe

Katika kikao hicho kampuni ya Y & P Architect imewasilisha rasimu ya michoro ya majengo matatu ya.Academic Complex, TEHAMA na Uvumbuzi pamoja na jengo la Mgahawa (Cafteria) yanayotarajiwa kujengwa eneo la Maekani Kampasi kuu Morogoro.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Y & P Architect, Yasin Mringo, ameishukuru Menejimenti ya Chuo Kikuu Mzumbe kwa ushirikiano uliosaidia kuwa na ufanisi hadi hatua iliyofikiwa ambapo pamoja na kupokea mapendekezo mbalimbali kwa ajili ya maboresho ameahidi kuongeza kasi kwenye utekelezaji wa shughuli zilizobaki kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilika mapema hata kabla ya muda wa mkataba.

“Tumekwisha kamilisha hatua ya kwanza tunashukuru mungu leo kwa kushirikiana na Uongozi wa chuo kikuu Mzumbe baada ya sikukuu hizi za mwisho wa mwaka kupita nimategemeo yetu kwamba katika kipindi cha miezi miwili na nusu ya kufanya kazi tutakamilisha mategemeo yetu ili kufikia mwezi wa Nne au watano mkandarasi kwa ajili ya ujenzi awe amepatikana”. Alisema Msanifu Majengo Yasin Mringo.

Mkataba wa huduma ya Ushauri Elekezi, Usanifu na usimamizi wa ujenzi wa miundombinu ya chuo hicho uliosainiwa Oktoba 9,2023 baina ya Chuo kikuu Mzumbe na kampuni ya Y & P Architect, sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa HEET kuboresha miundombinu ujenzi wa majengo eneo la chuo kikuu Mzumbe, pia kuanza mchakato wa ujenzi wa Kampasi mpya ya Chuo hicho katika mkoa wa Tanga.

RAIS MWINYI ARIDHIA UWANJA WA AMAAN KUITWA “NEW AMAAN SPORTS COMPLEX”

RAIS MWINYI ARIDHIA UWANJA WA AMAAN KUITWA “NEW AMAAN SPORTS COMPLEX”

December 28, 2023




Na, Brown Jonas – WUSM

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameridhia ushauri wa kuubadili jina uwanja wa Amaan na kuitwa “New Amaan Sports Complex” wakati wa uzinduzi wa awamu ya tatu ya Uwanja huo uliofanyika Desemba 27, 20203 kisiwani humo

Rais Mwinyi ameridhia ushauri huo uliotolewa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro alipokua akitoa salamu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Kutokana na maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kuufanya uwanja huu kuwa wa kisasa na wenye viwango vya Kimataifa, mimi naomba niubadilishe jina uitwe New Amaan Stadium” alisema Dkt. Ndumbaro.
- Advertisement -

Hafla ya Uzinduzi wa Uwanja huo ilipambwa na Burudani mbalimbali ikiwemo Muziki na mechi ya mpira wa miguu ya kirafiki baina ya Timu ya Mpira wa Miguu ya Tanzania Bara “Kilimanjaro Stars” na Timu ya Mpira wa Miguu ya Zanzibar “Zanzibar Heros ambazo zilitoka sare ya bila kufungana.
KARAFUU FURSA MPYA KWA WAKULIMA WA MIKOA YA MOROGORO NA TANGA

KARAFUU FURSA MPYA KWA WAKULIMA WA MIKOA YA MOROGORO NA TANGA

December 27, 2023










Na Mwandishi Wetu

MIKOA ya Morogoro na Tanga imepewa kipaumbele cha kulima zao la karafuu katika mpango wa pamoja wa serikali na wadau wa kilimo kutoka sekta binafasi na taasisi zisizo za kiserikali.

Ongezeko la Mkoa wa Tanga katika ulimaji wa karafuu kitaifa limetangazwa katika Mkutano wa Wadau wa Kilimo na Mazingira waliokutana jijini Dar es Salaam.

Wadau hao wamesema zao la karafuu limeonesha kustawi katika mikoa hiyo miwili, hivyo waamini ikipewa kipaumbele itaongeza uzalishaji.
- Advertisement -


“Morogoro ndiyo iliyotangulia na mwaka jana tu ilizalisha tani 2,000 sawa na nusu ya uzalishaji wa Zanzibar wa jumla ya tani 4,000, hivyo ongezeko la Tanga ni wazi Tanzania itakuwa mzalishaji mkubwa wa karafuu,” walisema wadau.

Ulimaji wa karafuu Tanzania Bara umetokana utafiti na ushauri wa Kituo cha Kuendeleza Kilimo Nyanda za Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), taasisi inayowashirikisha wadau katika sekta binafsi katika kulima mazao na kuendeleza minyororo ya thamani ya mazao hayo.

Akitangaza uamuzi wa kuiongeza Tanga kwenye mpango huo wa zao la karafuu, Ofisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT, Geoffrey Kirenga, amewambia wajumbe wa jukwaa la Wadau wa Kilimo na Mazingira kwamba utafiti umeonyesha kuwa mkoa huo unaweza kulima kwa mafanikio zao la karafuu.

Kirenga ameeleza kuwa zao la karafuu ni zao la thamani kubwa na ni sehemu ya mazao muhimu ya viungo na pia ni muhimu katika mazao ya mboga, matunda, mizizi na maua (hortculture) ambayo yana masoko yanayaotabirika duniani.

Alisema endapo Watanzania watachangamkia fursa zilizomo katika ulimaji wa zao la karafuu, basi uchumi wa mkulima mmoja mmoja na wa Taifa utaimarika na kukifanya kilimo kiwe na tija.

“Mazao ya viungo hususani karafuu yamekuwa na soko imara na la uhakika. Sasa bei elekezi ya kilo moja ya karafuu ni kati ya shilingi 14,000 hadi 18,000. Bei hizi zinaonyesha ni jinsi gani zao hili likipewa kipaumbele litakavyokuwa na maana kwa mkulima mdogo na pia likawa ni zao letu lenye tija kubwa katika soko la kimataifa”, Kirenga alilieleza jukwaa hilo.

Aliongeza kuwa karafuu ni zao la msingi Zanzibar na wao ndiyo wazalishaji wakuu wa zao hilo, wana masoko makubwa na ya uhakika.

“Hivi karibuni Tanzania Bara imeanza kuzalisha zao hili katika baadhi ya mikoa miwili. Uzalishaji umekuwa na mwelekeo mzuri kwani mikoa hii sasa inazalisha kwa wingi zaidi karafuu ikilinganishwa na Zanzibar ambao ndio waanzilishi. Mikoa hiyo kwa sasa ni Morogoro na Tanga”, alisema Kirenga.

Sasa hivi serikali inawashirikisha wadau wengine kuinua pato la Mtanzania kufikia dola za Marekani 3,000 kabla ya mwaka 2025.

Tanzania sasa inahesabiwa kuwa nchi yenye uchumi wa kati wa chini baada ya pato la Mtanzania kuvuka dola za Marekani 1,096, kigezo kinachotumiwa na Benki ya Dunia katika kupima umaskini wa watu katika taifa lao.

Ili kulifanya zao la karafuu likubalike kwa wakulima Mkoa wa Morogoro na SAGCOT wameshirikiana serikali ya mkoa kuwapeleka Zanzibar wakulima 20 wa Morogoro kujifunza ulimaji wa zao hilo.

Tayari ulimaji wa zao hilo umeimarika katika Wilaya za Morogoro Vijijini, Kilombero; katika Halimshauri ya Wilaya ya Mlimba na sasa imeongezeka Wilaya ya Mvomero.

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Judith Nguli, ameeleza uingizaji wa kilimo cha karufuu katika mkakati wa kuinua pato la mkulima una maana kubwa kwa wilaya yao.

Alisema ulimaji wa zao hilo unawaletea wakulima fursa tele na kwani wadau wamejizatiti kuunga mkono ulimaji wa zao katika wilaya yao.

“Wilaya yetu imekuwa ikiathiriwa na kilimo kisichokuwa na tija. Uwepo wa mazao kama haya ya kimkakati utapelekea kuinua maisha ya mwananchi mmoja mmoja. Tumethibitishiwa kuwa ardhi yetu itasitawisha zao la karafuu kama tutazingatia maelekezo ya wataalamu,’’ alisema Nguli.

Meneja wa SAGCOT, Mkoa wa Morogoro, John Banga alieleza kuwa Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa mikoa iliyopewa kipaumbele cha kuzalisha kilimo cha mazao ya viungo, na hasa karafuu, huku akianisha sababu zake ni kwamba mkoa una hali ya hewa inayofaa na afya ya udongo ni himilivu kwa zao la karafuu.

“Ndani ya miezi miwili wakulima wamegawiwa zaidi ya miche 150,000 ili waweze kuendeleza kilimo cha karafuu. Jambo kubwa na zuri wapo wadau ambao wamekuja kuunga mkono juhudi hizi za kulima karafuu katika milima ya Morogoro. Kilimo cha karafuu kwa njia hii kitasaidia katika kutunza afya ya mazingira ya misitu. Tutajiepusha na uchomaji wa maeneo na ukataji wa miti kwa ajili ya mkaa,’’ alisema Banga.

DAWA ZA KULEVYA AINA YA HEROIN NA METHAMPHETAMIN KILOGRAMU 3,182 ZAKAMATWA JIJINI DAR ES SALAAM NA IRINGA.

December 27, 2023

 Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ya Tanzania (DCEA) imekamata jumla ya kilogramu 3,182 za dawa za kulevya aina ya heroin na methamphetamine katika operesheni maalum iliyofanyika jijini Dar es Salaam na Iringa kati ya tarehe 5 hadi 23 mwezi Disemba, 2023. Watu saba wamekamatwa kuhusika na dawa hizo ambapo wawili kati yao wana asili ya Asia.


Kiasi hiki cha dawa za kulevya kinajumuisha kilogramu 2,180.29 za dawa aina ya methamphetamine na kilogramu 1001.71 aina ya heroin zilizokamatwa katika wilaya za Kigamboni, Ubungo na Kinondoni jijini Dar es Salaam pamoja na wilaya ya Iringa mkoani Iringa.

Ukamataji huu umehusisha kiasi kikubwa cha dawa za kulevya ambacho hakijawahi kukamatwa katika historia ya Tanzania tangu kuanza kwa shughuli za udhibiti wa dawa za kulevya. Hivyo, watuhumiwa waliokamatwa ni miongoni mwa mitandao mikubwa ya wauzaji wa dawa za kulevya inayofuatiliwa nchini na duniani.

Aidha, dawa hizi zilizozikamata zilikuwa zimefungashwa kwenye vifungashio vya bidhaa zenye chapa mbalimbali za kahawa na majani ya chai. Mbinu hii inatumika kwa lengo la kurahisisha usafirishaji wake na kukwepa kubainika.

Ukiacha dawa ya heroin inayotengenezwa kwa mchanganyiko wa kemikali kutoka kwenye mimea ya afyuni (opium popy) inayolimwa katika nchi za Asia na baadhi ya kutoka Amerika, dawa aina ya methamphetamine ni dawa mpya ya kulevya iliyopo katika kundi la vichangamshi sawa na cocaine.

Dawa hii huwa kwenye mfumo wa vidonge, unga au chembechembe mithili ya chumvi ang’avu yenye rangi mbalimbali ambayo huzalishwa kwenye maabara bubu kwa kuchanganya aina mbalimbali za kemikali bashirifu.

Dawa hii ni hatari kwa afya ya mtumiaji, madhara yake ni makubwa na hayatibiti kirahisi kwani mtumiaji hupata madhara ya kudumu kwenye ubongo na hivyo hupunguza uwezo wa kutunza kumbukumbu, kusababisha uraibu na kuathiri mfumo mzima wa fahamu.

Kiasi cha dawa za kulevya zilizokamatwa, endapo zingefanikiwa kuingia mtaani zingeweza kuathiri zaidi ya watu 76,368,000 kwa siku. Hivyo, ukamataji huu umeokoa nguvu kazi ambayo ingeangamia kutokana na madhara yatokanayo na matumizi ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi.

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa a Kulevya, inatoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Mamlaka kwani mafanikio haya yametokana na ushirikiano unaotokana na wananchi wanaotoa taarifa juu ya watu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya ikiwa ni pamoja na weledi na uzalendo mkubwa wa maafisa wa Mamlaka katika udhibiti wa biashara ya dawa za kulevya.

Pia, Mamlaka inatoa onyo kwa wote wanaoendelea kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya hapa nchini kuacha badala yake wajikite kwenye biashara nyingine halali kwani Mamlaka imejizatiti kukomesha biashara ya dawa za kulevya kwa kufanya operesheni katika maeneo mbalimbali nchini.

Aidha,Mamlaka inaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiwezesha Mamlaka katika kutekeleza kazi zake kwa ufanisi mkubwa.

Tukishirikiana, kwa umoja wetu tutaweza kuokoa vizazi vyetu na taifa letu dhidi ya tatizo la dawa za kulevya.









WATUMISHI WA HOSPITALI YA RUFAA BOMBO WAPEWA MKONO WA SIKUU YA CHRISTMAS

December 22, 2023

 


MGANGA Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo Dkt Naima Yusuf kushoto akigawa zawadi za sikukuu ya christmas kwa Muuguzi wa Hospitali hiyo Mwanakombo Hassani mapema leo ikiwa ni utamaduni wao wa kila sikuu kubwa kufanya hivyo.

MGANGA Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo Dkt Naima Yusuf kushoto akigawa zawadi za sikukuu ya christmas kwa Muuguzi wa Hospitali hiyo Mwanakombo Hassani mapema leo ikiwa ni utamaduni wao wa kila sikuu kubwa kufanya hivyo.
MGANGA Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo Dkt Naima Yusuf kushoto akigawa zawadi za sikukuu ya christmas kwa Afisa Takwimu wa Hospitali hiyo Rashid Lukumbuja mapema leo ikiwa ni utamaduni wao wa kila sikuu kubwa kufanya hivyo.
Mmoja wa watumishi akitoka kuchukua zawadi za sikuu ya Christmas mapema leo ambazo zimetolewa na Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo




Sehemu ya watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo wakiwa na zawadi zao za sikuu ya Christmas mapema leo ambao zimetolewa na Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo

Mmoja wa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo akiwa na zawadi zake za sikuu ya Christmas mapema leo ambao zimetolewa na Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo

Sehemu ya Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo wakiwa za zawadi zao za sikuuu ya Christmas ambazo zimetolewa na Uongozi wa Hospitali hiyo
Sehemu ya watumishi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo wakiwa kwenye foleni kuchukua zawadi za sikuu ya Christmas mapema leo ambazo zimetolewa na Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo




Na Oscar Assenga,Tanga

UONGOZI wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo umetoa zawadi za sikuu ya Krismas kwa wafanyakazi wake ikiwa ni utamaduni wao wa kila sikuu kubwa kufanya hivyo.

Zoezi la Ugawaji huo lilifanywa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Dkt Naima Yusuf ambaye alisema ni muhimu wafanyakazi kusherehekea sikuuu kwa amani na utulivu.

Alisema ugawaji wa zawadi hizo ni zoezi ambalo limekuwa likifanyika katika sikuu za Eid na Krismas lengo likiwa ni kutoa motisha kwa watumishi katika Hospitali hiyo.

Aidha aliwataka kuendelea kuchapa kazi kwa waledi na uaminifu mkubwa katika kuwahudumia wagonjwa wanaofika kupataa huduma mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba ya Watumishi wa Kitengo cha Maabara katika Hospitali hiyo Salvatory Lyimo alisema wana mshukuru Mganga Mfawidhi Dkt Naima Yusuf kwa zawadi hiyo aliyowapa wafanyakazi sikuu zitaenda kuwa nzuri endelee kuwa na moyo huo huo kuwajali.

Alisema aliushukuru uongozi kwa zawadi hizo ambazo wamekuwa wakizitoa kila sikuuu wanawalisha Mungu awabariki na kuwapa maisha mazuri.